< 2 Chronicles 4 >
1 And he made an altar of bronze, twenty cubits, the length thereof, and, twenty cubits, the breadth thereof, —and, ten cubits, the height thereof.
Mfalme Solomoni akatengeneza madhabahu ya shaba yenye urefu wa dhiraa ishirini, upana wa dhiraa ishirini na kimo chake dhiraa kumi.
2 And he made a molten sea, —ten—by the cubit, from the one brim thereof into the other brim thereof, it was round all about, and, five—by the cubit, was the height thereof, and, a line—of thirty by the cubit, did compass it round about.
Akatengeneza Bahari ya kusubu, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Kamba ya urefu wa dhiraa thelathini ingeweza kuizunguka.
3 And, the likeness of oxen, was under it round about on every side, encircling it, ten in a cubit, going round the sea, on every side, -two rows of oxen, made in the casting.
Chini ya huo ukingo, kulikuwa na mafahali kuizunguka, yaani mafahali kumi katika kila dhiraa moja. Hayo mafahali waliyasubu katika safu mbili yakiwa ya kitu kimoja na hiyo Bahari.
4 It was standing on twelve oxen, three, looking toward the north, and, three, looking toward the west, and, three, looking toward the south, and, three, looking toward the east, the sea, being upon them above, —and, all their hinder parts, inward.
Bahari hiyo ilikaa juu ya mafahali kumi na wawili, mafahali watatu walielekeza nyuso zao kaskazini, watatu magharibi, watatu kusini na watatu mashariki. Bahari hiyo ilikaa juu ya hao mafahali, nazo sehemu zao za nyuma zilielekeana.
5 And, the thickness thereof, was a hand-breadth, and, the brim thereof, was like the brim-work of a cup, with blossoms of lilies, —it could hold [many] baths, three thousand, would it contain.
Unene wake ulikuwa nyanda nne, na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 3,000.
6 And he made ten lavers, and set five on the right hand—and five on the left, to bathe therein, what is offered as an ascending-sacrifice, do they rinse therein, —but, the sea, was, that the priests should bathe therein.
Kisha akatengeneza masinia kumi kwa ajili ya kuoshea vifaa, naye akayaweka matano upande wa kusini na matano upande wa kaskazini. Ndani yake ndimo walioshea vifaa vya kutumika katika sadaka za kuteketezwa, lakini ile Bahari ilikuwa ni kwa ajili ya makuhani kunawia.
7 And he made ten lampstands of gold according to the regulation thereof, —and set in the temple, five, on the right hand, and, five, on the left.
Akatengeneza vinara vya taa kumi vya dhahabu kama ilivyoainishwa kwao na kuviweka hekaluni, vinara vitano upande wa kusini na vitano upande wa kaskazini.
8 And he made ten tables, and placed in the temple, five, on the right hand, and, five, on the left, —and he made a hundred tossing bowls of gold.
Akatengeneza meza kumi na kuziweka hekaluni, tano upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Pia akatengeneza mabakuli 100 ya dhahabu ya kunyunyizia.
9 And he made the court of the priests, and the large enclosure, —and doors to the enclosure, and, the doors thereof, overlaid he with bronze.
Akatengeneza ukumbi wa makuhani na ukumbi mwingine mkubwa na milango yake, naye akaifunika hiyo milango kwa shaba.
10 And, the sea, he set on the right side of the house, eastward over against the south.
Akaweka ile Bahari upande wa kusini, kwenye pembe ya kusini mashariki ya nyumba.
11 And Huram made—the pans, and the shovels, and the tossing bowls, —and Huram finished doing the work, which he did for King Solomon, in the house of God: —
Pia akatengeneza masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi katika Hekalu la Mungu kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:
12 two pillars, and the bowls and the capitals on the top of the two pillars, and the two frames of checker work, to cover the two bowls of the capitals, which were on the top of the pillars;
zile nguzo mbili; yale mataji mawili yaliyokuwa juu ya hizo nguzo, zile nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli yaliyowekwa juu ya zile nguzo;
13 and four hundred pomegranates, for the two frames, -two rows of pomegranates, for each frame, for covering the two bowls of the capitals, which were on the face of the pillars;
yale makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);
14 and, the stands, made he, —and, the lavers, made he upon the stands;
vishikio pamoja na masinia yake;
15 the one sea, —and the twelve oxen under it;
hiyo Bahari na hao mafahali kumi na wawili chini yake;
16 and, the pans and the shovels and the flesh-hooks, and all the vessels, made Huram his father for King Solomon, for the house of Yahweh, —of burnished bronze,
pia hayo masufuria, masepetu, uma za nyama na vyombo vingine vyote vilivyohusiana. Vitu vyote ambavyo Huramu-Abi alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyosuguliwa.
17 In the circuit of the Jordan, did the king cast them, in the clay ground between Succoth and Zeredah.
Mfalme aliagiza wavisubu vitu hivi kwenye kalibu za udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani kati ya Sukothi na Sereda.
18 So Solomon made all these utensils, in great abundance, —for the weight of the bronze could not be searched out.
Vitu hivi vyote Mfalme Solomoni alivyotengeneza vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.
19 Yea Solomon made all the utensils which were for the house of God, —and the altar of gold, and the tables, whereon was the Presence-bread;
Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu: madhabahu ya dhahabu; meza za kuweka mikate ya Wonyesho;
20 and the lamp-holders and their lamps, that they should burn according to the regulation before the shrine, of purified gold;
vinara vya taa vya dhahabu safi pamoja na taa zake ili ziwake mbele ya sehemu takatifu ya ndani kama ilivyoelekezwa;
21 and the blossom-work, and the lamps, and the tongs, of gold, —the same, was the purest gold;
maua ya dhahabu yaliyofanyizwa, taa na makoleo (vilikuwa vya dhahabu bora kabisa);
22 and the snuffers and the bowls and the spoons and the censers, of purified gold, —and the entrance of the house, the inner doors thereof for the holy of holies, and the doors of the house of the temple, were of gold.
mikasi ya dhahabu safi, mabakuli ya kunyunyizia, masinia na vyetezo; milango ya dhahabu ya Hekalu: yaani milango ya ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, na milango ya ukumbi mkuu.