< Psalms 63 >

1 A Psalm of David, when he was in the wilderness of Judah. O God, thou art my God; early will I seek thee: my soul thirsteth for thee, my flesh longeth for thee, in a dry and weary land, where no water is.
Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
2 So have I looked upon thee in the sanctuary, to see thy power and thy glory.
Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
3 For thy lovingkindness is better than life; my lips shall praise thee.
Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
4 So will I bless thee while I live: I will lift up my hands in thy name.
Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
5 My soul shall be satisfied as with marrow and fatness; and my mouth shall praise thee with joyful lips;
Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
6 When I remember thee upon my bed, [and] meditate on thee in the night watches.
nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
7 For thou hast been my help, and in the shadow of thy wings will I rejoice.
Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
8 My soul followeth hard after thee: thy right hand upholdeth me.
Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
9 But those that seek my soul, to destroy it, shall go into the lower parts of the earth.
Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
10 They shall be given over to the power of the sword: they shall be a portion for foxes.
watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 But the king shall rejoice in God: every one that sweareth by him shall glory; for the mouth of them that speak lies shall be stopped.
Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.

< Psalms 63 >