< 1 Kings 13 >

1 And lo! a man of God, came in out of Judah, by the word of Yahweh, unto Bethel, —as Jeroboam was standing by the altar, to make a perfume.
Mtu wa Mungu alikuja tokea Yuda kwa neno la BWANA kule Betheli. Naye Yeroboamu alikuwa amesimama karibu na madhabahu ili kufukiza uvumba.
2 And he made proclamation against the altar, by the word of Yahweh, and said, O altar! altar! Thus, saith Yahweh, —Lo! a son to be born unto the house of David, Josiah his name, who shall sacrifice upon thee the priests of the high-places, who are making a perfume upon thee, and, human bones, shall be burned upon thee;
Akalia kinyume na zile madhabahu kwa neno la BWANA: “Ee madhabahu, madhabahu” hivi ndivyo asemavyo BWANA, 'Tazama, mwana aitwaye Yosia atazaliwa katika familia ya Daudi, na juu yenu atawachinja makuhani ambao sasa wanafukiza uvumba mahali hapa pa juu kwa ajili yako. Juu yako watachoma mifupa ya watu.'”
3 and he shall give, on that day, a sign, saying, This, is the sign of which Yahweh hath spoken, —Lo! the altar, is to be rent, and the ashes that are upon thee shall be, poured out!
Kisha mtu wa Mungu akatoa ishara siku hiyohiyo, akisema, “Hii ndiyo isharaya kwamba BWANA amesema: 'Tazama, madhabahu zitavuunjika, na majivu yaliyo juu yatamwagika.”
4 And it came to pass, when the king heard the word of the man of God which he proclaimed against the altar in Bethel, Jeroboam thrust forth his hand, from off the altar, saying—Lay hold of him! and his hand which he had thrust forth against him was dried up, that he could not draw it back to him.
Naye mfalme aliposikia kile mtu wa Mungu alichosema, kwamba amelia kinyume cha zile madhabahu kule Betheli, Yeroboamu akanyosha mkono wake kutoka madhabahuni, akisema, “mkamateni.” Ndipo ule mkono aliokuwa ameunyosha dhidi ya mtu wa Mungu ukakauka, kiasi kwamba hakuweza kuurudisha mwenyewe.
5 Moreover, the altar, was rent, and the ashes poured out from the altar, —according to the sign which the man of God had given, by the word of Yahweh.
Na ile madhabahu ikavunjika vipande vipande, na yale majivu yakamwagika kutoka madhabahuni, kama ilivyokuwa imefafanuliwa kuwa ndiyo ishara ya kwamba mtu wa Mungu alikuwa amepewa kwa neno la BWANA.
6 Then responded the king and said unto the man of God—Appease, I pray thee, the face of Yahweh thy God, and pray for me, that my hand may be restored unto me. So the man of God appeased the face of Yahweh, and the hand of the king was restored unto him, and became as aforetime.
Mfalme Yeroboamu akajibu akimwambia mtu wa Mungu, “Msihi BWANA, Mungu wako akupe neema ili uniombee, ili kwamba mkono wangu urejee kwangu tena.” Kwa hiyo mtu wa Mungu akamwomba BWANA, na mkono wa mfalme ukarejea katika hali yake tena, na ukawa kama ulivyokuwa mwanzoni.
7 Then spake the king unto the man of God, Come home with me, and refresh thyself, —and let me give thee a present.
Yule mfalme akamwambia mtu wa Mungu, “twende nyumbani kwangu upate chakula, nami nitakupa zawadi.”
8 But the man of God said unto the king—If thou wouldst give me the half of thy house, I would not go in with thee, —neither would I eat bread or drink water, in this place;
Yule mtu wa Mungu akamwambia mfalme, “Hata kama utanipa nusu ya miliki yako. staende na wewe, wala sitakula au kunywa maji mahali hapa,
9 for, so, he charged me, by the word of Yahweh, saying, Thou shalt not eat bread, nor shalt thou drink water, —neither shalt thou come back by the way thou wentest.
kwa sababu BWANA ameniamuru kwa neno lake, 'hutakula mkate wala kunywa maji, wala kurudi kwa njia ulioijia.'”
10 So he departed another way, —and went not back by the way by which he came unto Bethel.
Kwa hiyo mtu wa Mungu akaondoka na hakurudi nyumbani kwa njia aliyokuja nayo huko Betheli.
