< 1 Corinthians 5 >

1 On all hands, there is reported to be among you—fornication, and such fornication as this—which, not among the nations, [is found], —as that one should have, his father’s wife: —
Ziko habari za kuaminika kwamba kuna uzinzi miongoni mwenu; tena ni uzinzi mbaya ambao haujapata kuwako hata kati ya watu wasiomjua Mungu. Nimeambiwa eti mmoja wenu anaishi na mke wa baba yake!
2 And, ye, have become puffed up, and have not rather mourned, in order that he might be removed out of your midst, who, this deed, hath wrought.
Mnawezaje kujivuna? Ingekuwa afadhali kwenu kuomboleza, na huyo aliyefanya kitu hicho aondolewe miongoni mwenu.
3 For, I, indeed, —being absent in the body, but present in the spirit, have already judged, as present, him who, thus, this thing hath perpetrated: —
Nami, kwa upande wangu, ingawa kwa mwili niko mbali nanyi, hata hivyo kwa roho niko hapo pamoja nanyi: na hivyo, kama vile nipo hapo, nimekwisha mhukumu huyo aliyefanya jambo hilo la aibu.
4 In the name of our Lord Jesus, ye being gathered together, and my spirit, with the power of our Lord Jesus,
Wakati mnapokusanyika pamoja kwa jina la Bwana Yesu, nami nikiwa pamoja nanyi kwa roho, basi, kwa uwezo wa Bwana wetu Yesu,
5 To deliver such a one as this, unto Satan, for the destruction of the flesh, —that, the spirit, may be saved in the day of the Lord.
mkabidhini mtu huyo kwa Shetani ili mwili wake uharibiwe na roho yake iweze kuokolewa Siku ile ya Bwana.
6 Unseemly, is your boast! Know ye not that, a little leaven, doth leaven, the whole of the lump?
Majivuno yenu hayafai! Je, hamjui kwamba chachu kidogo huchachusha donge lote la unga?
7 Purge ye out the old leaven, that ye may be a new lump, —even as ye are unleavened; for, our passover, hath even been sacrificed—Christ:
Jitakaseni, mkatupe mbali chachu ya kale ili mpate kuwa donge jipya lisilotiwa chachu kama mnavyopaswa kuwa; maana, Kristo, Pasaka yetu, amekwisha tolewa tambiko.
8 So then, let us be keeping the feast, not with old leaven, nor with leaven of baseness and wickedness, —but with the unleavened bread of sincerity and truth.
Basi, tufanye karamu hiyo si kwa chachu ile ya kale, chachu ya ubaya na uovu, bali kwa mkate usiotiwa chachu, mkate wa usafi na kweli.
9 I wrote unto you in my letter—not to be mixing yourselves up with fornicators; —
Niliwaandikia katika barua yangu msishirikiane na wazinzi.
10 Not at all, [meaning] the fornicators of this world, or the covetous and extortioners, or idolaters, —else had ye been obliged, in that case, to go out of the world!
Ukweli ni kwamba sikuwa na maana ya watu wote duniani walio wazinzi, wachoyo, walaghai na wenye kuabudu sanamu. Maana, ili kuwaepa hao wote ingewalazimu ninyi kuihama dunia hii kabisa!
11 But, now, I have written unto you not to be mixing yourselves up, —if anyone named a brother, be a fornicator, or covetous, or an idolater, or a reviler, or a drunkard, or an extortioner, with such a one as this, not so much, as to be eating together,
Nilichoandika ni hiki: msishirikiane na ndugu Mkristo aliye mzinzi, mchoyo, mwenye kuabudu sanamu, mchongezi mlevi na mlaghai. Mtu wa namna hiyo, hata kula msile naye.
12 For what have I to do to be judging them who are without? Do, ye, not judge, them who are within,
Je, ni shauri langu kuwahukumu watu walio nje? Hao Mungu atawahukumu. Je, ninyi hampaswi kuwahukumu wale walio katika jamii yenu ninyi wenyewe?
13 Whereas, them who are without, God, judgeth? Remove ye the wicked man from among, yourselves.
Mfukuzeni mbali nanyi huyo mwovu!

< 1 Corinthians 5 >