< 1 Chronicles 12 >

1 Now these, are they who came unto David, to Ziklag, he yet being shut up, because of Saul son of Kish, —and, they, were among the heroes, helpers in the war;
Hawa walikuwa wanaume walio kuja kwa Daudi huko Zikilagi, wakati akiwa bado amefukuzwa katika uwepo wa Sauli mwana wa Kishi. Walikuwa miongoni mwa wanajeshi, wasaidizi wake katika mapambano.
2 armed with the bow, using right hand or left with stones, and with arrows in the bow, —of the brethren of Saul, out of Benjamin:
Walikuwa wana upinde na waliweza kutumia mkono wa kuume na wakushoto kurusha mawe na manati na kupiga mishale kutoka kwenye upinde. Walikuwa Wabenjamini, ndugu wa kabila moja na Sauli.
3 the chief, Ahiezer, and Joash, sons of Shemaah the Gibeathite, and Jeziel and Pelet, sons of Azmaveth, —and Beracah, and Jehu the Anathothite;
Kiongozi alikuwa Ahi Eza, halafu Yoashi, Wana wote wa Shemaa Mgibeathi. Kulikuwa na Yezieli na Peleti, wana wa Azimavethi. Kulikuwa pia na Beraka, Yehu Waanathothi,
4 and Ishmaiah, the Gibeonite, a hero among the thirty, and over the thirty, —and Jeremiah and Jahaziel, and Johanan, and Jozabad, the Gederathite;
Ishimaia Mgibeoni, mwanajeshi kati ya wale thelathini ( na kiongozi wa wale thelathini); Yeremia, Yahazieli, Yohana, Yozabadi Wagederathi,
5 Eluzai and Jerimoth and Bealiah and Shemariah, and Shephatiah, the Haruphite;
Eluzai, Yerimothi, Bealia, Shemaria, Shefatia Waharufi,
6 Elkanah and Isshiah, and Azarel, and Joezer and Jashobeam, the Korahites;
Wakorahi ni Elkana, Ishia, Azareli, Yoeza, Yashobeamu, na
7 and Joelah and Zebadiah, sons of Jeroham, of Gedor.
Yoela na Zebadia, wana wa Yeroham wa Gedori.
8 And, of the Gadites, there separated themselves unto David, to the stronghold towards the desert, heroes of valour, men of war, for battle, men that could handle shield and spear, —and, faces of lions, were their faces, and, like gazelles upon the mountains, were they, for swiftness:
Baadhi ya Wagadi walijiunga na Daudi katika ngome iliyo nyikani. Walikuwa wanaume wapiganaji, waliofundishwa kwa mapambano, walioweza kumudu ngao na mkuki; ambao nyuso zao zilikuwa kali kama za simba. Walikuwa wepesi kwenye milima kama swala.
9 Ezer, the chief, Obadiah, the second, —Eliab, the third;
Kulikuwa na Eza kiongozi, Obadia wapili, Eliabu watatu,
10 Mashmannah, the fourth, Jeremiah, the fifth;
Mishimana wanne, Yeremia watano,
11 Attai, the sixth, Eliel the seventh;
Atai wasita, Elieli wasaba,
12 Johanan, the eighth, Elzabad, the ninth;
Yohana wanane, Elizabadi watisa,
13 Jeremiah, the tenth, Machbannai, the eleventh.
Yeremia wakumi, Makibanai wakumi na moja.
14 These, were of the sons of Gad, chiefs of the host, —one to a hundred, the least, and, the greatest, to a thousand.
Wana wa Gadi walikuwa viongozi wa jeshi. Wamwisho aliongoza mia moja, na mkubwa aliongoza elfu moja.
15 These, are they who passed over the Jordan, in the first month, when, it, was full, over all its banks, —and they put to flight all them of the vales, to the east and to the west.
Walikatisha Yordani kwa mwezi wa kwanza, wakati vijito vyake vilipofurika, na kuwafukuza wote wanaoishi katika mabonde, pande zote za mashariki na magharibi.
16 And there came, of the sons of Benjamin, and Judah, as far as the stronghold, unto David.
Baadhi ya wanaume wa Benjamini na Yuda walikuja kwenye ngome kwa Daudi.
17 And David went forth to meet them, and responded, and said to them, If, peaceably, ye are come unto me, to help me, I shall have towards you, a heart for unity, —but, if to betray me to mine adversaries, there being no violence in my hands, may the God of our fathers see and rebuke!
Daudi alienda nje kuwasalimu na kuwahutubia: “kama mmekuja kwa amani kunisaidia, mnaweza kujiunga nami. Lakini kama mmekuja kunisaliti kwa maadui zangu, Ee Mungu wa mababu zetu awaone na kuwakemea, tangu sijafanya kosa.”
18 Then, the spirit, clothed Amasai, chief of the thirty, Thine, O David, Yea, with, thee, O son of Jesse! Prosperity, prosperity to thee, And prosperity to thy helpers, For thy God, hath helped thee: So David accepted them, and set them among the chiefs of the band.
Kisha roho ikaja juu ya Amasai, ambaye alikuwa kiongozi wa wale thelathini. Amasai alisema, “Sisi ni wako, Daudi. Sisi tupo upande wako, mwana wa Yesse. na amani iwe juu ya yeyote atakaye kusaidia. Kuwa Mungu wako anakusaidia.” Kisha Daudi akawapokea na kuwafanya wakuu wa watu wake.
19 And, of Manasseh, there fell away unto David, when he came with the Philistines against Saul to battle, but they helped them not, —for the lords of the Philistines advisedly sent him away, saying, At the price of our heads, he might fall away to his master, Saul.
Baadhi kutoka kwa Manase pia wakamwendea Daudi alipokuja na Wafilisti dhidi ya Sauli katika pambano. Lakini hawakuwasaidia Wafilisti kwasababu mabwana wa Wafilisti walishauriana na wakamfukuza Daudi. Walisema, “Atamwendea Bwana wake Sauli na kuhatarisha maisha yetu.”
20 When he went into Ziklag, there fell away unto him, of Manasseh, Adnah and Jozabad, and Jediael and Michael and Jozabad, and Elihu and Zillethai, —chiefs of the thousands that pertained to Manasseh;
Alipokwenda kwa Zikilagi, wanaume wa Manase walioungana nae walikuwa Adina, Yozabadi, Yediaeli, Yozabadi, Elihu, na Zilethai, viongozi wa maelfu wa Manase.
21 and, they, helped with David, against the [marauding] band, for, heroes of valour, were they all, —and they became captains in the host;
Walimsaidia Daudi kupigana na kikundi cha wezi, maana walikuwa wanaume wa mapambano. Baadae walikuwa wakuu katika jeshi.
22 for, from day to day, there came unto David, to help him, —until it was a great camp, like a camp of God.
Siku hadi siku, wanaume walikuja kwa Daudi kumsaidia, mpaka wakawa jeshi kubwa, kama jeshi la Mungu.
23 And, these, are the numbers of the chiefs armed for war, they came unto David, to Hebron, —to turn round the kingdom of Saul unto him, according to the bidding of Yahweh:
Hii ni kumbukumbu ya wanajeshi wa vita, walio kuja kwa Daudi Hebroni, kuupindua ufalme wa Sauli kwake, ilikutimiza neno la Yahweh.
24 Sons of Judah, bearers of shield and spear, six thousand and eight hundred, armed for war.
Kutoka Yuda walio beba ngao na mkuki ni 6, 800, tayari kwa vita.
25 Of sons of Simeon, heroes of valour for the war, seven thousand, and one hundred.
Kutoka kwa Wasimeoni walikuwa 7, 100 wanaume wa mapambano.
26 Of the sons of Levi, four thousand, and six hundred.
Kutoka kwa Walawi kulikuwa na wanaume wa mapambano 4, 600.
27 And Jehoiada, was chief ruler for Aaron, —and, with him, three thousand and seven hundred;
Yehoiada alikuwa kiongozi wa uzao wa Aruni, na kwa yeye walikuwa 3, 700.
