< Acts 13 >

1 Now there were in Antioch, distributed through the existing assembly, —prophets and teachers: both Barnabas and Symeon who was called Niger, and Lucius the Cyrenian, Manaen also, Herod the tetrarch’s foster-brother, and Saul.
Katika kanisa la Antiokia kulikuwa na watu wengine waliokuwa manabii na walimu; miongoni mwao akiwa Barnaba, Simoni aitwaye pia Mweusi, Lukio wa Kurene, Manaeni ambaye alikuwa amelelewa pamoja na mfalme Herode, na Saulo.
2 And, as they were publicly ministering unto the Lord and fasting, the Holy Spirit said—Separate forthwith unto me, Barnabas and Saul, unto the work whereunto I have called them.
Walipokuwa wanafanya ibada yao kwa Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema: “Niteulieni Barnaba na Saulo kwa ajili ya kazi niliyowaitia.”
3 Then, fasting and praying, and laying their hands upon them, they sent them away.
Basi, baada ya kusali na kufunga zaidi, wakawawekea mikono, wakawaacha waende zao.
4 They, therefore, being sent forth by the Holy Spirit, went down unto Seleucia, and, from thence, sailed away unto Cyprus;
Basi, Barnaba na Saulo walipokwisha tumwa na Roho Mtakatifu, walishuka hadi Seleukia, na kutoka huko walipanda meli hadi kisiwa cha Kupro.
5 And, coming to be in Salamis, they declared the word of God in the synagogues of the Jews; —and they had, John also, as an attendant.
Walipofika Salami walihubiri neno la Mungu katika masunagogi ya Kiyahudi. Yohane (Marko) alikuwa msaidizi wao.
6 And, passing through the whole island, as far as Paphos, they found a certain man, a magician, a false-prophet, a Jew, whose name was Bar-jesus;
Walitembea toka upande mmoja wa kisiwa mpaka Pafo upande wa pili, na huko walimkuta mchawi mmoja Myahudi aitwaye Baryesu ambaye alijisingizia kuwa nabii.
7 Who was with the proconsul, Sergius Paulus, an intelligent man. The same, calling for Barnabas and Saul, sought to hear the word of God.
Huyu alikuwa pamoja na Sergio Paulo, mkuu wa kile kisiwa, ambaye alikuwa mtu mwelewa sana. Sergio Paulo aliwaita Barnaba na Saulo ili asikie neno la Mungu.
8 But Elymas the magician, —for so, when translated, is his name, —withstood them; seeking to turn aside the proconsul from the faith.
Lakini huyo mchawi Elima (kama alivyokuwa anaitwa kwa Kigiriki), alijaribu kuwapinga ili kumzuia huyo mkuu wa kisiwa asije akaigeukia imani ya Kikristo.
9 But Saul, who is also Paul, filled with Holy Spirit, looking steadfastly at him,
Basi, Saulo ambaye aliitwa pia Paulo, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alimkodolea macho huyo mchawi,
10 Said—O full of all guile, and all recklessness! Son of an adversary! Enemy of all righteousness!—Wilt thou not cease to pervert the straight ways of the Lord?
akasema, “Mdanganyifu wa kupindukia na mlaghai wewe! Wewe ni mtoto wa Ibilisi! Wewe ni adui wa chochote kile kilicho cha kweli; hukomi hata mara moja kujaribu kuzipotosha njia za Bwana zilizonyoka.
11 Now, therefore, lo! the hand of the Lord is upon thee, and thou shalt be blind, not seeing the sun, until a fitting time. And, instantly, there fell upon him a mist and darkness; and, going about, he was seeking such as might lead him by the hand.
Sasa, mkono wa Bwana utakuadhibu: utakuwa kipofu na hutaweza kuuona mwanga wa jua kwa kitambo.” Mara kila kitu kikawa kama ukungu na giza kwake, akaanza kwenda huku na huku akitafuta mtu wa kumshika mkono amwongoze.
