< 1 Chronicles 9 >

1 And, all Israel, registered themselves, and lo! they are written, in the Book of the Kings of Israel, and, Judah, was carried away captive to Babylon, for their faithlessness.
Waisraeli wote waliorodheshwa katika koo zilizoandikwa kwenye kitabu cha wafalme wa Israeli. Watu wa Yuda walichukuliwa mateka kwenda Babeli kwa sababu ya kukosa uaminifu kwa Mungu.
2 Now, the first inhabitants, who were in their possessions, in their cities, were Israel, the priests, the Levites, and the Nethinim.
Basi watu wa kwanza kurudi kukaa kwenye milki zao katika miji yao walikuwa baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi na watumishi wa Hekalu.
3 And, in Jerusalem, there dwelt, of the sons of Judah, and of the sons of Benjamin, —and of the sons of Ephraim, and Manasseh:
Wale waliotoka Yuda, Benyamini, Efraimu na Manase ambao waliishi Yerusalemu walikuwa:
4 Uthai son of Ammihud, son of Omri, son of Imri, son of Bani, of the sons of Perez, son of Judah.
Uthai mwana wa Amihudi, mwana wa Omri, mwana wa Imri, mwana wa Bani, wa wana wa Peresi, mwana wa Yuda.
5 And, of the Shilonites, Asaiah the firstborn, and his sons.
Wazao wa Washiloni waliorudi ni: Asaya mzaliwa wa kwanza na wanawe.
6 And, of the sons of Zerah, Jeuel, —and their brethren, six hundred and ninety.
Kwa wana wa Zera: Yeueli. Watu wa Yuda jumla yao walikuwa watu 690.
7 And, of the sons of Benjamin, Sallu, son of Meshullam, son of Hodaviah, son of Hassenuah;
Kwa Benyamini walikuwa: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Hodavia, mwana wa Hasenua;
8 and Ibneiah, son of Jeroham, and Elah, son of Uzzi, son of Michri, —and Meshullam, son of Shephatiah, son of Reuel, son of Ibnijah;
Ibneya mwana wa Yerohamu, Ela mwana wa Uzi, mwana wa Mikri; na Meshulamu mwana wa Shefatia, mwana wa Reueli, mwana wa Ibniya.
9 and their brethren, by their generations, nine hundred and fifty-six, —all these men, were ancestral chiefs, to their ancestral house.
Watu kutoka Benyamini kama walivyoorodheshwa katika koo zao jumla yao ni 956. Watu hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao.
10 And, of the priests, Jedaiah, and Jehoiarib, and Jachin, —
Wa jamaa za makuhani walikuwa: Yedaya, Yehoyaribu na Yakini;
11 and Azariah son of Hilkiah, son of Meshullam, son of Zadok, son of Meraioth, son of Ahitub, chief ruler of the house of God;
Azaria mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu aliyekuwa afisa kiongozi wa nyumba ya Mungu.
12 and Adaiah, son of Jeroham, son of Pashhur, son of Malchijah, —and Maasai son of Adiel, son of Jahzerah, son of Meshullam, son of Meshillemith, son of Immer;
Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya; Maasai, mwana wa Adieli, mwana wa Yahzera, mwana wa Meshulamu, mwana wa Meshilemithi, mwana wa Imeri.
13 and their brethren, chief men of their ancestral house, a thousand and seven hundred and sixty, —able men, for the business of the service of the house of God.
Makuhani waliokuwa viongozi wa jamaa zao walikuwa 1,760. Walikuwa watu wenye uwezo, waliowajibika kuhudumu katika nyumba ya Mungu.
14 And, of the Levites, Shemaiah, son of Hasshub, son of Azrikam, son of Hashabiah, of the sons of Merari;
Jamaa za Walawi walikuwa: Shemaya, mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, wa wana wa Merari.
15 and Bakbakkar, Heresh, and Galal, —and Mattaniah, son of Mica, son of Zichri, son of Asaph;
Bakbakari, Hereshi, Galali na Matania mwana wa Mika, mwana wa Zikri, mwana wa Asafu.
16 and Obadiah, son of Shemaiah, son of Galal, son of Jeduthun, —and Berechiah son of Asa, son of Elkanah, who dwelt in the villages of the Netophathites.
Obadia mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni. Berekia mwana wa Asa, mwana wa Elikana, ambao waliishi katika vijiji vya Wanetofathi.
17 And, the keepers of the gates, were Shallum, and Akkub, and Talmon, and Ahiman, —and their brethren—Shallum the chief;
Mabawabu katika Hekalu la Bwana waliorudi walikuwa: Shalumu, Akubu, Talmoni, Ahimani na ndugu zao. Shalumu alikuwa mlinzi wao mkuu.
18 and, hitherto, they were in the gate of the king, eastward, —the same, were the keepers of the gate, for the camps of the sons of Levi.
Walikuwa wamewekwa katika lango la mfalme lililokuwa upande wa mashariki, mpaka wakati huu. Hawa walikuwa mabawabu wa kutoka kwenye kambi ya Walawi.
19 And, Shallum, son of Kore, son of Ebiasaph, son of Korah and his brethren of his ancestral house—the Korahites, were over the business of the service, watchers at the vestibule of the tent, —and, their fathers, had been over the camp of Yahweh, watchers at the entrance.
Shalumu mwana wa Kore, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora, pamoja na mabawabu wenzake kutoka jamaa yake ya Kora waliwajibika kulinda malango ya Hema, kama vile baba zao walivyokuwa wamewajibika kulinda ingilio la Maskani ya Bwana.