28 and Zadok, a young man, a hero of valour, —and the house of his father, captains twenty and two.
Kwa Zadoki, kijana, mwenye nguvu, na mjasiri, walikuwa viongozi ishirini na mbili kwa familia ya baba yake.
29 And, of the sons of Benjamin, brethren of Saul, three thousand, —and, hitherto, the greater part of them, had been keeping the charge of the house of Saul.
Kutoka kwa Benjamini, kabila la Sauli, walikuwa elfu tatu. Wengi wao walibaki waaminifu kwa Sauli mpaka muda huu.
30 And, of the sons of Ephraim, twenty thousand, and eight hundred, —heroes of valour, men of renown, to their ancestral house.
Kutoka kwa Waefraimu palikuwa na wanume wa mapambano 20, 800, wanaume maharufu kwenye familia za baba zao.
31 And, of the half tribe of Manasseh, eighteen thousand, who were distinguished by name, coming in to make David king.
Kutoka kabila nusu la Manase palikuwa na wanaume elfu kumi na nane maharufu walio kuja kufanya Daudi mfalme.
32 And, of the sons of Issachar, such as were of good understanding of the times, to know what Israel, should do, their chiefs, were two hundred, and, all their brethren, were at their bidding.
Kutoka kwa Isakari, palikuwa na viongozi mia mbili walio kuwa na ufahamu wa nyakati na walijua nini Israeli ya paswa kufanya. Ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.
33 Of Zebulun—such as were ready to go forth in host, expert for battle with all weapons of war, fifty thousand, —and for setting in array, not of two minds!
Kutoka Zebuloni palikuwa na wanaume elfu hamsini wa mapambano, tayari kwa vita, na silaha zote za vita, na tayari kutoa uwaminifu usio pungua.
34 And, of Naphtali, a thousand captains, —and, with them, with shield and spear, thirty-seven thousand.
Kutoka kwa Naftali palikuwa na askari elfu moja, na pamoja nao wanaume elfu thelathini na saba wenye ngao na mikuki.
35 And, of the Danite, expert for war, twenty-eight thousand, and six hundred.
Kutoka kwa Wadani palikuwa na wanaume 28, 600 wameandaliwa kwa ajili ya pambano.
36 And, of Asher, such as were ready to go forth in host to set in array for battle, forty thousand.
Kutoka kwa Asheri palikuwa na wanaume elfu arobaini wameandaliwa kwa pambano.
37 And, from over the Jordan, of the Reubenites and Gadites and half tribe of Manasseh, with all manner of weapons of war for battle, a hundred and twenty thousand.
Kutoka upande wa pili wa Yordani, kutoka kwa Warubeni, Wagadi, na nusu kabila la Manase, palikuwa na wanaume 120, 000 wameandaliwa na silaha za kila namna kwa ajili ya pambano.
38 All these, being men of war, expert in setting in battle-array, with a perfect heart, came to Hebron, to make David king over all Israel, —moreover also, all the rest of Israel, were of one heart to make David king.
Wanajeshi hawa wote, waliandaliwa kwa pambano, kuja Hebroni kwa dhumuni maalumu la kumfanya Daudi mfalme wa Israeli yote. Israeli yote ilikubaliana na kumfanya Daudi mfalme.
39 So they were there, with David, three days, eating and drinking, —for their brethren had made preparation for them.
Walikuwa na Daudi siku tatu, kula na kunywa, kwa kuwa ndugu zao waliwapa mahitaji ya kwenda nayo.
40 Moreover also, they who were near of kin unto them, as far as Issachar and Zebulun and Naphtali, were bringing bread, on asses and on camels and on mules and on oxen, meal-food, cakes of figs and cakes of raisins, and wine, and oil, and oxen, and sheep—in abundance, —for there was joy Israel.
Kwa kuongezea, wao walio kuwa karibu nao, kwa umbali wa Isakari na Zebuloni na Naftali, walileta mkate kwa punda, ngamia, ng'ombe, na keki, mvinyo, mafuta, ng'ombe, na kondoo, kwa kuwa Israeli walikuwa wana sherehekea

< 1 Chronicles 12 >