< Psalms 77 >
1 For the Chief Musician; after the manner of Jeduthun. A Psalm of Asaph. I will cry unto God with my voice; even unto God with my voice, and he wilt give ear unto me.
Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
2 In the day of my trouble I sought the Lord: my hand was stretched out in the night, and slacked not; my soul refused to be comforted.
Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
3 I remember God, and am disquieted: I complain, and my spirit is overwhelmed. (Selah)
Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
4 Thou holdest mine eyes watching: I am so troubled that I cannot speak.
Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
5 I have considered the days of old, the years of ancient times.
Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
6 I call to remembrance my song in the night: I commune with mine own heart; and my spirit made diligent search.
Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
7 Will the Lord cast off for ever? and will he be favourable no more?
Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
8 Is his mercy clean gone for ever? doth his promise fail for evermore?
Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
9 Hath God forgotten to be gracious? hath he in anger shut up his tender mercies? (Selah)
Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
10 And I said, This is my infirmity; [but I will remember] the years of the right hand of the Most High.
Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
11 I will make mention of the deeds of the LORD; for I will remember thy wonders of old.
Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
12 I will meditate also upon all thy work, and muse on thy doings.
Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
13 Thy way, O God, is in the sanctuary: who is a great god like unto God?
Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
14 Thou art the God that doest wonders: thou hast made known thy strength among the peoples.
Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
15 Thou hast with thine arm redeemed thy people, the sons of Jacob and Joseph. (Selah)
Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
16 The waters saw thee, O God; the waters saw thee, they were afraid: the depths also trembled.
Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
17 The clouds poured out water; the skies sent out a sound: thine arrows also went abroad.
Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
18 The voice of thy thunder was in the whirlwind; the lightnings lightened the world: the earth trembled and shook.
Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
19 Thy way was in the sea, and thy paths in the great waters, and thy footsteps were not known.
Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
20 Thou leddest thy people like a flock, by the hand of Moses and Aaron.
Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.