< Psalms 88 >
1 A Song, a Psalm of the sons of Korah; for the Chief Musician; set to Mahalath Leannoth. Maschil of Heman the Ezrahite. O LORD, the God of my salvation, I have cried day and night before thee:
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
2 Let my prayer enter into thy presence; incline thine ear unto my cry:
Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
3 For my soul is full of troubles, and my life draweth nigh unto Sheol. (Sheol )
Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol )
4 I am counted with them that go down into the pit; I am as a man that hath no help:
Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
5 Cast off among the dead, like the slain that lie in the grave, whom thou rememberest no more; and they are cut off from thy hand.
Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
6 Thou hast laid me in the lowest pit, in dark places, in the deeps.
Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
7 Thy wrath lieth hard upon me, and thou hast afflicted me with all thy waves. (Selah)
Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
8 Thou hast put mine acquaintance far from me; thou hast made me an abomination unto them: I am shut up, and I cannot come forth.
Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
9 Mine eye wasteth away by reason of affliction: I have called daily upon thee, O LORD, I have spread forth my hands unto thee.
nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
10 Wilt thou shew wonders to the dead? shall they that are deceased arise and praise thee? (Selah)
Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
11 Shall thy lovingkindness be declared in the grave? or thy faithfulness in Destruction?
Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
12 Shall thy wonders be known in the dark? and thy righteousness in the land of forgetfulness?
Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
13 But unto thee, O LORD, have I cried, and in the morning shall my prayer come before thee.
Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
14 LORD, why castest thou off my soul? why hidest thou thy face from me?
Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
15 I am afflicted and ready to die from my youth up: while I suffer thy terrors I am distracted.
Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
16 Thy fierce wrath is gone over me; thy terrors have cut me off.
Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
17 They came round about me like water all the day long; they compassed me about together.
Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
18 Lover and friend hast thou put far from me, and mine acquaintance into darkness.
Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.