< 1 Chronicles 21 >

1 Then the accuser stood up, against Israel, —and moved David, to number Israel.
Shetani akainuka dhidi ya Israeli na kumshawishi Daudi ahesabu watu wa Israeli.
2 And David said unto Joab and unto the rulers of the people, Go, number Israel, from Beer-sheba even unto Dan, —and bring [the report] unto me, that I may know the number of them.
Kwa hiyo Daudi akamwambia Yoabu na majemadari wa jeshi, “Nendeni mkawahesabu Waisraeli kuanzia Beer-Sheba mpaka Dani. Kisha nileteeni taarifa ili kwamba niweze kufahamu wako wangapi.”
3 Then said Joab, May Yahweh add unto his people, as many as they are, a hundred times, but are they not, my lord O king, all of them my lord’s, as servants? wherefore should my lord seek this? wherefore should it become guilt to Israel?
Yoabu akajibu, “Bwana na aongeze jeshi lake mara mia na zaidi. Mfalme bwana wangu, kwani hawa wote si raiya wa bwana wangu? Kwa nini bwana wangu unataka kufanya hivi? Kwa nini kuleta hatia juu ya Israeli?”
4 But, the word of the king, prevailed against Joab, —and Joab departed, and went to and fro throughout all Israel, and came to Jerusalem.
Hata hivyo, neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu; kwa hiyo Yoabu akaondoka na kuzunguka Israeli yote kisha akarudi Yerusalemu.
5 And Joab delivered the sum of the number of the people, unto David, —and all Israel was found to be a thousand thousand and a hundred thousand men, who drew sword, and Judah, four hundred and seventy thousand men, who drew sword.
Yoabu akampa Daudi jumla ya idadi ya watu wanaoweza kupigana. Katika Israeli kulikuwa na watu 1,100,000 ambao wangeweza kutumia upanga na katika Yuda watu 470,000.
6 But, Levi and Benjamin, counted he not among them, —for detestable was the word of the king unto Joab.
Lakini Yoabu hakuwahesabu Walawi na Wabenyamini, kwa sababu alichukizwa sana na amri ya mfalme.
7 And it was displeasing in the eyes of God, concerning this thing, —therefore smote he Israel.
Amri hii ilikuwa mbaya machoni pa Mungu pia; hivyo akaiadhibu Israeli.
8 And David said unto God, I have sinned greatly, in that I have done this thing, —but, now, I beseech thee, take away the iniquity of thy servant, for I have shown myself very foolish.
Kisha Daudi akamwambia Mungu, “Nimetenda dhambi kubwa kwa kufanya jambo hili. Sasa, ninakusihi, ondoa hatia ya mtumishi wako. Nimefanya jambo la kipumbavu sana.”
9 Then spake Yahweh unto Gad, the seer of David saying:
Bwana akamwambia Gadi, mwonaji wa Daudi,
10 Go—and thou shalt speak unto David, saying, Thus, saith Yahweh, Three things, do I offer thee, —choose thee one from among them, that I may do it unto thee.
“Nenda ukamwambie Daudi, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Ninakupa wewe uchaguzi wa mambo matatu. Nichagulie mojawapo nitakalotenda dhidi yako.’”
11 So Gad came unto David, —and said to him, Thus, saith Yahweh,
Kwa hiyo Gadi akamwendea Daudi akamwambia, “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Chagua:
12 Choose thee: —Whether, for three years, [there be] famine, Or, for three months, that thou flee before thine adversaries, while the sword of thine enemies overtaketh thee, Or, for three days, the sword of Yahweh, and pestilence be in the land, with, the messenger of Yahweh, laying waste throughout all the boundary of Israel, —Now, therefore, see, what, answer, I shall return unto him that sent me.
miaka mitatu ya njaa, au miezi mitatu ya kushindwa na adui zako, ukipatwa na upanga wao, au siku tatu za upanga wa Bwana, yaani, siku tatu za tauni katika nchi na malaika wa Bwana akiangamiza kila mahali katika Israeli.’ Sasa basi, amua jinsi nitakavyomjibu yeye aliyenituma.”
13 And David said unto Gad, I am in a great strait, —Oh let me fall, I pray thee, into the hand of Yahweh, for abounding are his compassions, exceedingly, but, into the hand of man, let me not fall.
Daudi akamwambia Gadi, “Ninayo mahangaiko makubwa. Mimi na nianguke mikononi mwa Bwana kwa maana rehema zake ni kuu mno, lakini usiniache niangukie mikononi mwa wanadamu.”
14 So Yahweh laid pestilence, upon Israel, —and there fell, of Israel, seventy thousand men.
Basi Bwana akatuma tauni katika Israeli, watu 70,000 wa Israeli wakafa.
15 And God sent a messenger to Jerusalem, to lay it waste, but, as he was laying it waste, Yahweh looked, and relented concerning the calamity, and said unto the messenger who was laying waste, Enough! now, stay thy hand. And, the messenger of Yahweh, was standing by the threshing-floor of Ornan the Jebusite.
Mungu akapeleka malaika kuangamiza Yerusalemu. Lakini malaika alipokuwa akifanya hivyo, Bwana akaona na akahuzunika kwa sababu ya maafa, akamwambia yule malaika aliyekuwa anaangamiza watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Bwana alikuwa amesimama katika sakafu ya kupuria nafaka ya Arauna Myebusi.