12 Then, the proconsul, seeing what had happened, believed, being amazed at the teaching of the Lord.
Yule mkuu wa kisiwa alipoona hayo, aliongoka akawa muumini; akastaajabia sana mafundisho aliyosikia juu ya Bwana.
13 And, setting sail from Paphos, Paul’s company came into Perga of Pamphylia; but, John, withdrawing from them, returned unto Jerusalem.
Kutoka Pafo, Paulo na wenzake walipanda meli wakaenda hadi Perga katika Pamfulia; lakini Yohane (Marko) aliwaacha, akarudi Yerusalemu.
14 They, however, passing through from Perga, arrived at Antioch of Pisidia; and, going into the synagogue on the sabbath-day, sat down.
Lakini wao waliendelea na safari toka Pisga hadi mjini Antiokia Pisidia. Siku ya Sabato waliingia ndani ya Sunagogi, wakakaa.
15 And, after the reading of the law and the prophets, the synagogue-rulers sent unto them, saying—Brethren! if there is in you a word of exhortation unto the people, say on.
Baada ya masomo katika kitabu cha Sheria ya Mose na katika maandiko ya manabii, wakuu wa lile sunagogi waliwapelekea ujumbe huu: “Ndugu, kama mnalo jambo la kuwaambia watu ili kuwapa moyo, semeni.”
16 And Paul, standing up, and making a sign with his hand, said—Ye men of Israel! and such as revere God! hearken: —
Basi, Paulo alisimama, akatoa ishara kwa mkono, akaanza kuongea: “Wananchi wa Israeli na wengine wote mnaomcha Mungu, sikilizeni!
17 The God of this people Israel, chose our fathers, and, the people, he exalted, by their sojourn in the land of Egypt, —and, with a high arm, brought he them out of it;
Mungu wa taifa hili la Israeli aliwateua babu zetu na kuwafanya wawe taifa kubwa walipokuwa ugenini kule Misri. Mungu aliwatoa huko kwa uwezo wake mkuu.
18 And, for the time of about forty years, bare with their manners in the desert;
Aliwavumilia kwa muda wa miaka arobaini kule jangwani.
19 And, overthrowing seven nations in the land of Canaan, gave them their land as an inheritance—about four hundred and fifty years.
Aliyaangamiza mataifa ya nchi ya Kanaani akawapa hao watu wake ile nchi kuwa mali yao.
20 And, after these things, he gave them judges, until Samuel the prophet.
Miaka mia nne na hamsini ilipita, halafu akawapatia waamuzi wawaongoze mpaka wakati wa nabii Samweli.
21 And, from that time, they asked for themselves a king, and God gave them Saul, son of Kish, a man of the tribe of Benjamin, during forty years;
Hapo wakapendelea kuwa na mfalme, na Mungu akawapa Saulo, mtoto wa Kishi wa kabila la Benyamini, awe mfalme wao kwa muda wa miaka arobaini.
22 And, setting him aside, raised up, David, unto them for king, —of whom he also said, bearing witness—I have found David, the son of Jesse, —[a man] according to my heart, who will do all my will.
Baada ya kumwondoa Saulo, Mungu alimteua Daudi kuwa mfalme wao. Mungu alionyesha kibali chake kwake akisema: Nimemwona Daudi mtoto wa Yese; ni mtu anayepatana na moyo wangu; mtu ambaye atatimiza yale yote ninayotaka kuyatenda.
23 From this man’s seed, hath God, according to promise, brought unto Israel, a saviour—Jesus:
Kutokana na ukoo wake mtu huyu, Mungu, kama alivyoahidi, amewapelekea watu wa Israeli Mwokozi, ndiye Yesu.
24 John, beforehand proclaiming, before the face of his coming in, an immersion of repentance, unto all the people of Israel.
Kabla ya kuja kwake Yesu, Yohane alimtangulia akiwahubiria watu wote wa Israeli kwamba ni lazima watubu na kubatizwa.
25 And, as John was fulfilling his course, he was saying—Whom are ye supposing that I am? I, am not he! But lo! there cometh, after me, one of whom I am not worthy, the sandals of his feet, to loosen.
