< Psalms 101 >
1 A Psalm of David. I will sing of mercy and judgment: unto thee, O LORD, will I sing praises.
Nitaimba uaminifu wa agano lako na hukumu; kwako, Ee Yahwe, Nitakuimbia sifa.
2 I will behave myself wisely in a perfect way: Oh when wilt thou come unto me? I will walk within my house with a perfect heart.
Nitatembea katika njia ya uadilifu. Oh, ni lini utakuja kwangu? Nitatembea kwa uadilifu ndani ya nyumba yangu.
3 I will set no base thing before mine eyes: I hate the work of them that turn aside; it shall not cleave unto me.
Sitaweka matendo maovu mbele ya macho yangu; ninachukia uovu usio na maana; hauta shikamana nami.
4 A froward heart shall depart from me: I will know no evil thing.
Watu waliopotoka wataniacha mimi; mimi sichangamani na uovu.
5 Whoso privily slandereth his neighbour, him will I destroy: him that hath an high look and a proud heart will I not suffer.
Nitamwangamiza yeyote amsengenyaye jirani yake kwa siri. Sitamvumilia yeyote mwenye kiburi.
6 Mine eyes shall be upon the faithful of the land, that they may dwell with me: he that walketh in a perfect way, he shall minister unto me.
Nitawachagua walio waaminifu katika nchi wakae upande wangu. Wale watembeao katika njia ya uhadilifu watanitumikia.
7 He that worketh deceit shall not dwell within my house: he that speaketh falsehood shall not be established before mine eyes.
Watu wadanganyifu hawatabaki ndani ya nyumba yangu; waongo hawatakaribishwa mbele ya macho yangu.
8 Morning by morning will I destroy all the wicked of the land; to cut off all the workers of iniquity from the city of the LORD.
Asubuhi hata asubuhi nitawaangamiza waovu wote kutoka nchini; nitawaondoa watendao maovu wote katika mji wa Yahwe.