< Psalms 128 >
1 A Song of Ascents. Blessed is every one that feareth the LORD, that walketh in his ways.
Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
2 For thou shalt eat the labour of thine hands: happy shalt thou be, and it shall be well with thee.
Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
3 Thy wife shall be as a fruitful vine, in the innermost parts of thine house: thy children like olive plants, round about thy table.
Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.
4 Behold, that thus shall the man be blessed that feareth the LORD.
Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
5 The LORD shall bless thee out of Zion: and thou shalt see the good of Jerusalem all the days of thy life.
Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
6 Yea, thou shalt see thy children’s children. Peace be upon Israel.
nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.