< Mark 15 >
1 And straightway in the morning the chief priests with the elders and scribes, and the whole council, held a consultation, and bound Jesus, and carried him away, and delivered him up to Pilate.
Kulipopambazuka, makuhani wakuu walifanya shauri pamoja na wazee, walimu wa Sheria na Baraza lote, wakamfunga Yesu pingu, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato.
2 And Pilate asked him, Art thou the King of the Jews? And he answering saith unto him, Thou sayest.
Pilato akamwuliza Yesu, “Je, wewe ni mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
3 And the chief priests accused him of many things.
Makuhani wakuu wakamshtaki Yesu mambo mengi.
4 And Pilate again asked him, saying, Answerest thou nothing? behold how many things they accuse thee of.
Pilato akamwuliza tena Yesu, “Je, hujibu neno? Tazama wanavyotoa mashtaka mengi juu yako.”
5 But Jesus no more answered anything; insomuch that Pilate marveled.
Lakini Yesu hakujibu neno, hata pilato akashangaa.
6 Now at the feast he used to release unto them one prisoner, whom they asked of him.
Kila wakati wa sikukuu ya Pasaka, Pilato alikuwa na desturi ya kuwafungulia mfungwa mmoja waliyemtaka.
7 And there was one called Barabbas, [lying] bound with them that had made insurrection, men who in the insurrection had committed murder.
Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Baraba, ambaye alikuwa amefungwa pamoja na waasi wengine kwa kusababisha uasi na mauaji.
8 And the multitude went up and began to ask him [to do] as he was wont to do unto them.
Watu wengi wakamwendea Pilato wakamwomba awafanyie kama kawaida yake.
9 And Pilate answered them, saying, Will ye that I release unto you the King of the Jews?
Pilato akawauliza, “Je, mwataka niwafungulieni Mfalme wa Wayahudi?”
10 For he perceived that for envy the chief priests had delivered him up.
Alisema hivyo kwa sababu alijua wazi kwamba makuhani wakuu walimkabidhi Yesu kwake kwa sababu ya wivu.
11 But the chief priests stirred up the multitude, that he should rather release Barabbas unto them.
Lakini makuhani wakuu wakawachochea watu wamwombe Pilato awafungulie Baraba.
12 And Pilate again answered and said unto them, What then shall I do unto him whom ye call the King of the Jews?
Pilato akawauliza tena, “Basi, sasa mwataka nifanye nini na mtu huyu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
13 And they cried out again, Crucify him.
Watu wote wakapaaza sauti tena: “Msulubishe!”
14 And Pilate said unto them, Why, what evil hath he done? But they cried out exceedingly, Crucify him.
Lakini Pilato akawauliza, “Kwa nini! Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakazidi kupaaza sauti, “Msulubishe!”
15 And Pilate, wishing to content the multitude, released unto them Barabbas, and delivered Jesus, when he had scourged him, to be crucified.
Pilato alitaka kuuridhisha huo umati wa watu; basi, akamwachilia Baraba kutoka gerezani. Akaamuru Yesu apigwe viboko, kisha akamtoa asulubiwe.
16 And the soldiers led him away within the court, which is the Praetorium; and they call together the whole band.
Kisha askari walimpeleka Yesu ndani ukumbini, katika ikulu, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
17 And they clothe him with purple, and plaiting a crown of thorns, they put it on him;
Wakamvika vazi la rangi ya zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamwekea kichwani.
18 and they began to salute him, Hail, King of the Jews!
Wakaanza kumsalimu, “Shikamoo Mfalme wa Wayahudi!”
19 And they smote his head with a reed, and did spit upon him, and bowing their knees worshipped him.
Wakampiga kichwani kwa mwanzi, wakamtemea mate; wakampigia magoti na kumsujudia.
20 And when they had mocked him, they took off from him the purple, and put on him his garments. And they lead him out to crucify him.
Baada ya kumdhihaki, walimvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
21 And they compel one passing by, Simon of Cyrene, coming from the country, the father of Alexander and Rufus, to go [with them], that he might bear his cross.
Walipokuwa njiani, walikutana na mtu mmoja aitwaye Simoni, mwenyeji wa Kurene. Yeye alikuwa baba wa Aleksanda na Rufo, na wakati huo alikuwa akitoka shambani. Basi, wakamlazimisha auchukue msalaba wa Yesu.
22 And they bring him unto the place Golgotha, which is, being interpreted, The place of a skull.
Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha, maana yake, “Mahali pa Fuvu la Kichwa.”
23 And they offered him wine mingled with myrrh: but he received it not.
Wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini yeye akaikataa.
24 And they crucify him, and part his garments among them, casting lots upon them, what each should take.
Basi, wakamsulubisha, wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura waamue nani angepata nini.