11 But, a certain aged prophet, was dwelling in Bethel, —whose sons came in and related to him all the deeds which the man of God had done that day in Bethel—and the words which he had spoken unto the king, and they related them to their father.
Sasa kulikuwa na nabii mwingine mzee aliyekuwa akiishi Betheli, na mmoja wa wana wake akaja kumwambia mambo yote ambayo mtu wa Mungu amefanya siku hiyo kule Betheli. Wana wake wakamwambia pia maneno ambayo Yule mtu wa Mungu alimwambia mfalme.
12 And their father said unto them, Which way then went he? Now his sons had seen the way which the man of God went who had come in out of Judah.
Baba yao akawaambia, “Alienda kwa njia gani?” Wale wanawe walikuwa wamemwona yule mtu wa Mungu kutoka Yuda njia aliyotumia kurudi.
13 So he said unto his sons, Saddle for me, the ass. And they saddled for him the ass, and he rode thereon;
Kwa hiyo akawaambia wanawe, “Nitandikeni punda.” Kwa hiyo wakamtandikia punda naye akampanda.
14 and went after the man of God, and found him, sitting under an oak. And he said unto him—Art, thou, the man of God who came in out of Judah? And he said—I am.
Yule nabii mzee akamfuata yule mtu wa Mungu na akamkuta amekaa chini ya mti wa mwaloni; akamwambia, “Je, wewe ndiye mtu wa Mungu aliyetoka Yuda?” Naye akamjibu, “Mimi ndiye.”
15 Then said he unto him, Come home with me, —and eat bread.
Kisha yule nabii mzee akamwambia, “twende nyumbani kwangu ukale chakula.”
16 And he said—I may not return with thee, nor go in with thee, —neither will I eat bread or drink water with thee, in this place;
Yule mtu wa Mungu akamjibu, “Siwezi kurudi na wewe wala kuingia ndani na wewe, tena sitakula chakula wala kunywa maji pamoja na wewe mahali hapa,
17 for there came a message unto me by the word of Yahweh, Thou shalt neither eat bread, nor drink water there, —thou shalt not turn back to come by the way by which thou wentest.
kwa sababu niliamuriwa hivyo kwa neno la BWANA, 'Hautakula chakula wala kunywa maji kule, wala kurudi kwa njia utakayokuja nayo.'”
18 And he said to him-I also, am a prophet, like unto thee, and, a messenger, hath spoken unto me, by the word of Yahweh, saying—Bring him back with thee, into thy house, that he may eat bread, and drink water. He deceived him.
Kwa hiyo yule nabii mzee akamwambia, “Mimi pia ni nabii kama ulivyo, na malaika amesema na mimi neno la BWANA, akisema, 'Mrudishe aje na wewe katika nyumba yako, ili aweze kula chakula na kunywa maji.'” Lakini alikuwa anamdanganya mtu wa Mungu.
19 So he went back with him, and did eat bread in his house, and drank water.
Kwa hiyo yule mtu wa Mungu akarudi pamoja na yule nabii mzee na akala chakula nyumbani kwake na akanywa maji.
20 And so it was, as, they, were sitting at the table, yea, so it was, that the word of Yahweh came unto the prophet who had brought him back;
Walipokuwa wamekaa mezani, neno la BWANA likamjia yule nabii aliyemrudisha,
21 and he cried out unto the man of God who had come in out of Judah, saying, Thus, saith Yahweh, —Forasmuch as thou hast rebelled against the bidding of Yahweh, and hast not kept the commandment which Yahweh thy God commanded thee;
naye akalia kwa mtu wa Mungu aliyetoka Yuda, akisema “BWANA anasema, 'Kwa kuwa umeshindwa kutii nenola BWANA na umeshindwa kuishika amri ya BWANA ambayo Mungu wako alikupa,
22 but hast returned, and eaten bread and drunk water, in the place of which he said unto thee, Thou mayest neither eat bread nor drink water: thy dead body shall not enter the burying-place of thy fathers.
bali umerudi na umekula chakula na kunywa maji mahali ambapo BWANA alikwambia usile chakula wala kunywa maji, basi mwili wako hautazikwa kwenye makaburi ya baba zako.'”
23 And it came to pass, after he had eaten bread, and after he had drunk, that he saddled for him the ass, for the prophet whom he had brought back.
