< 2 Chronicles 26 >

1 Then all the people of Judah took Uzziah, when, he, was sixteen years old, —and made him king, instead of his father Amaziah.
Kisha watu wote wa Yuda wakamtwaa Uzia, aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, nao wakamfanya mfalme mahali pa Amazia baba yake.
2 He, built Eloth, and restored it to Judah, —after that the king slept with his fathers.
Ndiye alijenga upya Elathi kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
3 Sixteen years old, was Uzziah, when he began to reign, and, fifty-two years, reigned he in Jerusalem, -and, the name of his mother, was Jechiliah, of Jerusalem.
Uzia alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
4 And he did that which was right, in the eyes of Yahweh, —according to all that Amaziah his father had done.
Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
5 And it came to pass that he set himself to seek God, in the days of Zechariah, who gave understanding in the seeing of God, —and, throughout the days of his seeking Yahweh, God, prospered him.
Akamtafuta Mungu katika siku za Zekaria, aliyemwelekeza kumcha Mungu. Wakati wote alipomtafuta Bwana, Mungu alimfanikisha.
6 So he went forth and made war against the Philistines, and brake down the wall of Gath, and the wall of Jabneh, and the wall of Ashdod, —and built cities in Ashdod, and among the Philistines.
Alipigana vita dhidi ya Wafilisti na kubomoa kuta za Gathi, Yabne na Ashdodi. Kisha akajenga upya miji karibu na Ashdodi na mahali pengine katikati ya Wafilisti.
7 And God helped him against the Philistines and against the Arabians who dwelt in Gur-baal, and the Meunim.
Mungu akamsaidia dhidi ya Wafilisti na dhidi ya Waarabu walioishi Gur-Baali na dhidi ya Wameuni.
8 And the Ammonites gave a present to Uzziah, —and his name went forth as far as the entering in of Egypt, for he shewed exceeding great strength.
Waamoni wakamletea Uzia ushuru, umaarufu wake ukaenea hadi kwenye mpaka wa Misri, kwa sababu alikuwa amekuwa na nguvu sana.
9 And Uzziah built towers, in Jerusalem, over the corner-gate, and over the valley-gate, and over the angle, —and he made them strong.
Uzia akajenga minara huko Yerusalemu katika Lango la Pembeni, katika Lango la Bondeni na katika pembe, mahali kuta zikutanapo, kisha akaijengea ngome.
10 And he built towers in the desert, and digged many wells, for, much cattle, had he, both in the lowland, and in the plain, —husbandmen and vinedressers, in the mountains and in the fruitful field, for, a lover of the soil, was he.
Akajenga pia minara jangwani na kuchimba visima vingi vya maji, kwa sababu alikuwa na mifugo mingi chini ya vilimani na kwenye nchi tambarare. Alikuwa na watu wanaofanya kazi katika mashamba yake na kwenye mashamba yake ya mizabibu huko vilimani na katika ardhi zenye rutuba, kwa kuwa aliupenda udongo.
11 And it came to pass that Uzziah had a force ready to make war, to go forth as a host in company, by the number of their reckoning, under the direction of Jeiel the scribe, and Maaseiah the officer, —under the direction of Hananiah, from among the captains of the king.
Zaidi ya hayo, Uzia alikuwa na jeshi lililofunzwa vizuri, lililokuwa tayari kwenda vitani kwa vikosi kufuatana na idadi yao kama walivyokusanywa na Yeieli mwandishi na Maaseya msimamizi chini ya maelekezo ya Hanania, mmojawapo wa maafisa wa mfalme.
12 The whole number of the ancestral chiefs pertaining to the heroes of valour, was two thousand and six hundred;
Idadi yote ya viongozi wa jamaa waliowaongoza hawa wapiganaji walikuwa 2,600.
13 and, under their direction, was the force of a host, three hundred and seven thousand five hundred, ready to make war, with the strength of a force, —for helping the king against an enemy.
Chini ya uongozi wao kulikuwa na jeshi la askari 307,500 watu waliofundishwa kwa ajili ya vita, jeshi lenye nguvu la kumsaidia mfalme dhidi ya adui zake.
14 And Uzziah prepared for them, for all the host, bucklers and spears and helmets, and coats of mail, and bows, —and yea even sling-stones.