20 And, Phinehas son of Eleazar, was, chief ruler, over them aforetime, Yahweh, being with him.
Hapo zamani Finehasi mwana wa Eleazari alikuwa kiongozi wa mabawabu, naye Bwana alikuwa pamoja naye:
21 Zechariah son of Meshelemiah, was door-keeper at the entrance of the tent of meeting.
Zekaria mwana wa Meshelemia alikuwa bawabu katika ingilio la Hema la Kukutania.
22 All those who were chosen for door-keepers in the vestibule, were two hundred and twelve, —the same, in their villages, had registered themselves, the same, did David and Samuel the seer establish in their trust.
Jumla ya waliochaguliwa kuwa mabawabu katika sakafu za kupuria nafaka walikuwa watu 212. Waliandikishwa kwa koo zao kwenye vijiji vyao. Mabawabu hawa waliwekwa katika nafasi zao za kuaminiwa na Daudi pamoja na mwonaji Samweli.
23 So, they and their sons, were over the gates of the house of Yahweh, of the house of the tent, by watches.
Wao na wazao wao walikuwa viongozi wa kulinda malango ya nyumba ya Bwana, nyumba iliyoitwa Hema.
24 Towards the four winds, were the keepers of the gates, —eastward, westward, northward, and southward.
Mabawabu walikuwa pande zote nne: mashariki, magharibi, kaskazini na kusini.
25 And, their brethren in their villages, had to come in, every seven days, from time to time, along with these.
Ndugu zao katika vijiji vyao walikuwa wakija mara kwa mara na kuwasaidia katika kazi zao kwa vipindi mbalimbali vya siku saba.
26 For, in trust, were four mighty men of the keepers of the gates, the same, were Levites, —and they were over the chambers, and over the treasuries of the house of God.
Lakini mabawabu wanne wakuu, waliokuwa Walawi, walikabidhiwa wajibu kwa ajili ya vyumba na hazina katika nyumba ya Mungu.
27 And, round about the house of God, used they to lodge, —for, upon them, was the charge, and they were over the setting open, morning by morning.
Walikesha mahali walipowekwa kuizunguka nyumba ya Mungu, kwa sababu iliwapasa kuilinda. Pia walitunza funguo kwa ajili ya kufungua mlango kila siku asubuhi.
28 And, some from among them, were over the utensils of the service, —for, by number, used they to bring them in, and, by number, used they to take them forth.
Baadhi yao walikuwa viongozi wa kutunza vifaa vilivyotumika katika huduma ndani ya Hekalu; walivihesabu kila vilipoingizwa ndani na kila vilipotolewa.
29 And, some from among them, were appointed over the utensils, yea over all the vessels of the holy place, —and over the fine meal, and the wine, and the oil, and the frankincense, and the spices.
Wengine walipangiwa kutunza mapambo na vifaa vingine vya patakatifu, pamoja na unga, divai, mafuta, uvumba na vikolezo.
30 And, some from among the sons of the priests, were compounders of perfumes, with the spices.
Lakini baadhi ya makuhani walifanya kazi ya kuchanganya vikolezo.
31 And, Mattithiah, from among the Levites, —the same, was the firstborn of Shallum the Korahite—was in trust over the making of the flat cakes.
Mlawi aliyeitwa Matithia, mwana mzaliwa wa kwanza wa Shalumu, wa ukoo wa Kora, alikabidhiwa wajibu kwa ajili ya kuoka mikate ya sadaka.
32 And, some from among the Kohathites, of their brethren, were over the Bread that was set in Array, —to place it sabbath by sabbath.
Baadhi ya ndugu zao wa ukoo wa Kohathi walikuwa viongozi wa kuandaa mikate ya Wonyesho kwa ajili ya kila Sabato, mikate iliyokuwa inawekwa mezani.
33 These, also were the singers, ancestral chiefs of the Levites, in the chambers, free, —for, by day and by night, was there [a charge] upon them, in the business.
Wale waliokuwa waimbaji, viongozi wa jamaa za Walawi, waliishi katika vyumba vya Hekalu, nao hawakufanya shughuli nyingine yoyote kwa sababu iliwapasa kuwajibika kwa kazi hiyo usiku na mchana.
34 These, were the ancestral chiefs, of the Levites, by their generations, chief men, —these, dwelt in Jerusalem.
Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa za Walawi, wakuu kama walivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.
35 And, in Gibeon, dwelt the father of Gibeon, Jeiel, —the name of whose wife, was Maacah:
Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka,
36 and, his firstborn son, Abdon, —and Zur, and Kish, and Baal and Ner, and Nadab;
mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,
37 and Gedor, and Ahio, and Zechariah, and Mikloh.
Gedori, Ahio, Zekaria na Miklothi.
38 And, Mikloth, begat Shimeam—and, they also, over against their brethren, did dwell in Jerusalem, along with their brethren.
Miklothi akamzaa Shimeamu. Wao pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu.
39 And, Ner, begat Kith, and, Kish, begat Saul, —and, Saul, begat Jonathan, and Malchishua, and Abinadab, and Eshbaal;
Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli. Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.
40 and, the son of Jonathan, was Merib-baal, —and, Merib-baal, begat Micah;
Yonathani akamzaa Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika.
41 and, the sons of Micah, were Pithon, and Melech, and Tahrea [and Ahaz];
Wana wa Mika walikuwa: Pithoni, Meleki, Tarea, na Ahazi.
42 and, Ahaz, begat Jarah, and, Jarah begat Alemeth, and Azmaveth, and Zimri, —and Zimri, begat Moza;
Ahazi akamzaa Yara, Yara akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa.
43 and, Moza, begat Binea, —and Raphaiah his son, Eleasah his son, Azel his son;
Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Refaya, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli.
44 and, Azel, had six sons, and these are their names—Azrikam, [his firstborn], and Ishmael, and Sheariah and Obadiah, and Hanan, [and Asah]. These, were the sons of Azel.
Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Aseli.

< 1 Chronicles 9 >