< Luke 1 >
1 Forasmuch as many have taken in hand to draw up a narrative concerning those matters which have been fulfilled among us,
Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.
2 even as they delivered them unto us, which from the beginning were eyewitnesses and ministers of the word,
Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.
3 it seemed good to me also, having traced the course of all things accurately from the first, to write unto thee in order, most excellent Theophilus;
Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,
4 that thou mightest know the certainty concerning the things wherein thou wast instructed.
ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
5 There was in the days of Herod, king of Judaea, a certain priest named Zacharias, of the course of Abijah: and he had a wife of the daughters of Aaron, and her name was Elisabeth.
Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.
6 And they were both righteous before God, walking in all the commandments and ordinances of the Lord blameless.
Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.
7 And they had no child, because that Elisabeth was barren, and they both were [now] well stricken in years.
Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8 Now it came to pass, while he executed the priest’s office before God in the order of his course,
Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
9 according to the custom of the priest’s office, his lot was to enter into the temple of the Lord and burn incense.
Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
10 And the whole multitude of the people were praying without at the hour of incense.
Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
11 And there appeared unto him an angel of the Lord standing on the right side of the altar of incense.
Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
12 And Zacharias was troubled when he saw [him], and fear fell upon him.
Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
13 But the angel said unto him, Fear not, Zacharias: because thy supplication is heard, and thy wife Elisabeth shall bear thee a son, and thou shalt call his name John.
Lakini malaika akamwambia, “Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
14 And thou shalt have joy and gladness; and many shall rejoice at his birth.
Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15 For he shall be great in the sight of the Lord, and he shall drink no wine nor strong drink; and he shall be filled with the Holy Ghost, even from his mother’s womb.
Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16 And many of the children of Israel shall he turn unto the Lord their God.
Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
17 And he shall go before his face in the spirit and power of Elijah, to turn the hearts of the fathers to the children, and the disobedient [to walk] in the wisdom of the just; to make ready for the Lord a people prepared [for him].
Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake.”
18 And Zacharias said unto the angel, Whereby shall I know this? for I am an old man, and my wife well stricken in years.
Zakariya akamwambia huyo malaika, “Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu.”
19 And the angel answering said unto him, I am Gabriel, that stand in the presence of God; and I was sent to speak unto thee, and to bring thee these good tidings.
Malaika akamjibu, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.
20 And behold, thou shalt be silent and not able to speak, until the day that these things shall come to pass, because thou believedst not my words, which shall be fulfilled in their season.
Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia.”
21 And the people were waiting for Zacharias, and they marveled while he tarried in the temple.
Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.
22 And when he came out, he could not speak unto them: and they perceived that he had seen a vision in the temple: and he continued making signs unto them, and remained dumb.
Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
23 And it came to pass, when the days of his ministration were fulfilled, he departed unto his house.
Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.
24 And after these days Elisabeth his wife conceived; and she hid herself five months, saying,
Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:
25 Thus hath the Lord done unto me in the days wherein he looked upon [me], to take away my reproach among men.
“Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu.”
26 Now in the sixth month the angel Gabriel was sent from God unto a city of Galilee, named Nazareth,
Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,
27 to a virgin betrothed to a man whose name was Joseph, of the house of David; and the virgin’s name was Mary.
kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.
28 And he came in unto her, and said, Hail, thou that art highly favoured, the Lord [is] with thee.
Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe.”
29 But she was greatly troubled at the saying, and cast in her mind what manner of salutation this might be.
Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
30 And the angel said unto her, Fear not, Mary: for thou hast found favour with God.
Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
31 And behold, thou shalt conceive in thy womb, and bring forth a son, and shalt call his name JESUS.
Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.
32 He shall be great, and shall be called the Son of the Most High: and the Lord God shall give unto him the throne of his father David:
Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.
33 and he shall reign over the house of Jacob for ever; and of his kingdom there shall be no end. (aiōn )
Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn )
34 And Mary said unto the angel, How shall this be, seeing I know not a man?
Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?”
35 And the angel answered and said unto her, The Holy Ghost shall come upon thee, and the power of the Most High shall overshadow thee: wherefore also that which is to be born shall be called holy, the Son of God.
Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.
36 And behold, Elisabeth thy kinswoman, she also hath conceived a son in her old age: and this is the sixth month with her that was called barren.
Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.
37 For no word from God shall be void of power.
Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu.”
38 And Mary said, Behold, the handmaid of the Lord; be it unto me according to thy word. And the angel departed from her.
Maria akasema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema.” Kisha yule malaika akaenda zake.
39 And Mary arose in these days and went into the hill country with haste, into a city of Judah;
Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.
40 and entered into the house of Zacharias and saluted Elisabeth.
Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
41 And it came to pass, when Elisabeth heard the salutation of Mary, the babe leaped in her womb; and Elisabeth was filled with the Holy Ghost;
Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
42 and she lifted up her voice with a loud cry, and said, Blessed [art] thou among women, and blessed [is] the fruit of thy womb.
akasema kwa sauti kubwa, “Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
43 And whence is this to me, that the mother of my Lord should come unto me?
Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44 For behold, when the voice of thy salutation came into mine ears, the babe leaped in my womb for joy.
Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45 And blessed [is] she that believed; for there shall be a fulfillment of the things which have been spoken to her from the Lord.
Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia.”
46 And Mary said, My soul doth magnify the Lord,
Naye Maria akasema,
47 And my spirit hath rejoiced in God my Saviour.
“Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
48 For he hath looked upon the low estate of his handmaiden: For behold, from henceforth all generations shall call me blessed.
Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
49 For he that is mighty hath done to me great things; And holy is his name.
Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
50 And his mercy is unto generations and generations On them that fear him.
Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
51 He hath shewed strength with his arm; He hath scattered the proud in the imagination of their heart.
Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
52 He hath put down princes from [their] thrones, And hath exalted them of low degree.
amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
53 The hungry he hath filled with good things; And the rich he hath sent empty away.
Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
54 He hath holpen Israel his servant, That he might remember mercy
Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
55 (As he spake unto our fathers) Toward Abraham and his seed for ever. (aiōn )
Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele.” (aiōn )
56 And Mary abode with her about three months, and returned unto her house.
Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
57 Now Elisabeth’s time was fulfilled that she should be delivered; and she brought forth a son.
Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
58 And her neighbours and her kinsfolk heard that the Lord had magnified his mercy towards her; and they rejoiced with her.
Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
59 And it came to pass on the eighth day, that they came to circumcise the child; and they would have called him Zacharias, after the name of his father.
Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
60 And his mother answered and said, Not so; but he shall be called John.
Lakini mama yake akasema, “La, sivyo, bali ataitwa Yohane.”
61 And they said unto her, There is none of thy kindred that is called by this name.
Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”
62 And they made signs to his father, what he would have him called.
Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
63 And he asked for a writing tablet, and wrote, saying, His name is John. And they marveled all.
Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.
64 And his mouth was opened immediately, and his tongue [loosed], and he spake, blessing God.
Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65 And fear came on all that dwelt round about them: and all these sayings were noised abroad throughout all the hill country of Judaea.
Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
66 And all that heard them laid them up in their heart, saying, What then shall this child be? For the hand of the Lord was with him.
Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
67 And his father Zacharias was filled with the Holy Ghost, and prophesied, saying,
Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
68 Blessed [be] the Lord, the God of Israel; For he hath visited and wrought redemption for his people,
“Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
69 And hath raised up a horn of salvation for us In the house of his servant David
Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
70 (As he spake by the mouth of his holy prophets which have been since the world began), (aiōn )
Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu, (aiōn )
71 Salvation from our enemies, and from the hand of all that hate us;
kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72 To shew mercy towards our fathers, And to remember his holy covenant;
Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
73 The oath which he sware unto Abraham our father,
Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
74 To grant unto us that we being delivered out of the hand of our enemies Should serve him without fear,
tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
75 In holiness and righteousness before him all our days.
kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
76 Yea and thou, child, shalt be called the prophet of the Most High: For thou shalt go before the face of the Lord to make ready his ways;
Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
77 To give knowledge of salvation unto his people In the remission of their sins,
kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.
78 Because of the tender mercy of our God, Whereby the dayspring from on high shall visit us,
Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,
79 To shine upon them that sit in darkness and the shadow of death; To guide our feet into the way of peace.
na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani.”
80 And the child grew, and waxed strong in spirit, and was in the deserts till the day of his shewing unto Israel.
Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.