< Luke 18 >

1 And he spake a parable unto them to the end that they ought always to pray, and not to faint;
Basi, Yesu aliwasimulia mfano kuonyesha kwamba ni lazima kusali daima bila kukata tamaa.
2 saying, There was in a city a judge, which feared not God, and regarded not man:
Alisema: “Katika mji mmoja kulikuwa na hakimu ambaye hakuwa anamcha Mungu wala kumjali binadamu.
3 and there was a widow in that city; and she came oft unto him, saying, Avenge me of mine adversary.
Katika mji huohuo, kulikuwa pia na mama mmoja mjane, ambaye alimwendea huyo hakimu mara nyingi akimwomba amtetee apate haki yake kutoka kwa adui yake.
4 And he would not for a while: but afterward he said within himself, Though I fear not God, nor regard man;
Kwa muda mrefu huyo hakimu hakupenda kumtetea huyo mjane; lakini, mwishowe akajisemea: Ingawa mimi simchi Mungu wala simjali binadamu,
5 yet because this widow troubleth me, I will avenge her, lest she wear me out by her continual coming.
lakini kwa vile huyu mjane ananisumbua, nitamtetea; la sivyo ataendelea kufika hapa, na mwisho atanichosha kabisa!”
6 And the Lord said, Hear what the unrighteous judge saith.
Basi, Bwana akaendelea kusema, “Sikieni jinsi alivyosema huyo hakimu mbaya.
7 And shall not God avenge his elect, which cry to him day and night, and he is longsuffering over them?
Je, ndio kusema Mungu hatawatetea wale aliowachagua, ambao wanamlilia mchana na usiku? Je, atakawia kuwasikiliza?
8 I say unto you, that he will avenge them speedily. Howbeit when the Son of man cometh, shall he find faith on the earth?
Nawaambieni atawatetea upesi. Hata hivyo, je, kutakuwako na imani duniani wakati Mwana wa Mtu atakapokuja?”
9 And he spake also this parable unto certain which trusted in themselves that they were righteous, and set all others at nought:
Halafu Yesu aliwaambia pia mfano wa wale ambao walijiona kuwa wema na kuwadharau wengine.
10 Two men went up into the temple to pray; the one a Pharisee, and the other a publican.
“Watu wawili walipanda kwenda Hekaluni kusali: mmoja Mfarisayo, na mwingine mtoza ushuru.
11 The Pharisee stood and prayed thus with himself, God, I thank thee, that I am not as the rest of men, extortioners, unjust, adulterers, or even as this publican.
Huyo Mfarisayo akasimama, akasali kimoyomoyo: Ee Mungu, nakushukuru kwa vile mimi si kama watu wengine: walafi, wadanganyifu au wazinzi. Nakushukuru kwamba mimi si kama huyu mtoza ushuru.
12 I fast twice in the week; I give tithes of all that I get.
Nafunga mara mbili kwa juma, natoa zaka sehemu ya kumi ya pato langu.
13 But the publican, standing afar off, would not lift up so much as his eyes unto heaven, but smote his breast, saying, God, be merciful to me a sinner.
Lakini yule mtoza ushuru, akiwa amesimama kwa mbali bila hata kuinua macho yake mbinguni, ila tu akijipiga kifua kwa huzuni, alisema: Ee Mungu, unionee huruma mimi mwenye dhambi.
14 I say unto you, This man went down to his house justified rather than the other: for every one that exalteth himself shall be humbled; but he that humbleth himself shall be exalted.
Nawaambieni, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amesamehewa. Lakini yule mwingine, sivyo. Kwa maana kila anayejikweza atashushwa, na kila anayejishusha atakwezwa.”
15 And they brought unto him also their babes, that he should touch them: but when the disciples saw it, they rebuked them.
Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono yake. Wanafunzi walipowaona, wakawazuia kwa maneno makali.
16 But Jesus called them unto him, saying, Suffer the little children to come unto me, and forbid them not: for of such is the kingdom of God.
Lakini Yesu akawaita kwake akisema: “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu kama hawa.
17 Verily I say unto you, Whosoever shall not receive the kingdom of God as a little child, he shall in no wise enter therein.
Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hataingia katika Ufalme huo.”
18 And a certain ruler asked him, saying, Good Master, what shall I do to inherit eternal life? (aiōnios g166)
Kiongozi mmoja, Myahudi, alimwuliza Yesu, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niweze kuupata uzima wa milele?” (aiōnios g166)
19 And Jesus said unto him, Why callest thou me good? none is good, save one, [even] God.
Yesu akamwambia, “Mbona waniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
20 Thou knowest the commandments, Do not commit adultery, Do not kill, Do not steal, Do not bear false witness, Honour thy father and mother.