Yohane alipokuwa anamaliza ujumbe wake aliwaambia watu: Mnadhani mimi ni nani? Mimi si yule mnayemtazamia. Huyo anakuja baada yangu na mimi sistahili hata kuzifungua kamba za viatu vyake.
26 Brethren! sons of the race of Abraham, and those who among you revere God, —unto you, hath this word of salvation been sent forth.
“Ndugu, ninyi mlio watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wengine wote mnaomcha Mungu! Ujumbe huu wa wokovu umeletwa kwetu.
27 For, they who were dwelling in Jerusalem, and their rulers, not recognising him, have, by judging him, fulfilled, the very voices of the prophets which every sabbath are being read;
Kwa maana wenyeji wa Yerusalemu na wakuu wao hawakumtambua yeye kuwa Mwokozi. Wala hawakuelewa maneno ya manabii yanayosomwa kila Sabato. Hata hivyo, waliyafanya maneno ya manabii yatimie kwa kumhukumu Yesu adhabu ya kifo.
28 And, though no single cause of death they found, yet claimed they of Pilate that he should be slain.
Ingawa hawakumpata na hatia inayostahili auawe, walimwomba Pilato amhukumu auawe.
29 And, when they had finished all those things which, concerning him, had been written, taking him down from the tree, they put him in a tomb.
Na baada ya kutekeleza yote yaliyokuwa yameandikwa kumhusu yeye, walimshusha kutoka msalabani, wakamweka kaburini.
30 But, God, raised him from among the dead:
Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
31 Who appeared, during many days, unto them who had come up with him from Galilee unto Jerusalem; who, indeed, [now] are his witnesses unto the people.
Naye, kwa siku nyingi aliwatokea wale waliofuatana naye kutoka Galilaya mpaka Yerusalemu. Hao ndio walio sasa mashahidi wake kwa watu wa Israeli.
32 We, therefore, unto you, bring the good news, as to the promise which, unto our fathers, was made, —
Sisi tumekuja hapa kuwaleteeni Habari Njema: jambo lile Mungu alilowaahidia babu zetu amelitimiza sasa kwa ajili yetu sisi tulio wajukuu wao kwa kumfufua Yesu kutoka wafu.
33 That God hath fulfilled, the same, for our children, by raising up Jesus: as also, in the second psalm, it is written—My son, art, thou: I, this day, have begotten thee.
Kama ilivyoandikwa katika zaburi ya pili: Wewe ni Mwanangu, mimi leo nimekuwa baba yako.
34 And, in that he raised him from among the dead, no more destined to return unto corruption, on this wise hath he spoken—I will give unto you the faithful lovingkindnesses of David.
Na juu ya kumfufua kutoka wafu, asipate tena kurudi huko na kuoza, Mungu alisema hivi: Nitakupa baraka takatifu na za kweli nilizomwahidia Daudi.
35 Wherefore also, in a different [place], he saith—Thou wilt not give thy man of lovingkindness to see corruption.
Naam, na katika sehemu nyingine za zaburi asema: Hutamwacha Mtakatifu wako aoze.
36 For, David, indeed, unto his own generation having done service, by the counsel of God, fell asleep, and was added unto fathers, and saw corruption;
Sasa, Daudi mwenyewe alitimiza mapenzi ya Mungu wakati wake; kisha akafa na kuzikwa karibu na wazee wake, na mwili wake ukaoza.
37 But, he whom God hath raised, did not see corruption.
Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu hakupata kuoza.
38 Be it known unto you, therefore, brethren, —that, through this man, unto you, remission of sins is declared;
Jueni wazi, ndugu zangu, kwamba ujumbe kuhusu kusamehewa dhambi unahubiriwa kwenu kwa njia ya Yesu Kristo;
39 And, from all things from which ye could not, by the law of Moses, be justified, by this man, everyone that believeth, is justified.
na ya kwamba kila mmoja anayemwamini Yesu anasamehewa dhambi zote, jambo ambalo halingewezekana kwa njia ya Sheria ya Mose.
