< Acts 13 >
1 Now there were in Antioch, distributed through the existing assembly, —prophets and teachers: both Barnabas and Symeon who was called Niger, and Lucius the Cyrenian, Manaen also, Herod the tetrarch’s foster-brother, and Saul.
Sasa katika kanisa la Antiokia, palikuwa na baadhi ya manabii na walimu. Walikua Barnaba, Simeoni (aliyeitwa Nigeri). Lukio wa Kirene, Manaeni( ndugu asiye wa damu wa Herode kiongozi wa mkoa), na Sauli.
2 And, as they were publicly ministering unto the Lord and fasting, the Holy Spirit said—Separate forthwith unto me, Barnabas and Saul, unto the work whereunto I have called them.
Walipokuwa wakimwabudu Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema, “Niteengeeni pembeni Barnaba na Sauli, waifanye kazi niliyo waitia.”
3 Then, fasting and praying, and laying their hands upon them, they sent them away.
Baada ya Kanisa kufunga, kuomba, na kuweka mikono yao juu ya watu hawa, wakawaacha waende.
4 They, therefore, being sent forth by the Holy Spirit, went down unto Seleucia, and, from thence, sailed away unto Cyprus;
Kwa hiyo Barnabas na Sauli walimtii Roho Mtakatifu na walitelemka kuelekea Seleukia; Kutoka huko walisafiri baharini kuelekea kisiwa cha Kipro.
5 And, coming to be in Salamis, they declared the word of God in the synagogues of the Jews; —and they had, John also, as an attendant.
Walipokuwa katika mji wa Salami, walilitangaza neno la Mungu katika Masinagogi ya Wayahudi. Pia walikuwa pamoja na Yohana Marko kama msaidizi wao.
6 And, passing through the whole island, as far as Paphos, they found a certain man, a magician, a false-prophet, a Jew, whose name was Bar-jesus;
Walipokwenda katika kisiwa chote mpaka Pafo, walikuta mtu fulani mchawi, Myahudi nabii wa uongo, ambaye jina lake lilikuwa Bar Yesu.
7 Who was with the proconsul, Sergius Paulus, an intelligent man. The same, calling for Barnabas and Saul, sought to hear the word of God.
Mchawi huyu alishirikiana na Liwali Sergio Paulus, aliyekuwa mtu mwenye akili. Mtu huyu aliwaalika Barnaba na Sauli, kwa sababu alihitaji kusikia neno la Mungu.
8 But Elymas the magician, —for so, when translated, is his name, —withstood them; seeking to turn aside the proconsul from the faith.
Lakini Elima “yule mchawi” (hivyo ndivyo jina lake lilivyo tafsiriwa) aliwapinga; alijaribu kumgeuza yule liwali atoke kwenye imani.
9 But Saul, who is also Paul, filled with Holy Spirit, looking steadfastly at him,
Lakini Sauli aliyeitwa Paulo, alikuwa amejazwa na Roho Mtakatikfu, akamkazia macho
10 Said—O full of all guile, and all recklessness! Son of an adversary! Enemy of all righteousness!—Wilt thou not cease to pervert the straight ways of the Lord?
na akasema “Ewe mwana wa Ibilisi, umejazwa na aina zote za udanganyifu na udhaifu. Wewe ni adui wa kila aina ya haki. Hautakoma kuzigeuza njia za Bwana, zilizonyooka, je utaweza?
11 Now, therefore, lo! the hand of the Lord is upon thee, and thou shalt be blind, not seeing the sun, until a fitting time. And, instantly, there fell upon him a mist and darkness; and, going about, he was seeking such as might lead him by the hand.
Sasa tazama, mkono wa Bwana upo juu yako, na utakuwa kipofu. Hautaliona Jua kwa muda” mara moja ukungu na giza vilianguka juu ya Elimas; alianza kuzunguka pale akiomba watu wamwongoze kwa kumshika mkono.
