< Psalms 56 >
1 For the Chief Musician; set to Jonath elem rehokim. [A Psalm] of David: Michtam: when the Philistines took him in Gath. Be merciful unto me, O God; for man would swallow me up: all the day long he fighting oppresseth me.
Uwe na huruma nami, Mungu, kwa maana watu wananishambulia! Muda wote wale wanao pigana nami hunikaribia zaidi ili wanishambulie.
2 Mine enemies would swallow me up all the day long: for they be many that fight proudly against me.
Adui zangu hunikanyaga muda wote; maana ni wengi ambao kwa kiburi hupigana dhidi yangu.
3 What time I am afraid, I will put my trust in thee.
Wakati nina woga, nitaweka imani yangu katika wewe.
4 In God I will praise his word: in God have I put my trust, I will not be afraid; what can flesh do unto me?
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu - nimeweka imani yangu katika Mungu; sitaogopa; mtu wa kawaida atanifanya nini?
5 All the day long they wrest my words: all their thoughts are against me for evil.
Muda wote wanayageuza maneno yangu; mawazo yao yote yako kinyume na mimi kwa ajili ya uovu.
6 They gather themselves together, they hide themselves, they mark my steps, even as they have waited for my soul.
Wanajikusanya kwa pamoja, wanajificha wenyewe, na kuzifuatilia hatua zangu, wakisubiri kuniua.
7 Shall they escape by iniquity? in anger cast down the peoples, O God.
Usiwaache waikimbie adhabu yako kwa ajili ya uovu wao. Uwaangushe watu chini katika hasira yako, Mungu.
8 Thou tellest my wanderings: put thou my tears into thy bottle; are they not in thy book?
Wewe unahesabu kutangatanga kwangu na kuweka machozi yangu kwenye chupa yako; je, hayako kitabuni mwako?
9 Then shall mine enemies turn back in the day that I call: this I know, that God is for me.
Ndipo maadui zangu watakimbia katika siku ile nikuitapo wewe; hili najua, kwamba Mungu yupo kwa ajili yangu.
10 In God will I praise [his] word: in the LORD will I praise [his] word.
Katika Mungu ambaye neno lake ninalisifu, katika Yahwe ambaye neno lake ninalisifu,
11 In God have I put my trust, I will not be afraid; what can man do unto me?
katika Mungu ninaamini, sitaogopa. Yeyote atanifanya nini?
12 Thy vows are upon me, O God: I will render thank offerings unto thee.
Wajibu wa kutimiza viapo vyangu kwako uko juu yangu, Mungu; nitatoa sadaka ya shukurani.
13 For thou hast delivered my soul from death: [hast thou] not [delivered] my feet from falling? that I may walk before God in the light of the living.
Kwa kuwa umeokoa uhai wangu na mauti; umezuia miguu yangu isianguke, ili kwamba niweze kutembea mbele ya Mungu katika nuru ya uhai.