< 1 Timothy 2 >
1 I exhort, therefore, first of all, that there be made—supplications, prayers, intercessions, thankgivings, in behalf of all men,
Kwanza kabisa, basi naomba dua, sala, maombi na sala za shukrani zitolewe kwa Mungu kwa ajili ya watu wote,
2 In behalf of kings, and all them who are, in eminent station; in order that, an undisturbed, and quiet life, we may lead, in all godliness and gravity:
kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema.
3 This, is comely and acceptable before our Saviour God,
Jambo hili ni jema na lampendeza Mungu Mwokozi wetu,
4 Who willeth, all men, to be saved, and, unto a personal knowledge of truth, to come;
ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli.
5 For there is, one, God, one, mediator also, between God and men, —a man—Christ Jesus:
Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu,
6 Who gave himself a ransom in behalf of all, —the testimony, in its own fit times:
ambaye alijitoa mwenyewe kuwakomboa watu wote. Huo ulikuwa uthibitisho, wakati ufaao ulipowadia.
7 Unto which, I, have been appointed proclaimer and apostle—Truth I speak, I utter no falsehood—a teacher of nations, in faith and truth.
Kwa sababu hiyo mimi nilitumwa niwe mtume na mwalimu wa watu wa mataifa, niutangaze ujumbe wa imani na ukweli. Nasema ukweli; sisemi uongo!
8 I am minded, therefore, that—the men in every place be offering prayer, uplifting hands of lovingkindness, apart from anger and disputings;
Basi, popote mnapokutana kufanya ibada nataka wanaume wasali, watu waliojitolea kweli na ambao wanaweza kuinua mikono yao wakisali bila hasira wala ubishi.
9 In the same way, that, the women, in seemly attire, with modesty and sober-mindedness, be adorning themselves, —not with plaitings and ornamentation of gold, or with pearls, or with costly apparel, —
Hali kadhalika, nawataka wanawake wawe wanyofu na wenye busara kuhusu mavazi yao; wavae sawasawa na si kwa urembo wa mitindo ya kusuka nywele, kujipamba kwa dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
10 But, which becometh women promising godliness, through means of good works.
bali kwa matendo mema kama iwapasavyo wanawake wamchao Mungu.
11 Let, a woman, in quietness, be learning in all submission;
Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza.
12 But, teaching—unto a woman, I do not permit, nor yet to have authority over a man, —but to be in quietness;
Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya.
13 For, Adam, first was formed, then Eve,
Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.
14 And, Adam, was not deceived, whereas, the woman, having been wholly deceived, hath come to be, in transgression;
Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu.
15 She shall be saved, however, through means of the child-bearing, —if they abide in faith, and love, and holiness, with sobermindedness. Faithful, the saying.
Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu.