< 1 Chronicles 18 >

1 And it canto to pass, after this, that David smote the Philistines, and subdued them, —and took Gath and her villages, out of the hand of the Philistines.
Baada ya haya Daudi akawashambulia Wafilisti na kuwashinda. Alichukuwa Gathi na vijiji vyake katika utawala wa Wafilisti.
2 And he smote Moab, —and the Moabites became servants to David, bearers of a present.
Kisha akamshinda Moabu, na Wamoabu wakawa watumishi wa Daudi na wakamlipa ushuru maalumu.
3 And David smote Hadarezer king of Zobah, towards Hamath, —as he went to establish his hold of the river Euphrates.
Daudi kisha akamshinda Hadadezeri, mfalme wa Zoba huko Hamathi, wakati Hadadezeri alipo kuwa akisafiri kuimarisha utawala wake kwa Mto wa Frati.
4 And David captured from him a thousand chariots, and seven thousand horsemen, and twenty thousand footmen, —and David destroyed all the chariots, saving that he reserved from them a hundred chariots.
Daudi akateka magari ya farasi elfu, wanaume wa farasi elfu saba, na wanajeshi wa miguu elfu ishirini. Daudi aliwajeruhi farasi wote wagari, lakini akahifadhi baadhi kwa ajili ya magari ya farasi mia moja.
5 And, when the Syrians of Damascus came to help Hadarezer king of Zobah, David smote of the Syrians, twenty-two thousand men.
Waaramia wa Damasko walipo kuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Zoba, Daudi aliua wanaume elfu ishirini na mbili wa Kiaramia.
6 And David put [garrisons] in Syria of Damascus, and so it was that the Syrians became, David’s, servants, bearers of a present, —so Yahweh gave victory to David, whithersoever he went.
Kisha Daudi akaweka vikosi huko Aramu ya Damasko, na Waaramia wakawa watumishi wake na wakamletea ushuru maalaumu. Yahweh alimpatia Daudi ushindi popote alipoenda.
7 And David took the shields of gold, that were upon the servants of Hadarezer, —and brought them to Jerusalem;
Daudi alichukua ngao za dhahabu zilizo kuwa kwa watumishi wa Hadadezeri na kuleta Yerusalemu.
8 also, from Tibhath and from Cun, cities of Hadarezer, David took very much bronze, —therewith, did Solomon make the sea of bronze, and the pillars, and the vessels of bronze.
Kutoka Tibhathi na Kuni, miji ya Hadadezeri, Daudi alichukuwa shaba nyingi sana. Ilikuwa shaba hii ambayo baadae Sulemani alifanya saani ya shaba, nguzo, na vifaa vya shaba.
9 And, when Tou, king of Hamath, heard that David had smitten all the force of Hadarezer king of Zobah,
Wakati Toi, mfalme wa Hamathi, alipo sikia kuwa Daudi ameshinda majeshi yote ya Hadadezeri mfalme wa Zoba,
10 he sent Hadoram his son unto King David, to ask after his welfare, and to bless him, because he had made war against Hadarezer and had smitten him, for, a man making wars against Tou, had been Hadarezer, —and [he had with him] all manner of vessels of gold and silver and bronze;
Toi akamtuma Hadoramu mwanae kwa Mfalme Daudi kumsalimia na kumbariki, kwasababu Daudi amepigana na Hadadezeri na kumshinda, na kwasababu Hadadezeri alifanya vita na Toi. Hadoramu alipeleka vifaa vya fedha, dhahabu, na shaba.
11 them also, did King David hallow unto Yahweh, with the silver and the gold, that he bare away from all the nations, —from Edom, and from Moab, and from the sons of Ammon, and from the Philistines, and from Amalek.
Mfalme Daudi alivitenga hivi vitu kwa ajili ya Yahweh, pamoja na fedha na dhahabu aliyo ibeba kutoka kwa mataifa yote: Edomu, Moabu, watu wa Amoni, Wafilisti, na Waamaleki.
12 Moreover, Abishai, son of Zeruiah, smote Edom, in the Valley of Salt, —eighteen thousand;
Abishai mwana wa Zeruia akawaua Waedomi elfu kumi na nane katika Bonde la Chumvi.
13 and set, in Edom, garrisons, and all Edom became servants unto David, —and Yahweh gave David the victory, whithersoever he went.
Alieka vikosi huko Edomu, na Waedomi wote wakawa watumishi wa Daudi. Yahweh alimpa Daudi ushindi pote alipoenda.
14 So David reigned over all Israel, —and he was executing justice and righteousness for all his people;
Daudi alitawala Israeli yote, na alitenda haki na utaua kwa watu wote.
15 and, Joab, son of Zeruiah, was over the army, —and, Jehoshaphat, son of Elihud, was recorder;
Yoabu mwana wa Zeruia walikuwa mkuu wa jeshi, na Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mtunza kumbukumbu.
16 and, Zadok, son of Ahitub, and Abimelech son of Abiathar, were priests, —and, Shavsha, was scribe;
Zadoki mwana wa Ahitubi na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani, na Shavisha alikuwa mwandishi.
17 and, Benaiah, son of Jehoiada, was over the Cherethites, and the Pelethites, —and, the sons of David, were first, in attendance on the king.
Benaia mwana wa Yehoiada alikuwa mwangalizi wa Wakerethi na Wapelethi, na wana wa Daudi walikuwa washauri wakuu wa mfalme.

< 1 Chronicles 18 >