Uzia akalipatia jeshi lote ngao, mikuki, chapeo, dirii, pinde na mawe ya kombeo.
15 And he made in Jerusalem, inventions invented of the inventor, to be upon the towers and upon the turrets, for throwing with arrows, and with great stones, —so that his name went forth afar, for he was marvellously helped, until that he was strong.
Huko Yerusalemu watu wenye utaalamu mkubwa wakatengeneza mitambo iliyotumika katika minara na kwenye pembe za ulinzi ili kurusha mishale na kuvurumisha mawe makubwa. Sifa zake zikaenea mbali sana kwa sababu alisaidiwa mno mpaka akawa na nguvu sana.
16 But, when he became strong, uplifted was his heart, unto ruin, for he acted unfaithfully against Yahweh his God, —and entered into the temple of Yahweh, to burn incense upon the altar of incense.
Lakini baada ya Uzia kuwa na nguvu sana, majivuno yake yakamsababishia kuanguka. Alikosa uaminifu kwa Bwana Mungu wake, naye akaingia hekaluni mwa Bwana ili afukize uvumba kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba.
17 Then entered after him, Azariah the priest, —and with him eighty priests of Yahweh, sons of valour;
Azaria kuhani akiwa pamoja na makuhani wengine themanini wa Bwana wenye ujasiri wakamfuata huko ndani.
18 and they took their stand against Uzziah the king, and said unto him-It is not, for thee, O Uzziah, to burn incense unto Yahweh, but, for the priests, the sons of Aaron, who are hallowed, to burn incense. Go forth out of the sanctuary, for thou hast acted unfaithfully, and, not to thee, for an honour, [shall it be] from Yahweh Elohim.
Wakamkabili na kumwambia, “Siyo sawa kwako, Uzia, kumfukizia Bwana uvumba. Hiyo ni kazi ya makuhani, wazao wa Aroni, ambao wamewekwa wakfu ili kufukiza uvumba. Ondoka mahali patakatifu, kwa kuwa umekosa uaminifu nawe hutaheshimiwa na Bwana.”
19 Then was Uzziah wroth, and, in his hand, was a censer, to burn incense, —and, when he was wroth with the priests, a leprosy, shot forth in his forehead, before the priests, in the house of Yahweh, from off the altar of incense.
Uzia, ambaye alikuwa na chetezo mkononi mwake tayari kufukiza uvumba, akakasirika. Alipokuwa anawaghadhibikia makuhani mbele ya madhabahu ya kufukizia uvumba katika Hekalu la Bwana, ukoma ukamtokea penye kipaji chake cha uso.
20 When Azariah the chief priest and all the priests turned towards him, lo! he, was leprous, in his forehead, so they hastened him from thence, —yea, even he himself, hurried to go out, because Yahweh had smitten him.
Azaria kuhani mkuu pamoja na makuhani wengine wote walipomtazama wakaona kwamba alikuwa na ukoma penye kipaji chake cha uso wakaharakisha kumtoa nje. Naam, hata yeye mwenyewe alikuwa anatamani kuondoka kwa sababu Bwana alikuwa amempiga.
21 And it came to pass that, Uzziah the king, was a leper until the day of his death, and dwelt in a house apart—a leper, for he was cut off from the house of Yahweh, —and, Jotham his son, was over the house of the king, judging the people of the land.
Mfalme Uzia alikuwa na ukoma mpaka siku ya kufa kwake. Akatengwa katika nyumba ya pekee akiwa mwenye ukoma, naye akawa ametengwa kutoka Hekalu la Bwana. Yothamu mwanawe akawa msimamizi wa jumba la mfalme, pia akawaongoza watu wa nchi.
22 Now, the rest of the story of Uzziah, first and last, hath Isaiah son of Amoz, the prophet, written.
Matukio mengine ya utawala wa Uzia, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa na nabii Isaya mwana wa Amozi.
23 And Uzziah slept with his fathers, and they buried him with his fathers in the field of burial that pertained unto the kings, for they said, A leper, he is. And Jotham his son reigned in his stead.
Uzia akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika shamba la kuzikia lililokuwa mali ya wafalme, kwa kuwa watu walisema, “Alikuwa na ukoma.” Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Chronicles 26 >