< John 13 >
1 Now before the feast of the passover, Jesus knowing that his hour was come that he should depart out of this world unto the Father, having loved his own which were in the world, he loved them unto the end.
Sasa kabla ya sikukuu ya pasaka, kwa sababu Yesu alifahamu kuwa saa yake imefika ambayo atatoka katika dunia hii kwenda kwa baba, akiwa amewapenda watu wake ambao walikuwa duniani, aliwapenda upeo.
2 And during supper, the devil having already put into the heart of Judas Iscariot, Simon’s [son], to betray him,
Na ibilisi alikuwa amewekwa tayari katika moyo wa Yuda Isikariote, mwana wa simoni, kumsaliti Yesu.
3 [Jesus], knowing that the Father had given all things into his hands, and that he came forth from God, and goeth unto God,
Yesu alifahamu kuwa baba ameweka vitu vyote katika mikono yake na kwamba ametoka kwa Mungu na alikuwa anakwenda tena kwa Mungu.
4 riseth from supper, and layeth aside his garments; and he took a towel, and girded himself.
Aliamka chakulani na akatandika chini vazi lake la nje. Kisha alichukua taulo na akajifunga mwenyewe.
5 Then he poureth water into the bason, and began to wash the disciples’ feet, and to wipe them with the towel wherewith he was girded.
Kisha akatia maji katika bakuli na akaanza kuwaosha miguu wanafunzi wake na kuwafuta na taulo ambayo alijifunga yeye mwenyewe.
6 So he cometh to Simon Peter. He saith unto him, Lord, dost thou wash my feet?
Akaja kwa Simoni Petro, na Petro akamwambia, “Bwana, Unataka kuniosha miguu yangu?”
7 Jesus answered and said unto him, What I do thou knowest not now; but thou shalt understand hereafter.
Yesu akajibu na kumwambia, “Nifanyalo hulijui sasa, lakini utaelewa baadaye.”
8 Peter saith unto him, Thou shalt never wash my feet. Jesus answered him, If I wash thee not, thou hast no part with me. (aiōn )
Petro akamwambia, “Hutaniosha miguu yangu kamwe.” Yesu akamjibu, “Ikiwa sitakuosha, hutakuwa na sehemu pamoja nami.” (aiōn )
9 Simon Peter saith unto him, Lord, not my feet only, but also my hands and my head.
Simoni Petro akamwambia, “Bwana, usinioshe miguu yangu tuu, bali pia na mikono na kichwa changu.”
10 Jesus saith to him, He that is bathed needeth not save to wash his feet, but is clean every whit: and ye are clean, but not all.
Yesu akamwambia, “Yeyote ambaye amekwisha kuoga haitaji kuoga isipokuwa miguu yake, na amekuwa safi mwili wake wote; ninyi mmekuwa safi, lakini si nyote.”
11 For he knew him that should betray him; therefore said he, Ye are not all clean.
Kwa kuwa Yesu alijua yule atakaye msaliti; hii ndiyo sababu alisema, si nyote mmekuwa safi.”
12 So when he had washed their feet, and taken his garments, and sat down again, he said unto them, Know ye what I have done to you?
Wakati Yesu alipokuwa amewaosha miguu yao na akiisha chukua vazi lake na kukaa tena, aliwaambia, “Je Mnaelewa kile ambacho nimewafanyia?
13 Ye call me, Master, and, Lord: and ye say well; for so I am.
Mnaniita mimi “Mwalimu” na Bwana hii mnasema kweli, maana ndivyo nilivyo.
14 If I then, the Lord and the Master, have washed your feet, ye also ought to wash one another’s feet.
Ikiwa mimi Bwana na mwalimu, nimewaosha miguu yenu, ninyi pia imewapasa kuwaosha wenzenu miguu.
15 For I have given you an example, that ye also should do as I have done to you.
Kwa kuwa nimewapa mfano ili kwamba ninyi pia mfanye kama mimi nilivyo fanya kwenu.
16 Verily, verily, I say unto you, A servant is not greater than his lord; neither one that is sent greater than he that sent him.
Amini, Amini, nawambia, mtumwa si mkuu kuliko bwana wake; wala yule ambaye ametumwa ni mkuu kuliko yule aliye mtuma.
17 If ye know these things, blessed are ye if ye do them.
Ikiwa unafahamu mambo haya, umebarikiwa ukiyatenda.
18 I speak not of you all: I know whom I have chosen: but that the scripture may be fulfilled, He that eateth my bread lifted up his heel against me.
