< 2 Kings 22 >

1 Eight years old, was Josiah when he began to reign, and, thirty-one years, reigned he in Jerusalem, —and, this mother’s name, was Jedidah daughter of Adaiah, of Bozkath.
Yosia alikuwa na miaka minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka thelathini na mmoja. Mama yake aliitwa Yedida binti Adaya, kutoka Boskathi.
2 And he did that which was right in the eyes of Yahweh, —and walked in all the way of David his father, and turned not aside, to the right hand or to the left.
Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana na kuenenda katika njia zote za Daudi baba yake. Hakugeuka upande wa kuume wala wa kushoto.
3 And it came to pass, in the eighteenth year of King Josiah, that the king sent Shaphan son of Azaliah son of Meshullam, the scribe, to the house of Yahweh, saying—
Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wake, Mfalme Yosia akamtuma mwandishi Shafani mwana wa Azalia, mwana wa Meshulamu, kwenda katika Hekalu la Bwana. Akasema:
4 Go up unto Hilkiah, the high priest, that he pour out the silver that hath been brought into the house of Yahweh, —which the keepers of the entrance-hall have gathered from the people,
“Panda uende kwa Hilkia, kuhani mkuu, umwambie ahesabu zile fedha ambazo zimeletwa katika Hekalu la Bwana, ambazo mabawabu wamekusanya kutoka kwa watu.
5 that they may give it into the hand of the doers of the work, who have oversight of the house of Yahweh, that they may give it to the doers of the work, who are in the house of Yahweh, to repair the breaches of the house;
Waambie waikabidhi kwa watu walioteuliwa kusimamia kazi ya Hekalu. Waamuru watu hawa wawalipe wafanyakazi ambao wanakarabati Hekalu la Bwana:
6 to the carpenters, and to the builders, and to the masons, —and to buy timber, and hewn stones, for repairing the house.
wale maseremala, wajenzi na waashi. Waambie pia wanunue mbao na mawe yaliyochongwa ili kukarabati Hekalu.
7 Howbeit there used to be no reckoning made with them, as to the silver that was given into their hand, —because, with faithfulness, were they dealing.
Lakini hawahitajiki kutoa hesabu ya fedha walizokabidhiwa, kwa sababu wanafanya kwa uaminifu.”
8 Then said Hilkiah the high priest, unto Shaphan the scribe—The book of the law, have I found, in the house of Yahweh. So Hilkiah delivered the book unto Shaphan, and he read it.
Hilkia kuhani mkuu akamwambia Shafani mwandishi, “Nimekipata Kitabu cha Sheria ndani ya Hekalu la Bwana.” Akampa Shafani, ambaye alikisoma.
9 Then came Shaphan the scribe unto the king, and brought the king word again, —and said—Thy servants have poured out the silver that was found in the house, and have delivered it unto the hand of the doers of the work, who have oversight of the house of Yahweh.
Kisha Shafani mwandishi akamwendea mfalme na kumpa taarifa akisema: “Maafisa wako wametoa ile fedha ambayo ilikuwa ndani ya Hekalu la Bwana na imekabidhiwa mikononi mwa wasimamizi wa marekebisho ya Hekalu.”
10 Then Shaphan the scribe told the king, saying—A book, hath Hilkiah the priest delivered unto me. And Shaphan read it before the king.
Ndipo Shafani mwandishi akampasha mfalme habari kwamba: “Hilkia kuhani amenipa kitabu hiki.” Naye Shafani akakisoma kile kitabu mbele ya mfalme.
11 And it came to pass, when the king heard the words of the book of the law, that he rent his clothes.
Mfalme aliposikia maneno ya kile Kitabu cha Sheria, akararua mavazi yake.
