< Proverbs 29 >

1 He that being often reproved hardeneth his neck shall suddenly be broken, and that without remedy.
Mtu aliyepokea makaripio mengi lakini anashupaza shingo yake atavunjika ndani ya muda mfupi na hata pona.
2 When the righteous are increased, the people rejoice: but when a wicked man beareth rule, the people sigh.
Watenda mema wanapoongezeka, watu wanafurahi, bali wakati mtu mwovu anapotawala, watu huugua.
3 Whoso loveth wisdom rejoiceth his father: but he that keepeth company with harlots wasteth [his] substance.
Mwenye kupenda hekima baba yake anafurahi, bali anayeshikamana na makahaba huuharibu utajiri wake.
4 The king by judgment establisheth the land: but he that exacteth gifts overthroweth it.
Mfalme huimarisha nchi kwa haki, bali mwenye kudai rushwa huirarua.
5 A man that flattereth his neighbour spreadeth a net for his steps.
Mtu anayejipendekeza kwa jirani yake anatandaza wavu kwenye miguu yake.
6 In the transgression of an evil man there is a snare: but the righteous doth sing and rejoice.
Mtu mbaya hunaswa kwenye mtego wa dhambi yake mwenyewe, bali yeye atendaye haki huimba na kufurahi.
7 The righteous taketh knowledge of the cause of the poor: the wicked hath not understanding to know [it].
Atendaye haki hutetea madai ya masikini; mtu mwovu hafahamu maarifa kama hayo.
8 Scornful men set a city in a flame: but wise men turn away wrath.
Mwenye dhihaka huutia moto mji, bali wale wenye busara huigeuza ghadhabu.
9 If a wise man hath a controversy with a foolish man, whether he be angry or laugh, there will be no rest.
Mtu mwenye busara anapojadiliana na mpumbavu, hughadhabika na kucheka, hakutakuwa na utulivu.
10 The bloodthirsty hate him that is perfect: and as for the upright, they seek his life.
Mkatili humchukia mwenye ukamilifu na hutafuta maisha ya mwenye haki.
11 A fool uttereth all his anger: but a wise man keepeth it back and stilleth it.
Mpumabavu huonyesha hasira yake, bali mtu mwenye busara huishikilia na kujituliza mwenyewe.
12 If a ruler hearkeneth to falsehood, all his servants are wicked.
Kama matawala atazinagatia uongo, maafisa wake wote watakuwa waovu.
13 The poor man and the oppressor meet together: the LORD lighteneth the eyes of them both.
Mtu masikini na mkandamizaji wanafanana, maana Yehova huyapa nuru macho yao wote.
14 The king that faithfully judgeth the poor, his throne shall be established for ever.
Kama mfalme atamhukumu masikini kwa uaminifu, kiti chake cha enzi kitaimarishwa milele.
15 The rod and reproof give wisdom: but a child left to himself causeth shame to his mother.
Fimbo na maonyo huleta hekima, bali mtoto huru mbali na makaripio humwaibisha mama yake.
16 When the wicked are increased, transgression increaseth: but the righteous shall look upon their fall.
Watu waovu wanapotawala, uovu huongezeka, bali wenye kutenda haki wataona anguko la watu waovu.
17 Correct thy son, and he shall give thee rest; yea, he shall give delight unto thy soul.
Mwadibishe mwanao naye atakupa pumziko; ataleta furaha katika maisha yako.
18 Where there is no vision, the people cast off restraint: but he that keepeth the law, happy is he.
Pasipo na maono ya kinabii watu huenda bila utaratibu, bali mwenye kuitunza sheria amebarikiwa.
19 A servant will not be corrected by words: for though he understand he will not give heed.
Mtumwa hawezi kurekebishwa kwa maneno, maana ingawa anaelewa, hakuna mwitikio.
20 Seest thou a man that is hasty in his words? there is more hope of a fool than of him.
Je unamwona mtu mwenye haraka katika maneno yake? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
21 He that delicately bringeth up his servant from a child shall have him become a son at the last.
Mwenye kumdekeza mtumwa wake tangu ujana, mwisho wake itakuwa taabu.
22 An angry man stirreth up strife, and a wrathful man aboundeth in transgression.
Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi na bwana mwenye hasira sana hutenda dhambi nyingi.
23 A man’s pride shall bring him low: but he that is of a lowly spirit shall obtain honour.
Kiburi cha mtu humshusha chini, bali mwenye roho ya unyenyekevu atapewa heshima.
24 Whoso is partner with a thief hateth his own soul: he heareth the adjuration and uttereth nothing.
Anayeshirikiana na mwizi huyachukia maisha yake mwenyewe; husikia laana na wala hasemi chochote.
25 The fear of man bringeth a snare: but whoso putteth his trust in the LORD shall be safe.
Kumwogopa binadamu ni mtego, bali mwenye kumtumaini Yehova atalindwa.
26 Many seek the ruler’s favour: but a man’s judgment [cometh] from the LORD.
Wengi huutafuta uso wa mtawala, bali kutoka kwa Yehova huja haki kwa ajili yake.
27 An unjust man is an abomination to the righteous: and he that is upright in the way is an abomination to the wicked.
Mtu dhalimu ni chukizo kwa wenye kutenda haki, bali mwenye njia ya haki ni chukizo kwa watu waovu.

< Proverbs 29 >