< Proverbs 21 >

1 The king’s heart is in the hand of the LORD as the watercourses: he turneth it whithersoever he will.
Moyo wa mfalme ni mfereji wa maji katika mkono wa Yehova; anaugeuza popote anakopenda.
2 Every way of a man is right in his own eyes: but the LORD weigheth the hearts.
Kila njia ya mtu ni sawa katika macho yake mwenyewe, lakini ni Yehova anayeipima mioyo.
3 To do justice and judgment is more acceptable to the LORD than sacrifice.
Kutenda haki na adili hukubaliwa zaidi na Yehova kuliko sadaka.
4 An high look, and a proud heart, [even] the lamp of the wicked, is sin.
Macho ya kiburi na moyo wa majivuno- taa ya waovu- ni dhambi.
5 The thoughts of the diligent [tend] only to plenteousness: but every one that is hasty [hasteth] only to want.
Mipango ya mwenye juhudi huelekea kwenye mafanikio tu, bali kila mtu anayetenda kwa haraka huelekea umasikini.
6 The getting of treasures by a lying tongue is a vapour driven to and fro; they [that seek them] seek death.
Kujipatia utajiri kwa ulimi wa uongo ni mvuke unaopita upesi na mtego ambao unafisha.
7 The violence of the wicked shall sweep them away; because they refuse to do judgment.
Vurugu ya waovu itawaburuta mbali, maana wanakataa kutenda haki.
8 The way of him that is laden with guilt is exceeding crooked: but as for the pure, his work is right.
Njia ya mwenye hatia ni ukatiri, bali mwenye usafi hutenda yaliyo ya haki.
9 It is better to dwell in the corner of the housetop, than with a contentious woman in a wide house.
Bora kuishi kwenye kona ya juu darini kuliko katika nyumba pamoja na mke mgonvi.
10 The soul of the wicked desireth evil: his neighbour findeth no favour in his eyes.
Hamu ya mwovu ni uchu wa mabaya; jirani yake haoni ukarimu katika macho yake.
11 When the scorner is punished, the simple is made wise: and when the wise is instructed, he receiveth knowledge.
Mwenye dhihaka anapoadhibiwa mjinga hupata busara, na mtu mwenye busara anapofundishwa, anaongeza maarifa.
12 The righteous man considereth the house of the wicked; [how] the wicked are overthrown to [their] ruin.
Atendaye haki huilinda nyumba ya mwovu; huwashusha waovu kwenye uharibifu.
13 Whoso stoppeth his ears at the cry of the poor, he also shall cry, but shall not be heard.
Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
14 A gift in secret pacifieth anger, and a present in the bosom strong wrath.
Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
15 It is joy to the righteous to do judgment; but it is a destruction to the workers of iniquity.
Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
16 The man that wandereth out of the way of understanding shall rest in the congregation of the dead.
Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
17 He that loveth pleasure shall be a poor man: he that loveth wine and oil shall not be rich.
Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
18 The wicked is a ransom for the righteous; and the treacherous [cometh] in the stead of the upright.
Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
19 It is better to dwell in a desert land, than with a contentious and fretful woman.
Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
20 There is precious treasure and oil in the dwelling of the wise; but a foolish man swalloweth it up.
Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
21 He that followeth after righteousness and mercy findeth life, righteousness, and honour.
Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima.
22 A wise man scaleth the city of the mighty, and bringeth down the strength of the confidence thereof.
Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.
23 Whoso keepeth his mouth and his tongue keepeth his soul from troubles.
Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu.
24 The proud and haughty man, scorner is his name, he worketh in the arrogance of pride.
Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai.
25 The desire of the slothful killeth him; for his hands refuse to labour.
Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
26 There is that coveteth greedily all the day long: but the righteous giveth and withholdeth not.
Kwa siku nzima hupatwa na uchu na uchu zaidi, lakini atendaye haki hutoa na wala hazuii.
27 The sacrifice of the wicked is an abomination: how much more, when he bringeth it with a wicked mind!
Sadaka ya mwovu ni chukizo; huwa ni chukizo zaidi anapoileta kwa nia mbaya.
28 A false witness shall perish: but the man that heareth shall speak unchallenged.
Shahidi wa uongo ataangamia, bali anayesikiliza ataongea kwa muda wote.
29 A wicked man hardeneth his face: but as for the upright, he ordereth his ways.
Mtu mwovu huufanya uso wake kuwa mgumu, bali mtu mwadilifu ni thabiti juu ya njia zake.
30 There is no wisdom nor understanding nor counsel against the LORD.
Hakuna hekima, hakuna ufahamu, na hakuna shauri linaloweza kusimama kinyume na Yehova.
31 The horse is prepared against the day of battle: but victory is of the LORD,
Farasi hutayarishwa kwa siku ya mapigano, lakini ushindi hupatikana kwa Yehova.

< Proverbs 21 >