< Amos 6 >
1 Alas for the careless in Zion, and for them who put confidence in the mountain of Samaria, —the distinguished among the first group of nations, to whom came in the house of Israel.
Ole wenu ninyi mnaostarehe na kuridhika katika Sayuni, na ninyi mnaojisikia salama juu ya Mlima Samaria, ninyi watu mashuhuri wa taifa lililoendelea kuliko mataifa mengine, ambao watu wa Israeli wanawategemea!
2 Pass ye over to Calneh, and see, and go on from thence to Hamath the great, —and go down to Gath of the Philistines, are they better than these kingdoms? or their boundary larger than your boundary?
Nendeni Kalne mkaone kutoka huko; mwende hadi Hamathi iliyo kuu, kisha mshuke hadi Gathi ya Wafilisti. Je, wao ni bora kuliko falme zenu mbili? Je, nchi yao ni kubwa kuliko yenu?
3 Ye who are putting far away the day of calamity, —but bringing near the abode of violence:
Mnaiweka mbali siku iliyo mbaya na kuleta karibu utawala wa kuogofya.
4 Who are lying on beds of ivory, and sprawling on their couch of pleasure, —and eating the well-fed of the flock, and the fatted calves out of the midst of the stalls:
Ninyi mnalala juu ya vitanda vilivyofunikwa kwa pembe za ndovu, na kujinyoosha juu ya viti vya fahari. Mnajilisha kwa wana-kondoo wazuri na ndama walionenepeshwa.
5 Who are bawling at the bidding of the harp, —like David, have they invented for themselves instruments of song:
Ninyi mnapiga vinubi kama Daudi, huku mkitunga nyimbo za vinanda mbalimbali.
6 Who are quaffing bowls of wine, and, with the best of oils, anointing themselves, —and are not afflicted for the injury of Joseph: —
Mnakunywa mvinyo kwa bakuli zilizojazwa, na mnajipaka mafuta mazuri, lakini hamhuzuniki kwa maangamizi ya Yosefu.
7 Therefore, at once, shall they go into exile among the first of the exiles, —so shall be disturbed the revelry of sprawlers.
Kwa hiyo mtakuwa miongoni mwa watu wa kwanza kwenda uhamishoni; karamu zenu na kustarehe kutakoma.
8 Sworn hath the Lord, Yahweh, by his own life, Declareth Yahweh, God of hosts, abhorring am I, the grandeur of Jacob, and, his palaces, I hate, —therefore will I cast off the city and the fulness thereof.
Bwana Mwenyezi ameapa kwa nafsi yake mwenyewe: Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema: “Nachukia kiburi cha Yakobo, nachukia ngome zake; nitautoa mji wao na kila kitu kilichomo ndani mwake.”
9 And it shall come to pass, though there be left remaining ten men in one house, yet shall they die;
Kama watu kumi watabaki katika nyumba moja, wao pia watakufa.
10 And a man’s near of kin, even he who is about to burn the bones, shall carry him out of the house, when he shall say to him that is in the hinder parts of the house—Are there yet any with thee? and he shall say—No one. Then shall he say—Hush! for we must not invoke the name of Yahweh.
Kama jamaa ambaye atachoma miili akija ili kuitoa nje ya nyumba, na kumuuliza yeyote ambaye bado anajificha humo, “Je, yuko mtu yeyote pamoja nawe?” Naye akisema, “Hapana,” ndipo atakaposema, “Nyamaza kimya! Haturuhusiwi kutaja jina la Bwana.”
11 For lo! Yahweh, is giving command, and will smite the great house into ruins, —and the little house with clefts.
Kwa kuwa Bwana ameamuru, naye atabomoa jumba kubwa vipande vipande na nyumba ndogo vipande vidogo vidogo.
12 Shall horses run upon crag? or will a man plough [there] with oxen? For ye have turned to poison the sentence of justice, and the fruit of righteousness, to wormwood:
Je, farasi waweza kukimbia kwenye miamba mikali? Je, aweza mtu kulima huko kwa maksai? Lakini mmegeuza haki kuwa sumu na matunda ya uadilifu kuwa uchungu:
13 Who rejoice in a thing of nought, —who say, Have we not by our own strength, taken to ourselves horns?
ninyi mnaoshangilia kushindwa kwa Lo-Debari na kusema, “Je, hatukuteka Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
14 For behold me! raising up against you, O house of Israel, Declareth Yahweh, the God of hosts—a nation! And they shall crush you, from the entering in of Hamath, unto the torrent-bed of the waste plain.
Maana Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote asema, “Nitainua taifa dhidi yenu, ee nyumba ya Israeli, nalo litawatesa kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bonde la Araba.”