< Psalms 111 >
1 Praise ye the LORD. I will give thanks unto the LORD with my whole heart, in the council of the upright, and in the congregation.
Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
2 The works of the LORD are great, sought out of all them that have pleasure therein.
Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
3 His work is honour and majesty: and his righteousness endureth for ever.
Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
4 He hath made his wonderful works to be remembered: the LORD is gracious and full of compassion.
Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
5 He hath given meat unto them that fear him: he will ever be mindful of his covenant.
Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
6 He hath shewed his people the power of his works, in giving them the heritage of the nations.
Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
7 The works of his hands are truth and judgment; all his precepts are sure.
Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
8 They are established for ever and ever, they are done in truth and uprightness.
Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
9 He hath sent redemption unto his people; he hath commanded his covenant for ever: holy and reverend is his name.
Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
10 The fear of the LORD is the beginning of wisdom; a good understanding have all they that do thereafter: his praise endureth for ever.
Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.