12 Then, the proconsul, seeing what had happened, believed, being amazed at the teaching of the Lord.
Baada ya liwali kuona kilichotokea, aliamini, kwa sababu alishangazwa kwa mafundisho kuhusu Bwana.
13 And, setting sail from Paphos, Paul’s company came into Perga of Pamphylia; but, John, withdrawing from them, returned unto Jerusalem.
Sasa Paulo na rafiki zake walisafiri majini kutoka Pafo na wakafika Perge katika Pamfilia. Lakini Yohana aliwaacha na kurudi Yerusalemu.
14 They, however, passing through from Perga, arrived at Antioch of Pisidia; and, going into the synagogue on the sabbath-day, sat down.
Paulo na rafiki yake walisafiri kutoka Perge na wakafika Antiokia ya Pisidia. Huko walikwenda katika sinagogi siku ya Sabato na kukaa chini.
15 And, after the reading of the law and the prophets, the synagogue-rulers sent unto them, saying—Brethren! if there is in you a word of exhortation unto the people, say on.
Baada ya kusoma sheria na manabii, viongozi wa sinagogi aliwatumia ujumbe wakisema, “Ndugu, kama mnao ujumbe wa kutia moyo watu hapa, semeni”
16 And Paul, standing up, and making a sign with his hand, said—Ye men of Israel! and such as revere God! hearken: —
Kwa hiyo Paulo alisimama na kuwapungia mkono; alisema, “Wanaume wa Israeli na enyi mnao mtii Mungu, sikilizeni.
17 The God of this people Israel, chose our fathers, and, the people, he exalted, by their sojourn in the land of Egypt, —and, with a high arm, brought he them out of it;
Mungu wa hawa watu wa Israeli aliwachagua baba zetu na kuwafanya watu wengi walipokaa katika nchi Misri, na kwa mkono wake kuinuliwa aliwaongoza nje yake.
18 And, for the time of about forty years, bare with their manners in the desert;
Kwa miaka arobaini aliwavumilia katika jangwa.
19 And, overthrowing seven nations in the land of Canaan, gave them their land as an inheritance—about four hundred and fifty years.
Baada ya kuyaharibu mataifa saba katika nchi ya Kaanani, aliwapa watu wetu nchi yao kwa urithi.
20 And, after these things, he gave them judges, until Samuel the prophet.
Matukio haya yote yalitokea zaidi ya miaka mia nne na hamsini. Baada ya vitu hivi vyote, Mungu aliwapa waamuzi mpaka Samweli Nabii.
21 And, from that time, they asked for themselves a king, and God gave them Saul, son of Kish, a man of the tribe of Benjamin, during forty years;
Baada ya haya, watu waliomba mfalme, hivyo Mungu aliwapa Sauli mwana wa Kishi, mtu wa kabila la Benjamini, kuwa mfalme kwa miaka arobaini.
22 And, setting him aside, raised up, David, unto them for king, —of whom he also said, bearing witness—I have found David, the son of Jesse, —[a man] according to my heart, who will do all my will.
Kisha baada ya Mungu kumuondoa katika ufalme, alimwinua Daudi kuwa mfalme wao. Ilikuwa ni kuhusu Daudi kwamba Mungu alisema, 'Nimempata Daudi mwana wa Yese kuwa mtu apendezwaye na moyo wangu; ambaye atafanya kila kitu nipendacho.'
23 From this man’s seed, hath God, according to promise, brought unto Israel, a saviour—Jesus:
Kutoka kwenye ukoo wa mtu huyu Mungu ameiletea Israeli mkombozi, Yesu, kama alivyoahidi kufanya.
24 John, beforehand proclaiming, before the face of his coming in, an immersion of repentance, unto all the people of Israel.
Hili lilianza kutokea, kabla ya Yesu kuja, Yohana kwanza alitangaza ubatizo wa toba kwa watu wote wa Israeli.
