< 3 John 1 >
1 The elder, unto Gaius the beloved, whom, I, love in truth.
Mzee, kwa Gayo mpenzi, ninayempenda katika kweli.
2 Beloved! concerning all things, I pray thou mayest be prospering, and be in health, even as, thy soul, is prospering,
Mpendwa, nakuombea ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya njema, kama vile roho yako inavyofanikiwa.
3 For I rejoiced exceedingly, at brethren coming and bearing witness unto thy truth, —even as, thou, in truth, art walking.
Maana nilifurahi sana wakati nilipoambiwa na ndugu waliokuja na kutoa ushuhuda juu ya kweli yako, kama vile unavyoenenda katika kweli.
4 I have no, greater, favour than these things, that I should be hearing that, my own children, in the truth, are walking.
Sina furaha kubwa zaidi ya hii, kusikia kwamba watoto wangu wanatembea katika kweli.
5 Beloved! a faithful thing, art thou doing, whatsoever thou shalt accomplish for them that are brethren, and withal strangers, —
Mpendwa, unaenenda kwa uaminifu unapowahudumia ndugu na wageni,
6 Who have borne witness to thy love before the assembly: whom thou wilt do, nobly, to set forward worthily of God.
ambao wametoa ushuhuda wa upendo wako mbele ya kanisa. Unafanya vizuri kuwasafirisha katika safari zao kwa namna ambayo inampendeza Mungu.
7 For, in behalf of The Name, have they gone forth, taking, nothing, from them of the nations.
Kwa sababu kwa ajili ya Jina, walienda bila kuchukua kitu chochote kutoka kwa watu wa Mataifa.
8 We, therefore ought to be sustaining such as these, that we may become, fellowworkers, with the truth.
Hivyo, tunatakiwa kuwakaribisha watu kama hawa, ili tuwe watenda kazi wenza kwa ajili ya kweli.
9 I wrote something unto the assembly; but, he who is fond of taking the first place among them—Diotrephes, doth not make us welcome.
Nililiandikia kusanyiko jambo fulani, lakini Diotrofe, anayependa kuwa wa kwanza miongoni mwao, hakubaliani na sisi.
10 For this cause, if I come, I will bring to remembrance his works which he is doing, —with wicked words, prating against us; and, not content with these, he neither, himself, maketh the brethren welcome, but, them who are minded [to do it], he forbiddeth, and, out of the assembly, doth cast [them].
Hivyo, kama nikija nitayakumbuka matendo yake anayoyafanya, jinsi anavyosema maneno mabaya kinyume nasi. Hajaridhika na matendo haya, yeye mwenyewe hawapokei ndugu. Hata huwakataza wengine ambao wanatamani kuwakaribisha hao ndugu na kuwafukuza watoke kwenye kusanyiko.
11 Beloved! be not thou imitating what is bad, but what is good. He that doeth good, is, of God: he that doeth what is bad, hath not seen God.
Mpenzi, usiige kilicho kibaya, bali iga kilicho chema. Yeye atendaye mema ni wa Mungu; na yeye atendaye mabaya hajamwona Mungu.
12 Unto Demetrius, hath witness been borne by all and by the truth itself; howbeit, we also, bear witness, and thou knowest that, our witness, is, true.
Demetrio ameshuhudiwa na wote na kweli yenyewe. sisi pia ni mashahidi, na unajua kuwa ushahuhuda wetu ni wa kweli.
13 Many things, had I to write unto thee, —but I am unwilling, with ink and pen, to be writing;
Ninayo mambo mengi ya kukuandikia, lakini sipendi kukuandikia kwa kalamu na wino.
14 I hope, however, straightway, to see thee, and, mouth to mouth, will we talk. Peace be unto thee. The friends salute thee. Salute the friends by name.
Bali ninatarajia kukuona hivi karibuni, na tutaongea nawe ana kwa ana. Amani iwe pamoja nawe. Marafiki wanakusalimu. Wasalimu marafiki kila mmoja kwa jina lake.