Baada ya kula chakula na kunywa maji, Yule nabii akatandika punda wa mtu wa Mungu, yule mtu aliyerudi naye.
24 And, when he had gone, there met him a lion by the way, and slew him, —and his dead body was cast out in the way, and, the ass, was standing near it, and, the lion, was standing near the dead body.
Baada ya mtu wa Mungu kuondoka, akakutana na simba njiani na kumwua barabarani, na mwili wake uliachwa barabarani. Na yule punda akasimama pembeni yake, na yule simba naye akasimama pembeni ya ule mwili.
25 And lo! certain men, passing by, saw the dead body, cast out in the way, and the lion standing near the dead body, —so they came in, and spake [of it] in the city, wherein, the aged prophet, dwelt.
Watu walipopita na kuuona ule mwili umeachwa barabarani, na yule simba akisimama karibu na ule mwili, walikuja wakaeleza habari hiyo mjini kule ambako yule nabii mzee aliishi.
26 And, when the prophet who had brought him back from the way heard of it, he said—The man of God, it is, who rebelled against the bidding of Yahweh, —therefore did Yahweh deliver him unto the lion, and it hath torn him and slain him, according to the word of Yahweh which he spake unto him.
Yule nabii aliyemrudisha toka njiani aliposikia, akasema, “Yeye mtu wa Muugu ndiye aliyeshindwa kutii neno la BWANA. Kwa hiyo BWANA alimtoa kwa simba, ambaye amemrarua katika vipande vipande na kumwua, kama vile neno la BWANA lilivyokuwa limemwonya.”
27 And he spake unto his sons, saying, Saddle for me the ass. And they saddled it.
Kwa hiyo yule nabii mzee akawaamnbia wanawe, akisema, “Tandikeni punda wangu,” nao wakamtandikia.
28 So he went and found his dead body, cast out in the way, with, the ass and the lion, standing near the dead body, —the lion had neither eaten the dead body, nor had it torn the ass.
Akaenda akaukuta mwili umeachwa barabarani, punda na simba wamesimama pembeni ya ule mwili. Yule simba hakuula ule mwili, wala hakumshambulia yule punda.
29 And the prophet took up the dead body of the man of God, and laid it upon the ass, and brought it back, —and the aged prophet came into the city, to make lamentation, and to bury him.
Yule nabii akauchukua ule mwili wa mtu wa Mungu, akaulaza juu ya punda, na akaurudisha. Akaja kwenye mji wake kuomboleza na kuuzika.
30 And he laid his dead body in his own grave, —and they lamented over him, [saying] —Alas, my brother!
Akaulaza mwili kwenye kaburi lake, nao wakamwombolezea, wakisema, “Aa! ndugu yangu!”
31 And it came to pass, after he had buried him, that he spake unto his sons, saying, When I die, then shall ye bury me in the grave wherein the man of God is buried; beside his bones, lay my bones;
Kisha baada ya kumzika, yule nabii mzee akawaambia wanawe, akasema, “Nitakapokufa, mtanizika kwenye kaburi ambalo tumemzika mtu wa Mungu. Mtalaza mifupa yangu pembeni mwa mifupa yake.
32 For the message which he proclaimed, by the ward of Yahweh, against the altar which is in Bethel, —and against all the houses of the high places which are in the cities of Samaria, shall surely come to pass.
Kwa kuwa ule ujumbe uliosemwa na BWANA, dhidi ya madhabahu kule Betheli na dhidi ya nyumba zote za mahali pa juu katika mji wa Samaria, hakika yatatokea.
33 After this thing, Jeroboam turned not from his wicked way, —but again made, from the whole compass of the people, priests of high places, whomsoever he would, he installed, and he became priest of high places.
Baada ya haya Yeroboamu hakuuacha uovu wake, aliendelea kuchagua makuhani wa kawaida kwa ajili ya mahali pa juu kutoka kwa watu wa kila aina. Yeyote ambaye angeweza kutumika alimtakasa kuwa kuhani.
34 And so this thing became the sin of the house of Jeroboam, —that it should be both taken away and destroyed, from off the face of the ground.
Jambo hili likawa dhambi kwenye familia ya Yeroboamu na kusababisha familia yake kuangamizwa na kuondolewa kabisa katika uso wa dunia.

< 1 Kings 13 >