< Mark 3 >
1 And he entered again into the synagogue; and there was a man there which had his hand withered.
Yesu aliingia tena katika sunagogi na mle ndani mlikuwa na mtu aliyekuwa na mkono uliopooza.
2 And they watched him, whether he would heal him on the sabbath day; that they might accuse him.
Humo baadhi ya watu walimngojea amponye mtu huyo siku ya sabato ili wapate kumshtaki.
3 And he saith unto the man that had his hand withered, Stand forth.
Yesu akamwambia huyo mtu aliyekuwa na mkono uliopooza, “Njoo hapa katikati.”
4 And he saith unto them, Is it lawful on the sabbath day to do good, or to do harm? to save a life, or to kill? But they held their peace.
Kisha, akawauliza, “Je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuua?” Lakini wao hawakusema neno.
5 And when he had looked round about on them with anger, being grieved at the hardening of their heart, he saith unto the man, Stretch forth thy hand. And he stretched it forth: and his hand was restored.
Hapo akawatazama wote kwa hasira, akaona huzuni kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao. Kisha akamwambia huyo mtu, “Nyosha mkono wako!” Naye akaunyosha mkono wake, ukawa mzima tena.
6 And the Pharisees went out, and straightway with the Herodians took counsel against him, how they might destroy him.
Mara Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri pamoja na watu wa kikundi cha Herode jinsi ya kumwangamiza Yesu.
7 And Jesus with his disciples withdrew to the sea: and a great multitude from Galilee followed: and from Judaea,
Yesu aliondoka hapo pamoja na wanafunzi wake, akaenda kando ya ziwa, na umati wa watu ukamfuata. Watu hao walikuwa wametoka Yerusalemu, Yudea,
8 and from Jerusalem, and from Idumaea, and beyond Jordan, and about Tyre and Sidon, a great multitude, hearing what great things he did, came unto him.
Idumea, ng'ambo ya mto Yordani, Tiro na Sidoni. Watu hao wengi walimwendea Yesu kwa sababu ya kusikia mambo mengi aliyokuwa ameyatenda.
9 And he spake to his disciples, that a little boat should wait on him because of the crowd, lest they should throng him:
Yesu akawaambia wanafunzi wake wamtayarishie mashua moja, ili umati wa watu usije ukamsonga.
10 for he had healed many; insomuch that as many as had plagues pressed upon him that they might touch him.
Alikuwa amewaponya watu wengi, na wagonjwa wote wakawa wanamsonga ili wapate kumgusa.
11 And the unclean spirits, whensoever they beheld him, fell down before him, and cried, saying, Thou art the Son of God.
Na watu waliokuwa wamepagawa na pepo wachafu walipomwona, walijitupa chini mbele yake na kupaaza sauti, “Wewe ni Mwana wa Mungu!”
12 And he charged them much that they should not make him known.
Lakini Yesu akawaamuru kwa ukali wasimjulishe kwa watu.
13 And he goeth up into the mountain, and calleth unto him whom he himself would: and they went unto him.
Yesu alipanda kilimani, akawaita wale aliowataka. Basi, wakamwendea,
14 And he appointed twelve, that they might be with him, and that he might send them forth to preach,
naye akawateua watu kumi na wawili ambao aliwaita mitume, wakae naye, awatume kuhubiri
15 and to have authority to cast out devils:
na wawe na mamlaka ya kuwafukuza pepo.
16 and Simon he surnamed Peter;
Basi, hao kumi na wawili walioteuliwa ndio hawa: Simoni (ambaye Yesu alimpa jina, Petro),
17 and James the [son] of Zebedee, and John the brother of James; and them he surnamed Boanerges, which is, Sons of thunder:
Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo (Yesu aliwapa hawa ndugu wawili jina Boanerge, maana yake “wanangurumo”),
18 and Andrew, and Philip, and Bartholomew, and Matthew, and Thomas, and James the [son] of Alphaeus, and Thaddaeus, and Simon the Cananaean,
Andrea na Filipo, Batholomayo, Mathayo, Thoma, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkanani na
19 and Judas Iscariot, which also betrayed him. And he cometh into a house.
Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.
20 And the multitude cometh together again, so that they could not so much as eat bread.
Kisha Yesu alikwenda nyumbani. Umati wa watu ukakusanyika tena, hata Yesu na wafuasi wake wasiweze kupata nafasi ya kula chakula.
21 And when his friends heard it, they went out to lay hold on him: for they said, He is beside himself.
Basi, watu wa jamaa yake walipopata habari hiyo wakatoka kwenda kumchukua maana walikuwa wanasema kwamba amepatwa na wazimu.
22 And the scribes which came down from Jerusalem said, He hath Beelzebub, and, By the prince of the devils casteth he out the devils.
Nao walimu wa Sheria waliokuwa wametoka Yerusalemu, wakasema, “Ana Beelzebuli! Tena, anawafukuza pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo.”
23 And he called them unto him, and said unto them in parables, How can Satan cast out Satan?
Hapo Yesu akawaita, akawaambia kwa mifano, “Shetani anawezaje kumfukuza Shetani?
24 And if a kingdom be divided against itself, that kingdom cannot stand.
Ikiwa utawala mmoja umegawanyika makundimakundi yanayopigana, utawala huo hauwezi kudumu.
25 And if a house be divided against itself, that house will not be able to stand.
Tena, ikiwa jamaa moja imegawanyika makundimakundi yanayopingana, jamaa hiyo itaangamia.
26 And if Satan hath risen up against himself, and is divided, he cannot stand, but hath an end.
Ikiwa basi, utawala wa Shetani umegawanyika vikundivikundi hauwezi kudumu, bali utaangamia kabisa.
27 But no one can enter into the house of the strong [man], and spoil his goods, except he first bind the strong [man]; and then he will spoil his house.
“Hakuna mtu awezaye kuivamia nyumba ya mtu mwenye nguvu na kumnyang'anya mali yake, isipokuwa kwanza amemfunga huyo mtu mwenye nguvu; hapo ndipo atakapoweza kumnyang'anya mali yake.
28 Verily I say unto you, All their sins shall be forgiven unto the sons of men, and their blasphemies wherewith soever they shall blaspheme:
“Kweli nawaambieni, watu watasamehewa dhambi zao zote na kufuru zao zote;
29 but whosoever shall blaspheme against the Holy Spirit hath never forgiveness, but is guilty of an eternal sin: (aiōn , aiōnios )
lakini anayesema mabaya dhidi ya Roho Mtakatifu, hatasamehewa kamwe; ana hatia ya dhambi ya milele.” (aiōn , aiōnios )
30 because they said, He hath an unclean spirit.
(Yesu alisema hivyo kwa sababu walikuwa wanasema, “Ana pepo mchafu.”)
31 And there come his mother and his brethren; and, standing without, they sent unto him, calling him.
Mama yake Yesu na ndugu zake walifika hapo, wakasimama nje, wakampelekea ujumbe kutaka kumwona.
32 And a multitude was sitting about him; and they say unto him, Behold, thy mother and thy brethren without seek for thee.
Umati wa watu ulikuwa umekaa hapo kumzunguka. Basi, wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanataka kukuona.”
33 And he answereth them, and saith, Who is my mother and my brethren?
Yesu akawaambia, “Mama yangu na ndugu zangu ni kina nani?”
34 And looking round on them which sat round about him, he saith, Behold, my mother and my brethren!
Hapo akawatazama watu waliokuwa wamemzunguka, akasema, “Tazameni! Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.
35 For whosoever shall do the will of God, the same is my brother, and sister, and mother.
Mtu yeyote anayefanya anayotaka Mungu, huyo ndiye kaka yangu, dada yangu na mama yangu.”