< Psalms 73 >
1 A Psalm of Asaph. Surely God is good to Israel, [even] to such as are pure in heart.
Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
2 But as for me, my feet were almost gone; my steps had well nigh slipped.
Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
3 For I was envious at the arrogant, when I saw the prosperity of the wicked.
kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
4 For there are no bands in their death: but their strength is firm.
Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
5 They are not in trouble as [other] men; neither are they plagued like [other] men.
Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
6 Therefore pride is as a chain about their neck; violence covereth them as a garment.
Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
7 Their eyes stand out with fatness: they have more than heart could wish.
Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
8 They scoff, and in wickedness utter oppression: they speak loftily.
Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
9 They have set their mouth in the heavens, and their tongue walketh through the earth.
Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
10 Therefore his people return hither: and waters of a full [cup] are wrung out by them.
Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
11 And they say, How doth God know? and is there knowledge in the Most High?
Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
12 Behold, these are the wicked; and, being alway at ease, they increase in riches.
Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
13 Surely in vain have I cleansed my heart, and washed my hands in innocency;
Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
14 For all the day long have I been plagued, and chastened every morning.
Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
15 If I had said, I will speak thus; behold, I had dealt treacherously with the generation of thy children.
Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
16 When I thought how I might know this, it was too painful for me;
Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
17 Until I went into the sanctuary of God, and considered their latter end.
Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
18 Surely thou settest them in slippery places: thou castest them down to destruction.
Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
19 How are they become a desolation in a moment! they are utterly consumed with terrors.
Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
20 As a dream when one awaketh; so, O Lord, when thou awakest, thou shalt despise their image.
Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
21 For my heart was grieved, and I was pricked in my reins:
Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
22 So brutish was I, and ignorant; I was [as] a beast before thee.
Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
23 Nevertheless I am continually with thee: thou hast holden my right hand.
Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
24 Thou shalt guide me with thy counsel, and afterward receive me to glory.
Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
25 Whom have I in heaven [but thee]? and there is none upon earth that I desire beside thee.
Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
26 My flesh and my heart faileth: [but] God is the strength of my heart and my portion for ever.
Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
27 For, lo, they that are far from thee shall perish: thou hast destroyed all them that go a whoring from thee.
Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 But it is good for me to draw near unto God: I have made the Lord GOD my refuge, that I may tell of all thy works.
Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.