25 And it was the third hour, and they crucified him.
Ilikuwa saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
26 And the superscription of his accusation was written over, THE KING OF THE JEWS.
Na mshtaka wake ulikuwa umeandikwa: “Mfalme wa Wayahudi.”
27 And with him they crucify two robbers; one on his right hand, and one on his left.
Pamoja naye waliwasulubisha wanyang'anyi wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
Hapo yakatimia Maandiko Matakatifu yanayosema, “Aliwekwa kundi moja na waovu.”
29 And they that passed by railed on him, wagging their heads, and saying, Ha! thou that destroyest the temple, and buildest it in three days,
Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana, wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe mwenye kuvunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu!
30 save thyself, and come down from the cross.
Sasa, shuka msalabani ujiokoe mwenyewe!”
31 In like manner also the chief priests mocking [him] among themselves with the scribes said, He saved others; himself he cannot save.
Nao makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria walimdhihaki wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi!
32 Let the Christ, the King of Israel, now come down from the cross, that we may see and believe. And they that were crucified with him reproached him.
Eti yeye ni Kristo, Mfalme wa Israeli! Basi, na ashuke msalabani ili tuone na kuamini.” Hata watu wale waliosulubiwa pamoja naye walimtukana.
33 And when the sixth hour was come, there was darkness over the whole land until the ninth hour.
Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa kulikuwa giza nchini kote.
34 And at the ninth hour Jesus cried with a loud voice, Eloi, Eloi, lama sabachthani? which is, being interpreted, My God, my God, why hast thou forsaken me?
Saa tisa alasiri Yesu akalia kwa sauti kubwa, “Eloi, Eloi, lema sabakthani?” Maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
35 And some of them that stood by, when they heard it, said, Behold, he calleth Elijah.
Baadhi ya watu waliosimama pale waliposikia hivyo, walisema, “Sikiliza! Anamwita Eliya!”
36 And one ran, and filling a sponge full of vinegar, put it on a reed, and gave him to drink, saying, Let be; let us see whether Elijah cometh to take him down.
Mtu mmoja akakimbia, akachovya sifongo katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe akisema, “Hebu tuone kama Eliya atakuja kumteremsha msalabani!”
37 And Jesus uttered a loud voice, and gave up the ghost.
Yesu akapaaza sauti kubwa, akakata roho.
38 And the veil of the temple was rent in twain from the top to the bottom.
Basi, pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini.
39 And when the centurion, which stood by over against him, saw that he so gave up the ghost, he said, Truly this man was the Son of God.
Jemadari mmoja aliyekuwa amesimama mbele yake aliona jinsi Yesu alivyolia kwa sauti na kukata roho, akasema, “Kweli mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
40 And there were also women beholding from afar: among whom [were] both Mary Magdalene, and Mary the mother of James the less and of Joses, and Salome;
Walikuwako pia wanawake waliotazama kwa mbali, miongoni mwao akiwa Maria toka mji wa Magdala, Salome, na Maria mama wa kina Yakobo mdogo na Yose.
41 who, when he was in Galilee, followed him, and ministered unto him; and many other women which came up with him unto Jerusalem.
Hawa walimfuata Yesu alipokuwa Galilaya na kumtumikia. Kulikuwa na wanawake wengine wengi waliokuja Yerusalemu pamoja naye.
42 And when even was now come, because it was the Preparation, that is, the day before the sabbath,
Wakati wa jioni ulikuwa umekwisha fika. Hiyo ilikuwa siku ya Maandalio, yaani siku inayotangulia Sabato.
43 there came Joseph of Arimathaea, a councillor of honourable estate, who also himself was looking for the kingdom of God; and he boldly went in unto Pilate, and asked for the body of Jesus.
Hapo akaja Yosefu mwenyeji wa Armathaya, mjumbe wa Baraza Kuu, aliyeheshimika sana. Yeye pia alikuwa anatazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Basi, alimwendea Pilato bila uoga, akaomba apewe mwili wa Yesu.
44 And Pilate marveled if he were already dead: and calling unto him the centurion, he asked him whether he had been any while dead.
Pilato alishangaa kusikia kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa. Basi, akamwita jemadari, akamwuliza kama Yesu alikuwa amekufa kitambo.
45 And when he learned it of the centurion, he granted the corpse to Joseph.
Pilato alipoarifiwa na huyo jemadari kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa, akamruhusu Yosefu auchukue mwili wake.
46 And he bought a linen cloth, and taking him down, wound him in the linen cloth, and laid him in a tomb which had been hewn out of a rock; and he rolled a stone against the door of the tomb.
Hapo Yosefu akanunua sanda ya kitani, akauteremsha chini huo mwili, akauzungushia sanda. Akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa mwambani, kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango.
47 And Mary Magdalene and Mary the [mother] of Joses beheld where he was laid.
Nao Maria Magdalene na Maria mama yake Yose walipaona hapo alipolazwa.