< 2 Samuel 10 >

1 And it came to pass, after this, that the king of the sons of Ammon died, —and that Hanun his son reigned in his stead.
Baada ya muda, mfalme wa Waamoni akafa, naye Hanuni mwanawe akaingia mahali pake.
2 Then said David—I will shew lovingkindness unto Hanun son of Nahash, as his father shewed, unto me, lovingkindness. So David sent to comfort him, by the hand of his servants, as to his father, —and the servants of David came into the land of the sons of Ammon.
Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kama vile baba yake alivyonitendea mimi wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe kuonyesha wema wake kwa Hanuni kuhusu baba yake. Watu wa Daudi walipofika katika nchi ya Waamoni,
3 Then said the rulers of the sons of Ammon unto Hanun their lord—Is David honouring thy father, in thine eyes, that he hath sent unto thee comforters? Is it not, for the sake of exploring the city, and spying it out, and overthrowing it, that David hath sent his servants unto thee?
wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni bwana wao, “unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kukutumia watu ili kuonyesha masikitiko? Je, Daudi hakuwatuma watu hawa kuchunguza na kuupeleleza mji ili kuupindua?”
4 Wherefore Hanun took David’s servants, and shaved off half their beards, and cut off their upper garments in the middle, as far as their buttocks, —and let them go.
Basi Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa kila mmoja ndevu zake nusu, akakata mavazi yao nyuma katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
5 And, when they told David, he sent to meet them, because the men were greatly ashamed, —and the king said—Tarry at Jericho, until your beards be grown, then shall ye return.
Daudi alipoambiwa jambo hili, akatuma wajumbe ili kwenda kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote ndipo mje.”
6 And, when the sons of Ammon saw that they had made themselves odious with David, the sons of Ammon sent and hired the Syrians of Beth-rehob, and the Syrians of Zoba—twenty thousand footmen, and of king Maacah—a thousand men, and men of Tob—twelve thousand men.
Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, wakaajiri askari wa miguu 20,000 Waaramu kutoka Beth-Rehobu na Soba, pia mfalme wa Maaka pamoja na watu 1,000, na vilevile watu 12,000 kutoka Tobu.
7 And, when David heard of it, he sent Joab and all the army of heroes,
Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
8 And the sons of Ammon came out, and set in array for battle, at the entrance of the gate, —whereas, the Syrians of Zoba, and of Rehob, and the men of Tob and of Maacah, were by themselves, in the field.
Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati Waaramu wa Soba, wa Rehobu, watu wa Tobu na Maaka walikuwa peke yao kwenye eneo la wazi.
9 And, when Joab saw that the front of the battle was towards him, before and behind, he chose out of all the chosen men of Israel, and set them in array against the Syrians;
Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
10 while, the rest of the people, he delivered into the hand of Abishai his brother, —and set [them] in array against the sons of Ammon.
Akawaweka waliobaki chini ya uongozi wa Abishai nduguye na kuwapanga dhidi ya Waamoni.
11 And he said—If the Syrians be too strong for me, then shalt thou become my deliverance, —but, if, the sons of Ammon, be too strong for thee, then will I come with deliverance to thee.
Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itawabidi mje kunisaidia. Lakini kama Waamoni watawazidi nguvu, basi nitakuja kuwasaidia.
12 Be strong, and let us put forth our strength, for the sake of our people, and for the sake of the cities of our God, —and, Yahweh, do what is good in his own eyes.
Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
13 And Joab drew nigh, and the people that were with him, to fight against the Syrians, —and they fled before him.
Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
14 And, when, the sons of Ammon, saw that the Syrians had fled, then fled they before Abishai, and entered the city, —so Joab returned from the sons of Ammon, and entered Jerusalem.
Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao wakakimbia mbele ya Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi kutoka kupigana na Waamoni na kufika Yerusalemu.
15 And, when the Syrians saw that they were defeated before Israel, they gathered themselves together;
Baada ya Waaramu kuona wameshindwa na Israeli, wakajikusanya tena.
16 and Hadadezer sent and brought out the Syrians that were beyond the River, and they entered Helam, —Shobach the prince of the host of Hadadezer being before them.
Hadadezeri akaagiza Waaramu walioletwa kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakaenda Helamu pamoja na Shobaki jemadari wa jeshi la Hadadezeri akiwaongoza.
17 And, when it was told David, he gathered together all Israel, and passed over the Jordan, and entered Helam, —and the Syrians set themselves in array to meet David, and fought with him.
Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote, wakavuka Mto Yordani, wakaenda Helamu. Waaramu wakapanga vikosi vyao vya askari kukabiliana na kupigana dhidi ya Daudi.
18 Then fled the Syrians before Israel, and David slew of the Syrians seven hundred chariots, and forty thousand horsemen, —Shobach also, prince of their host, smote he, that he died, there.
Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari mia saba na askari wao wa miguu 40,000. Vilevile alimpiga Shobaki jemadari wa jeshi lao, naye akafa huko.
19 And, when all the kings who were servants to Hadadezer saw that they were defeated before Israel, they made peace with Israel, and served them, —and the Syrians feared to give help any more unto the sons of Ammon.
Wafalme wote waliokuwa wanamtumikia Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya amani na Waisraeli na wakawa chini yao. Hivyo Waaramu wakaogopa kuwasaidia Waamoni tena.

< 2 Samuel 10 >