< Titus 2 >
1 But speak thou the things which befit the sound doctrine:
Lakini wewe unapaswa kuhubiri mafundisho safi.
2 that aged men be temperate, grave, soberminded, sound in faith, in love, in patience:
Waambie wazee kwamba wanapaswa kuwa na kiasi, wawe na busara na wataratibu; wanapaswa kuwa timamu katika imani yao, upendo na uvumilivu.
3 that aged women likewise be reverent in demeanour, not slanderers nor enslaved to much wine, teachers of that which is good;
Hali kadhalika waambie wanawake wazee wawe na mwenendo wa uchaji wa Mungu; wasiwe wachongezi, au watumwa wa pombe. Wanapaswa kufundisha mambo mema,
4 that they may train the young women to love their husbands, to love their children,
ili wawazoeze kina mama vijana kuwapenda waume zao na watoto,
5 [to be] soberminded, chaste, workers at home, kind, being in subjection to their own husbands, that the word of God be not blasphemed:
wawe na kiasi na safi, waangalie vizuri mambo ya nyumbani, na wawatii waume zao, ili ujumbe wa Mungu usije ukadharauliwa.
6 the younger men likewise exhort to be soberminded:
Kadhalika, wahimize vijana wawe na kiasi.
7 in all things shewing thyself an ensample of good works; in thy doctrine [shewing] uncorruptness, gravity,
Katika mambo yote wewe mwenyewe unapaswa kuwa mfano wa matendo mema. Uwe mnyofu na uwe na uzito katika mafundisho yako.
8 sound speech, that cannot be condemned; that he that is of the contrary part may be ashamed, having no evil thing to say of us.
Maneno yako yasiwe na hitilafu yoyote ili adui zako waaibike wasipopata chochote kibaya cha kusema juu yetu.
9 [Exhort] servants to be in subjection to their own masters, [and] to be well-pleasing [to them] in all things; not gainsaying;
Watumwa wanapaswa kuwatii wakuu wao na kuwapendeza katika mambo yote. Wasibishane nao,
10 not purloining, but shewing all good fidelity; that they may adorn the doctrine of God our Saviour in all things.
au kuiba vitu vyao. Badala yake wanapaswa kuonyesha kwamba wao ni wema na waaminifu daima, ili, kwa matendo yao yote, wayapatie sifa njema mafundisho juu ya Mungu, Mwokozi wetu.
11 For the grace of God hath appeared, bringing salvation to all men,
Maana neema ya Mungu imedhihirishwa kwa ajili ya wokovu wa watu wote.
12 instructing us, to the intent that, denying ungodliness and worldly lusts, we should live soberly and righteously and godly in this present world; (aiōn )
Neema hiyo yatufunza kuachana na uovu wote na tamaa za kidunia; tuwe na kiasi, tuishi maisha adili na ya kumcha Mungu katika ulimwengu huu wa sasa, (aiōn )
13 looking for the blessed hope and appearing of the glory of our great God and Saviour Jesus Christ;
tukiwa tunangojea siku ile ya heri tunayoitumainia, wakati utakapotokea utukufu wa Mungu Mkuu na Mwokozi wetu Yesu Kristo.
14 who gave himself for us, that he might redeem us from all iniquity, and purify unto himself a people for his own possession, zealous of good works.
Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu ili atukomboe kutoka katika uovu wote na kutufanya watu safi walio wake yeye mwenyewe, watu walio na hamu ya kutenda mema.
15 These things speak and exhort and reprove with all authority. Let no man despise thee.
Basi, fundisha mambo hayo na tumia mamlaka yako yote ukiwahimiza na kuwaonya wasikilizaji wako. Mtu yeyote na asikudharau.