< Proverbs 10 >
1 The proverbs of Solomon. A wise son maketh a glad father: but a foolish son is the heaviness of his mother.
Mithali za Sulemani. Mwana mwenye hekima humfurahisha baba yake lakini mwana mpumbavu huleta majonzi kwa mama yake.
2 Treasures of wickedness profit nothing: but righteousness delivereth from death.
Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
3 The LORD will not suffer the soul of the righteous to famish: but he thrusteth away the desire of the wicked.
Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
4 He becometh poor that dealeth with a slack hand: but the hand of the diligent maketh rich.
Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
5 He that gathereth in summer is a wise son: [but] he that sleepeth in harvest is a son that causeth shame.
Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
6 Blessings are upon the head of the righteous: but violence covereth the mouth of the wicked.
Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
7 The memory of the just is blessed: but the name of the wicked shall rot.
Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
8 The wise in heart will receive commandments: but a prating fool shall fall.
Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
9 He that walketh uprightly walketh surely: but he that perverteth his ways shall be known.
Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
10 He that winketh with the eye causeth sorrow: but a prating fool shall fall.
Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
11 The mouth of the righteous is a fountain of life: but violence covereth the mouth of the wicked.
Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
12 Hatred stirreth up strifes: but love covereth all transgressions.
Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
13 In the lips of him that hath discernment wisdom is found: but a rod is for the back of him that is void of understanding.
Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
14 Wise men lay up knowledge: but the mouth of the foolish is a present destruction.
Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
15 The rich man’s wealth is his strong city: the destruction of the poor is their poverty.
Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
16 The labour of the righteous [tendeth] to life; the increase of the wicked to sin.
Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
17 He is in the way of life that heedeth correction: but he that forsaketh reproof erreth.
Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
18 He that hideth hatred is of lying lips; and he that uttereth a slander is a fool.
Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
19 In the multitude of words there wanteth not transgression: but he that refraineth his lips doeth wisely.
Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
20 The tongue of the righteous is as choice silver: the heart of the wicked is little worth.
Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
21 The lips of the righteous feed many: but the foolish die for lack of understanding.
Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
22 The blessing of the LORD, it maketh rich, and he addeth no sorrow therewith.
Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
23 It is as sport to a fool to do wickedness: and [so is] wisdom to a man of understanding.
Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
24 The fear of the wicked, it shall come upon him: and the desire of the righteous shall be granted.
Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
25 When the whirlwind passeth, the wicked is no more: but the righteous is an everlasting foundation.
Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
26 As vinegar to the teeth, and as smoke to the eyes, so is the sluggard to them that send him.
Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 The fear of the LORD prolongeth days: but the years of the wicked shall be shortened.
Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
28 The hope of the righteous [shall] be gladness: but the expectation of the wicked shall perish.
Matumaini ya wale watendao haki ndiyo furaha yao, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
29 The way of the LORD is a strong hold to the upright; but it is a destruction to the workers of iniquity.
Njia ya Yehova huwalinda wale wenye uadilifu, bali kwa waovu ni uhalibifu.
30 The righteous shall never be removed: but the wicked shall not dwell in the land.
Wale watendao haki hawataondolewa, bali waovu hawatabaki katika nchi.
31 The mouth of the righteous bringeth forth wisdom: but the froward tongue shall be cut off.
Katika kinywa cha wale watendao haki hutoka tunda la hekima, bali ulimi wa kupotosha utakatwa.
32 The lips of the righteous know what is acceptable: but the mouth of the wicked [speaketh] frowardness.
Midomo ya wale watendao mema huyajua yanayokubalika, bali kinywa cha waovu, huyajua yanayopotosha.