< Proverbs 28 >

1 The wicked flee when no man pursueth: but the righteous are bold as a lion.
Waovu hukimbia wakati hakuna mtu anayewafukuza, bali wale watendao haki ni thabiti kama simba kijana.
2 For the transgression of a land many are the princes thereof: but by men of understanding [and] knowledge the state [thereof] shall be prolonged.
Kwa sababu ya uhalifu wa nchi, kuna wakuu wengi, bali kwa mtu mwenye ufahamu na maarifa, itadumu kwa muda mrefu.
3 A needy man that oppresseth the poor is [like] a sweeping rain which leaveth no food.
Mtu masikini mwenye kukandamiza watu wengine masikini ni kama mvua inayopiga ambayo haisazi chakula.
4 They that forsake the law praise the wicked: but such as keep the law contend with them.
Wale wanaokataa sheria huwatukuza watu waovu, bali wale wenye kuitunza sheria hupigana dhidi yao.
5 Evil men understand not judgment: but they that seek the LORD understand all things.
Watu wabaya hawafahamu haki, bali wale wanaomtafuta Yehova wanafahamu kila kitu.
6 Better is the poor that walketh in his integrity, than he that is perverse in [his] ways, though he be rich.
Ni bora mtu masikini ambaye anatembea katika uadilifu, kuliko mtu tajiri ambaye ni mdanganyifu katika njia zake.
7 Whoso keepeth the law is a wise son: but he that is a companion of gluttonous men shameth his father.
Yeye anayetunza sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali mwenye ushirika na walafi humwaibisha baba yake.
8 He that augmenteth his substance by usury and increase, gathereth it for him that hath pity on the poor.
Anayepata mafanikio kwa kutoza riba kubwa anakusanya utajiri wake kwa ajili ya mwingine ambaye atakuwa na huruma kwa watu masikini.
9 He that turneth away his ear from hearing the law, even his prayer is an abomination.
Kama mtu atageuzia mbali sikio lake kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
10 Whoso causeth the upright to go astray in an evil way, he shall fall himself into his own pit: but the perfect shall inherit good.
Yeye anayempotosha mwenye uadilifu katika njia ya uovu ataangukia kwenye shimo lake mwenyewe, bali wakamilifu watapata urithi mwema.
11 The rich man is wise in his own conceit; but the poor that hath understanding searcheth him out.
Mtu tajiri anaweza kuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu masikini mwenye ufahamu atamtafuta.
12 When the righteous triumph, there is great glory: but when the wicked rise, men hide themselves.
Kunapokuwa na ushindi kwa wenye kutenda haki, kunafuraha kuu, bali wanapoinuka waovu, watu hujificha wenyewe.
13 He that covereth his transgressions shall not prosper: but whoso confesseth and forsaketh them shall obtain mercy.
Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali mwenye kutubu na kuziacha ataonyeshwa rehema.
14 Happy is the man that feareth alway: but he that hardeneth his heart shall fall into mischief.
Anafuraha ambaye huishi kwa unyenyekevu, bali anayeufanya moyo wake ataanguka katika taabu.
15 [As] a roaring lion, and a ranging bear; [so is] a wicked ruler over a poor people.
Kama simba anayeunguruma au dubu anayeshabulia ni kama mtawala mwovu juu ya watu masikini.
16 The prince that lacketh understanding is also a great oppressor: [but] he that hateth covetousness shall prolong his days.
Mtawala anayekosa ufahamu ni mkandamizaji katili, bali mwenye kuchukia aibu atadumu katika siku zake.
17 A man that is laden with the blood of any person shall flee unto the pit; let no man stay him.
Kama mtu anahatia kwa sababu amemwaga damu ya mtu, atakuwa mkimbizi hadi kifo na hakuna atakayemsaidia.
18 Whoso walketh uprightly shall be delivered: but he that is perverse in [his] ways shall fall at once.
Mwenye kuenenda kwa ukaminifu atakuwa salama, bali mwenye njia ya udanganyifu ataanguka ghafla.
19 He that tilleth his land shall have plenty of bread: but he that followeth after vain [persons] shall have poverty enough.
Anayefanya kazi kwenye shamba lake atapata chakula kingi, bali afuataye shughuli za upuuzi atapata umasikini mkubwa.
20 A faithful man shall abound with blessings: but he that maketh haste to be rich shall not be unpunished.
Mtu mwaminifu atapata baraka nyingi bali apataye utajiri wa haraka hawezi kukosa adhabu.
21 To have respect of persons is not good: neither that a man should transgress for a piece of bread.
Siyo vema kuonyesha upendeleo, lakini kwa kipande cha mkate mtu atafanya ubaya.
22 He that hath an evil eye hasteth after riches, and knoweth not that want shall come upon him.
Mtu mchoyo huharakisha kwenye utajiri, lakini hajui ni umasikini gani utakuja juu yake.
23 He that rebuketh a man shall afterward find more favour than he that flattereth with the tongue.
Anayemkaripia mtu baadaye atapata fadhila zaidi kutoka kwake kuliko mwenye kumsifia sana kwa ulimi wake.
24 Whoso robbeth his father or his mother, and saith, It is no transgression; the same is the companion of a destroyer.
Yule anayemwibia baba yake na mama yake na kusema, “Hiyo siyo dhambi,” ni mshirika wa mwenye kuharibu.
25 He that is of a greedy spirit stirreth up strife: but he that putteth his trust in the LORD shall be made fat.
Mtu mwenye tamaa huchochea mafarakano, bali anayemtumaini Yehova atafanikiwa.
26 He that trusteth in his own heart is a fool: but whoso walketh wisely, he shall be delivered.
Yule anayeutumaini moyo wake mwenyewe ni mpumbavu, bali anayekwenda kwa hekima atajilinda mbali na hatari.
27 He that giveth unto the poor shall not lack: but he that hideth his eyes shall have many a curse.
Mwenye kuwapa masikini hatapungukiwa kitu, bali anayewafumbia macho atapokea laana nyingi.
28 When the wicked rise, men hide themselves: but when they perish, the righteous increase.
Watu waovu wanapoinuka, watu hujificha wenyewe, lakini watu waovu wataangamia, wale watendao haki wataongezeka.

< Proverbs 28 >