25 And, as John was fulfilling his course, he was saying—Whom are ye supposing that I am? I, am not he! But lo! there cometh, after me, one of whom I am not worthy, the sandals of his feet, to loosen.
Naye Yohana alipokuwa akimalizia kazi yake, alisema, 'Mwanifikiri mimi ni nani? mimi si yule. Lakini sikilizeni, ajaye nyuma yangu, sisitahili kulegeza viatu vya miguu yake.'
26 Brethren! sons of the race of Abraham, and those who among you revere God, —unto you, hath this word of salvation been sent forth.
Ndugu, watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wale ambao kati yenu mnamwabudu Mungu, ni kwa ajili yetu kwamba ujumbe huu wa ukombozi umetumwa.
27 For, they who were dwelling in Jerusalem, and their rulers, not recognising him, have, by judging him, fulfilled, the very voices of the prophets which every sabbath are being read;
Kwa wale waishio Yerusalemu, na watawala wao, hawakumtambua kwa uhalisia, na wala hawakuutambua ujumbe wa manabii ambao husomwa kila Sabato; kwa hiyo walitimiliza ujumbe wa manabii kwa kumhukumu kifo Yesu.
28 And, though no single cause of death they found, yet claimed they of Pilate that he should be slain.
Japokuwa hawakupata sababu nzuri kwa kifo ndani yake, walimwomba Pilato amuue.
29 And, when they had finished all those things which, concerning him, had been written, taking him down from the tree, they put him in a tomb.
Walipomaliza mambo yote yaliyoandikwa kuhusu yeye, walimshusha kutoka mtini na kumlaza kaburini.
30 But, God, raised him from among the dead:
Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
31 Who appeared, during many days, unto them who had come up with him from Galilee unto Jerusalem; who, indeed, [now] are his witnesses unto the people.
Alionekana kwa siku nyingi kwa wale waliokwenda pamoja naye kutoka Galilaya kuelekea Yerusalemu. Watu hawa sasa ni mashahidi wa watu.
32 We, therefore, unto you, bring the good news, as to the promise which, unto our fathers, was made, —
Hivyo tunawaletea habari njema kuhusu ahadi walizopewa mababu zetu.
33 That God hath fulfilled, the same, for our children, by raising up Jesus: as also, in the second psalm, it is written—My son, art, thou: I, this day, have begotten thee.
Mungu aliweka ahadi hizi kwetu, watoto wao, katika hilo alimfufua Yesu na kumrudisha tena katika uhai. Hili pia liliandikwa katika Zaburi ya pili: 'Wewe ni Mwanangu, leo nimekuwa Baba yako'
34 And, in that he raised him from among the dead, no more destined to return unto corruption, on this wise hath he spoken—I will give unto you the faithful lovingkindnesses of David.
Pia kuhusu ukweli ni kwamba alimfufua kutoka wafu ili kwamba mwili wake usiharibike, ameongea hivi: 'Nitakupatia utakatifu na baraka halisi za Daudi'
35 Wherefore also, in a different [place], he saith—Thou wilt not give thy man of lovingkindness to see corruption.
Hii ndiyo sababu kasema pia katika zaburi nyingine, 'Hautaruhusu mtakatifu wako kuuona uozo.'
36 For, David, indeed, unto his own generation having done service, by the counsel of God, fell asleep, and was added unto fathers, and saw corruption;
Kwa kuwa baada ya Daudi kutumikia mapenzi ya Mungu katika kizazi chake, alilala, alilazwa pamoja na baba zake, na aliuona uaharibifu,
37 But, he whom God hath raised, did not see corruption.
Lakini aliyefufuliwa na Mungu hakuuona uharibifu.
38 Be it known unto you, therefore, brethren, —that, through this man, unto you, remission of sins is declared;
Hivyo na ifahamike kwenu, ndugu, kupitia mtu huyu, msamaha wa dhambi umehubiriwa.
39 And, from all things from which ye could not, by the law of Moses, be justified, by this man, everyone that believeth, is justified.