16 And, when David lifted up his eyes, and saw the messenger of Yahweh, standing, between the earth and the heavens, and his sword drawn, in his hand, stretched out over Jerusalem, then fell David and the elders, clothed in sackcloth, upon their faces.
Daudi akayainua macho yake akamwona huyo malaika wa Bwana akiwa amesimama katikati ya mbingu na dunia, naye ameunyoosha upanga wake juu ya Yerusalemu tayari kuangamiza. Kisha Daudi na wazee, waliokuwa wamevaa nguo za gunia, wakaanguka kifudifudi.
17 And David said unto God, Was it not, I, who gave word to number the people? Yea, I, it was who sinned and did the great wrong, what then had, these sheep, done? O Yahweh, my God, let thy hand, I beseech thee, be against me, and against the house of my father, but not against, thy people, that they should be plagued!
Daudi akamwambia Mungu, “Je, si mimi ndiye niliyeamuru watu wahesabiwe? Mimi ndiye niliyetenda dhambi na kukosa. Hawa ni kondoo tu. Wamefanya nini? Ee Bwana, Mungu wangu, mkono wako na uwe juu yangu mimi na jamaa yangu, lakini usiache tauni hii iendelee juu ya watu wako.”
18 And, the messenger of Yahweh, commanded Gad, to say unto David, —that David should go up, to rear an altar unto Yahweh, in the threshing-floor of Ornan the Jebusite.
Kisha malaika wa Bwana akamwamuru Gadi amwambie Daudi apande na kumjengea Bwana madhabahu kwenye sakafu ya kupuria nafaka ya Arauna Myebusi.
19 So David went up, according to the word of Gad, which he spake in the name of Yahweh.
Kwa hiyo Daudi akakwea, akalitii lile neno ambalo Gadi alikuwa amelisema katika jina la Bwana.
20 And Ornan turned, and saw the messenger, but, his four sons with him, were hiding themselves, —now, Ornan, had been threshing wheat.
Arauna alipokuwa akipura ngano, akageuka akamwona yule malaika. Wanawe wanne waliokuwa pamoja naye wakajificha, yeye akaendelea kupura ngano.
21 Then came David unto Ornan, —and Ornan looked, and saw David, and went forth out of the threshing-floor, and bowed himself unto David, with his face to the ground.
Kisha Daudi akakaribia, Arauna alipotazama na kumwona, akaondoka kwenye uwanja wa kupuria nafaka akamsujudia Daudi akiuinamisha uso wake ardhini.
22 And David said unto Ornan, Grant me the place of the threshing-floor, that I may build thereon an altar, unto Yahweh, —for silver in full, shalt thou grant it me, that the plague may be stayed from off the people.
Daudi akamwambia, “Nipatie huu uwanja wako wa kupuria nafaka ili niweze kujenga madhabahu ya Bwana tauni ipate kukomeshwa katika watu. Niuzie kwa bei yake kamili.”
23 And Ornan said unto David, Take it to thee, and let my lord the king do what is good in his own eyes, —see! I have given the oxen for ascending-sacrifices, and, the threshing implements for wood, and the wheat for a meal-offering, —the whole, have I given.
Arauna akamwambia Daudi, “Uchukue huo uwanja. Mfalme bwana wangu na afanye lolote analopenda. Tazama, nitatoa maksai kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, vifaa vya kupuria kuwa kuni, pamoja na ngano kwa ajili ya dhabihu ya nafaka. Natoa hivi vyote.”
24 Then said King David to Ornan, Nay! but I will, surely buy, it for silver in full, —for I will not take that which is thine for Yahweh, nor offer an ascending-sacrifice that hath cost me nothing.
Lakini Mfalme Daudi akamjibu Arauna, “La hasha! Lakini ninasisitiza kwamba nitalipa bei yake kamili. Sitachukua kilicho chako kwa ajili ya Bwana au kutoa sadaka ya kuteketezwa ambayo hainigharimu chochote.”
25 So David gave to Ornan, for the place, —shekels of gold, by weight, six hundred.
Basi Daudi akamlipa Arauna shekeli za dhahabu 600 kwa ajili ya ule uwanja.
26 And David built there an altar unto Yahweh, and caused to go up ascending-sacrifices, and peace-offerings, —and called unto Yahweh, and he responded to him, by fire, out of the heavens, upon the altar of ascending-sacrifice.
Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu mahali hapo, na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Akamwita Bwana naye Bwana akajibu maombi yake kwa moto toka mbinguni juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa.
27 And Yahweh gave word to tile messenger, and he put back his sword into its sheath.
Kisha Bwana akanena na yule malaika, naye akarudisha upanga wake katika ala yake.
28 At that time, when David saw that Yahweh had answered him in the threshing-floor of Ornan the Jebusite, then he sacrificed there.
Wakati huo, Daudi alipoona kwamba Bwana amemjibu kule kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Arauna Myebusi, akatoa dhabihu huko.
29 But, the habitation of Yahweh, which Moses made in the desert, and the altar of ascending-sacrifice, were, at that time, in the high place at Gibeon;
Maskani ya Bwana ambayo Mose aliitengeneza kule jangwani, pamoja na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa wakati huo vilikuwa viko mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni.
30 and David could not go before it, to seek God, —for he had been terrified, because of the sword of the messenger of Yahweh.
Lakini Daudi hakuthubutu kuisogelea ili kumuuliza Mungu, kwa sababu aliuogopa upanga wa yule malaika wa Bwana.

< 1 Chronicles 21 >