40 Be taking heed, therefore, lest that come upon you which hath been spoken in the prophets—
Jihadharini basi, msije mkapatwa na yale yaliyosemwa na manabii:
41 See, ye despisers, and marvel, and disappear: in that, a work, am, I, working in your days, —a work, which in nowise will ye believe, though one relate it in full unto you.
Sikilizeni enyi wenye madharau, shangaeni mpotee! Kwa maana kitu ninachofanya sasa, nyakati zenu, ni kitu ambacho hamtakiamini hata kama mtu akiwaelezeni.”
42 And, as they were going out, they kept on beseeching that, on the ensuing sabbath, might be spoken unto them these things.
Paulo na Barnaba walipokuwa wanatoka katika ile sunagogi, wale watu waliwaalika waje tena siku ya Sabato iliyofuata, waongee zaidi juu ya mambo hayo.
43 And, when the congregation was broken up, there followed many of the Jews, and of the devout proselytes, with Paul and Barnabas; who, indeed, in speaking unto them, went on persuading them to abide in the favour of God.
Mkutano huo ulipomalizika, Wayahudi wengi na watu wa mataifa mengine waliokuwa wameongokea dini ya Kiyahudi waliwafuata Paulo na Barnaba. Hao mitume waliongea nao, wakawatia moyo waendelee kuishi wakitegemea neema ya Mungu.
44 And, on the coming sabbath, almost all the city, was gathered together, to hear the word of God.
Siku ya Sabato iliyofuata, karibu kila mtu katika ule mji alikuja kusikiliza neno la Bwana.
45 But, the Jews, seeing, the multitudes, were filled with jealousy, —and began speaking against the things which, by Paul, were being spoken, defaming them.
Lakini Wayahudi walipoliona hilo kundi la watu walijaa wivu, wakapinga alichokuwa anasema Paulo na kumtukana.
46 And Paul and Barnabas, speaking boldly, said—Unto you, was it necessary, that the word of God should first be spoken: seeing ye are thrusting it from you, and, unworthy, are judging yourselves of the age-abiding life, lo! we turn unto the nations; (aiōnios g166)
Hata hivyo, Paulo na Barnaba waliongea kwa uhodari zaidi, wakasema, “Ilikuwa ni lazima neno la Mungu liwafikieni ninyi kwanza; lakini kwa kuwa mmelikataa na kujiona hamstahili uzima wa milele, basi, tunawaacheni na kuwaendea watu wa mataifa mengine. (aiōnios g166)
47 For so hath the Lord commanded us—I have set thee for a light of nations, that thou mayest be for salvation unto the end of the earth.
Maana Bwana alituagiza hivi: Nimekuteua wewe uwe mwanga kwa mataifa, uwe njia ya wokovu kwa ulimwengu wote.”
48 And they of the nations, hearing [this], began to rejoice, and to be glorifying God, and they believed—as many as had become disposed for life age-abiding. (aiōnios g166)
Watu wa mataifa mengine waliposikia jambo hilo walifurahi, wakausifu ujumbe wa Mungu; na wale waliokuwa wamechaguliwa kupata uzima wa milele, wakawa waumini. (aiōnios g166)
49 And the word of the Lord went on to be carried through the whole country.
Neno la Bwana likaenea kila mahali katika sehemu ile.
50 But, the Jews, urged on the devout women of the higher class, and the chief men of the city, and roused up a persecution against Paul and Barnabas, —and thrust them out from their bounds.
Lakini Wayahudi waliwachochea wanawake wa tabaka ya juu wa mataifa mengine ambao walikuwa wacha Mungu, na wanaume maarufu wa mji huo. Wakaanza kuwatesa Paulo na Barnaba, wakawafukuza kutoka katika eneo lao.
51 But they, shaking off the dust of their feet against them, came into Iconium.
Basi, mitume wakayakung'uta mavumbi yaliyokuwa katika miguu yao kama onyo, kisha wakaenda Ikonio.
52 And, the disciples, were filled with joy, and with Holy Spirit.
Lakini hao wafuasi walikuwa wamejaa furaha na Roho Mtakatifu.

< Acts 13 >