12 And the king commanded Hilkiah the priest, and Ahikam son of Shaphan, and Achbor son of Micaiah, and Shaphan the scribe, and Asaiah the king’s servant, saying:
Akatoa maagizo haya kwa Hilkia kuhani, Ahikamu mwana wa Shafani, Akbori mwana wa Mikaya, Shafani mwandishi, na Asaya mtumishi wa mfalme:
13 Go ye—enquire of Yahweh, for me and for the people, and for all Judah, concerning the words of this book which hath been found, —for, great, is the wrath of Yahweh, in that it hath fired up against us, because our fathers have not hearkened unto the words of this book, to do according to all which is written concerning us.
“Nendeni mkamuulize Bwana kwa ajili yangu, na kwa ajili ya watu na Yuda wote kuhusu yale yaliyoandikwa ndani ya kitabu hiki ambacho kimepatikana. Hasira ya Bwana ni kubwa inayowaka dhidi yetu kwa sababu baba zetu hawakuyatii maneno ya kitabu hiki. Hawajatenda kulingana na yale yote yaliyoandikwa humo kutuhusu sisi.”
14 So Hilkiah the priest, and Ahikam, and Achbor, and Shaphan, and Asaiah, went unto Huldah the prophetess, wife of Shallum son of Tikvah, son of Harhas keeper of the vestments, she having her dwelling in Jerusalem, in the new city, —and they spake unto her.
Hilkia kuhani, Ahikamu, Akbori, Shafani na Asaya wakaenda kuongea na nabii mke Hulda, ambaye alikuwa mke wa Shalumu mwana wa Tikwa, mwana wa Harhasi mtunzaji wa chumba cha mavazi. Hulda aliishi Yerusalemu katika Mtaa wa Pili.
15 And she said unto them, Thus, saith Yahweh, God of Israel, Say ye unto the man who hath sent you unto me:
Akawaambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: Mwambieni yule mtu aliyewatuma ninyi kwangu,
16 Thus, saith Yahweh, Behold me! about to bring calamity upon this place, and upon the inhabitants thereof, —all the words of the book, which, the king of Judah, hath read:
‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Nitaleta maafa juu ya mahali hapa na watu wake, kulingana na kila kitu kilichoandikwa katika kitabu hicho mfalme wa Yuda alichosoma.
17 Because they have forsaken me, and burned incense unto other gods, that they might provoke me to anger, with all the workmanship of their hands; and so my wrath shall fire up against this place, and shall not be quenched:
Kwa sababu wameniacha mimi na kufukiza uvumba kwa miungu mingine, na kunighadhibisha kwa sanamu zote zilizotengenezwa kwa mikono yao, hasira yangu itawaka dhidi ya mahali hapa, wala haitatulizwa.’
18 But, unto the king of Judah, who hath sent you to enquire of Yahweh, thus, shall ye say unto him, —Thus, saith Yahweh, God of Israel, As touching the words which thou hast heard:
Mwambieni mfalme wa Yuda, ambaye amewatuma kumuuliza Bwana, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli, kuhusu maneno uliyoyasikia:
19 Because, tender, was thy heart, and thou didst humble thyself before Yahweh when thou heardest what I had spoken against this place and against the inhabitants thereof—that they should become a desolation and a curse, and didst rend thy clothes, and weep before me, therefore also, I, have hearkened—declareth Yahweh.
Kwa kuwa moyo wako ulikuwa msikivu na ulijinyenyekeza mbele za Bwana uliposikia kile nilichosema dhidi ya mahali hapa na watu wake, kwamba wangelaaniwa na kuachwa ukiwa, basi kwa sababu uliyararua mavazi yako na kulia mbele zangu, nimekusikia, asema Bwana.
20 For this cause, behold me! about to gather thee unto thy fathers, and thou shalt be gathered unto thy graves, in peace, and so thine eyes shall not look upon all the misfortune which I am about to bring upon this place. And they brought the king word again.
Kwa hiyo nitakukusanya kwa baba zako, nawe utazikwa kwa amani. Macho yako hayataona maafa yote nitakayoleta juu ya mahali hapa.’” Basi wakapeleka jibu lake kwa mfalme.

< 2 Kings 22 >