Unazijua amri: Usizini; usiue; usiibe; usitoe ushahidi wa uongo; waheshimu baba yako na mama yako.”
21 And he said, All these things have I observed from my youth up.
Yeye akasema, “Hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu.”
22 And when Jesus heard it, he said unto him, One thing thou lackest yet: sell all that thou hast, and distribute unto the poor, and thou shalt have treasure in heaven: and come, follow me.
Yesu aliposikia hayo akamwambia, “Unatakiwa bado kufanya kitu kimoja: uza kila ulicho nacho, wagawie maskini, na hivyo utakuwa na hazina yako mbinguni; halafu njoo unifuate.”
23 But when he heard these things, he became exceeding sorrowful; for he was very rich.
Lakini huyo mtu aliposikia hayo, alihuzunika sana kwa sababu alikuwa tajiri sana.
24 And Jesus seeing him said, How hardly shall they that have riches enter into the kingdom of God!
Yesu alipoona akihuzunika hivyo, akasema, “Jinsi gani ilivyo vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!
25 For it is easier for a camel to enter in through a needle’s eye, than for a rich man to enter into the kingdom of God.
Naam, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
26 And they that heard it said, Then who can be saved?
Wale watu waliposikia hayo, wakasema, “Nani basi, atakayeokolewa?”
27 But he said, The things which are impossible with men are possible with God.
Yesu akajibu, “Yasiyowezekana kwa binadamu, yanawezekana kwa Mungu.”
28 And Peter said, Lo, we have left our own, and followed thee.
Naye Petro akamwuliza, “Na sisi je? Tumeacha vitu vyote tukakufuata!”
29 And he said unto them, Verily I say unto you, There is no man that hath left house, or wife, or brethren, or parents, or children, for the kingdom of God’s sake,
Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, mtu yeyote aliyeacha nyumba au mke au kaka au wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,
30 who shall not receive manifold more in this time, and in the world to come eternal life. (aiōn g165, aiōnios g166)
atapokea mengi zaidi wakati huu wa sasa, na kupokea uzima wa milele wakati ujao.” (aiōn g165, aiōnios g166)
31 And he took unto him the twelve, and said unto them, Behold, we go up to Jerusalem, and all the things that are written by the prophets shall be accomplished unto the Son of man.
Yesu aliwachukua kando wale kumi na wawili, akawaambia, “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu na huko kila kitu kilichoandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Mtu kitakamilishwa.
32 For he shall be delivered up unto the Gentiles, and shall be mocked, and shamefully entreated, and spit upon:
Kwa maana atakabidhiwa kwa watu wa mataifa nao watamtendea vibaya na kumtemea mate.
33 and they shall scourge and kill him: and the third day he shall rise again.
Watampiga mijeledi, watamuua; lakini siku ya tatu atafufuka.”
34 And they understood none of these things; and this saying was hid from them, and they perceived not the things that were said.
Lakini wao hawakuelewa hata kidogo jambo hilo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.
35 And it came to pass, as he drew nigh unto Jericho, a certain blind man sat by the way side begging:
Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.
36 and hearing a multitude going by, he inquired what this meant.
Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, “Kuna nini?”
37 And they told him, that Jesus of Nazareth passeth by.
Wakamwambia, “Yesu wa Nazareti anapita.”
38 And he cried, saying, Jesus, thou son of David, have mercy on me.
Naye akapaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
39 And they that went before rebuked him, that he should hold his peace: but he cried out the more a great deal, Thou son of David, have mercy on me.
Wale watu waliotangulia wakamkemea wakimwambia anyamaze; lakini yeye akazidi kupaza sauti: “Mwana wa Daudi, nihurumie;”
40 And Jesus stood, and commanded him to be brought unto him: and when he was come near, he asked him,
Yesu alisimama, akaamuru wamlete mbele yake. Yule kipofu alipofika karibu, Yesu akamwuliza,
41 What wilt thou that I should do unto thee? And he said, Lord, that I may receive my sight.
“Unataka nikufanyie nini?” Naye akamjibu, “Bwana, naomba nipate kuona tena.”
42 And Jesus said unto him, Receive thy sight: thy faith hath made thee whole.
Yesu akamwambia, “Ona! Imani yako imekuponya.”
43 And immediately he received his sight, and followed him, glorifying God: and all the people, when they saw it, gave praise unto God.
Na mara yule aliyekuwa kipofu akapata kuona, akamfuata Yesu akimtukuza Mungu. Watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.

< Luke 18 >