Kwa yeye kila aaminiye anahesabiwa haki na mambo yote ambayo sheria ya Musa isingewapatia haki.
40 Be taking heed, therefore, lest that come upon you which hath been spoken in the prophets—
Hivyo basi kuweni waangalifu kwamba kitu walichokiongelea manabii kisitokee kwenu:
41 See, ye despisers, and marvel, and disappear: in that, a work, am, I, working in your days, —a work, which in nowise will ye believe, though one relate it in full unto you.
'Tazama, enyi mnaodharau, na mkashangae na mkaangamie; kwa vile nafanya kazi katika siku zenu, Kazi ambayo hamwezi kuiamini, hata kama mtu atawaeleza.”
42 And, as they were going out, they kept on beseeching that, on the ensuing sabbath, might be spoken unto them these things.
Wakati Paulo na Barnaba walipoondoka, watu wakawaomba waongee maneno haya siku ya Sabato ijayo.
43 And, when the congregation was broken up, there followed many of the Jews, and of the devout proselytes, with Paul and Barnabas; who, indeed, in speaking unto them, went on persuading them to abide in the favour of God.
Wakati mkutano wa sinagogi ulipokwisha, Wayahudi wengi na waongofu thabiti waliwafuata Paulo na Barnaba, ambao waliongea nao na waliwahimiza waendelee katika neema ya Mungu.
44 And, on the coming sabbath, almost all the city, was gathered together, to hear the word of God.
Sabato iliyofuata, karibu mji mzima ulikusanyika kusikia neno la Mungu.
45 But, the Jews, seeing, the multitudes, were filled with jealousy, —and began speaking against the things which, by Paul, were being spoken, defaming them.
Wayahudi walipoona makutano, walijawa na wivu na kuongea maneno yaliyopinga vitu vilivyosemwa na Paulo na walimtukana.
46 And Paul and Barnabas, speaking boldly, said—Unto you, was it necessary, that the word of God should first be spoken: seeing ye are thrusting it from you, and, unworthy, are judging yourselves of the age-abiding life, lo! we turn unto the nations; (aiōnios )
Lakini Paulo na Barnaba waliongea kwa ujasiri na kusema, “Ilikuwa ni muhimu kwamba neno la Mungu liongelewe kwanza kwenu. Kwa kuwa mnalisukumia mbali kutoka kwenu nakujiona kuwa hamkusitahili uzima wa milele, angalieni tutawageukia Mataifa. (aiōnios )
47 For so hath the Lord commanded us—I have set thee for a light of nations, that thou mayest be for salvation unto the end of the earth.
Kama ambavyo Bwana ametuamuru, akisema, 'Nimewaweka ninyi kama nuru kwa watu wa mataifa, kwamba mlete wokovu kwa pande zote za dunia.”
48 And they of the nations, hearing [this], began to rejoice, and to be glorifying God, and they believed—as many as had become disposed for life age-abiding. (aiōnios )
Mataifa waliposikia hili, walifurahi na kulisifu neno la Bwana. Wengi waliochaguliwa kwa uzima wa milele waliamini. (aiōnios )
49 And the word of the Lord went on to be carried through the whole country.
Neno la Bwana lilienea nchi yote.
50 But, the Jews, urged on the devout women of the higher class, and the chief men of the city, and roused up a persecution against Paul and Barnabas, —and thrust them out from their bounds.
Lakini wayahudi waliwasihi waliojitoa na wanawake muhimu, pia na viongozi wa mji. Haya yalichochea mateso dhidi ya Paulo na Barnaba na waliwatupa nje ya mipaka ya mji.
51 But they, shaking off the dust of their feet against them, came into Iconium.
Lakini Paulo na Barnaba walikung'uta vumbi ya miguu yao. Kisha walienda kwenye mji wa Ikonia.
52 And, the disciples, were filled with joy, and with Holy Spirit.
Na wanafunzi walijawa na furaha pamoja na Roho mtakatifu.