Sisemi kuhusu ninyi nyote, kwa kuwa nawajua wale ambao nimewachagua - bali nasema haya ili kwamba maandiko yaweze kutimilizwa: 'Yeye alaye mkate wangu ameniinulia kisigino chake.'
19 From henceforth I tell you before it come to pass, that, when it is come to pass, ye may believe that I am [he].
Ninawambia hili sasa kabla halijatokea ili kwamba litakapotokea, muweze kuamini kuwa mimi NDIYE.
20 Verily, verily, I say unto you, He that receiveth whomsoever I send receiveth me; and he that receiveth me receiveth him that sent me.
“Amini, amini, nawambia, anipokeaye mimi humpokea ambaye nina mtuma, na yule anipokeaye mimi humpokea yule aliye nituma mimi.”
21 When Jesus had thus said, he was troubled in the spirit, and testified, and said, Verily, verily, I say unto you, that one of you shall betray me.
Wakati Yesu aliposema haya, alisumbuka rohoni, alishuhudia na kusema, “Amini, amini, nawambia kwamba mmoja wenu atanisaliti.”
22 The disciples looked one on another, doubting of whom he spake.
Wanafunzi wake wakatazamana, wakishangaa ni kwa ajili ya nani alizungumza.
23 There was at the table reclining in Jesus’ bosom one of his disciples, whom Jesus loved.
Kulikuwa katika meza, mmoja wa wanafunzi wake ameegama kifuani mwa Yesu yule ambaye Yesu alimpenda.
24 Simon Peter therefore beckoneth to him, and saith unto him, Tell [us] who it is of whom he speaketh.
Simoni Petro alimuuliza mwanafunzi huyu na kusema, “Twambie ni yupi ambaye kwake anazungumza.”
25 He leaning back, as he was, on Jesus’ breast saith unto him, Lord, who is it?
Mwanafunzi yule aliye egama kifuani mwa Yesu na akamwambia, “Bwana, ni nani?”
26 Jesus therefore answereth, He it is, for whom I shall dip the sop, and give it him. So when he had dipped the sop, he taketh and giveth it to Judas, [the son] of Simon Iscariot.
Kisha Yesu alijibu, “Ni kwake yule nitakaye chovya kipande cha mkate na kumpatia.” Hivyo alipo kuwa amechovya mkate, alimpatia Yuda mwana wa Simon Iskariote.
27 And after the sop, then entered Satan into him. Jesus therefore saith unto him, That thou doest, do quickly.
Na baada ya mkate, Shetani alimuingia. Kisha Yesu akamwambia, “Kile ambacho unataka kukifanya ukifanye haraka.”
28 Now no man at the table knew for what intent he spake this unto him.
Sasa hakuna mtu katika meza alijua sababu ya Yesu kusema jambo hili kwake.
29 For some thought, because Judas had the bag, that Jesus said unto him, Buy what things we have need of for the feast; or, that he should give something to the poor.
Baadhi yao walidhani kwamba, kwa sababu Yuda alishika mfuko wa fedha, Yesu alimwambia, “Nunua vitu tunavyohitaji kwa ajili ya sikukuu,” au kwamba anapaswa kutoa kitu kwa masikini.
30 He then having received the sop went out straightway: and it was night.
Baada ya Yuda kupokea mkate, alitoka nje harak; na ilikuwa usiku.
31 When therefore he was gone out, Jesus saith, Now is the Son of man glorified, and God is glorified in him;
Wakati Yuda alipokuwa ameondoka, Yesu alisema, “Sasa mwana wa Adam ametukuzwa, na Mungu ametukuzwa katika yeye.
32 and God shall glorify him in himself, and straightway shall he glorify him.
Mungu atamtukuza katika yeye mwenyewe, na atamtukuza haraka.
33 Little children, yet a little while I am with you. Ye shall seek me: and as I said unto the Jews, Whither I go, ye cannot come; so now I say unto you.
Watoto wadogo, niko pamoja nanyi kitambo kidogo. Mtanitafuta, na kama nilivyowambia Wayahudi, 'Niendako, hamuwezi kuja.' sasa nawambia ninyi, pia.
34 A new commandment I give unto you, that ye love one another; even as I have loved you, that ye also love one another.
Ninawapa amri mpya, kwamba mpendane; kama mimi nilivyo wapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi pia imewapasa kupendana ninyi kwa ninyi.
35 By this shall all men know that ye are my disciples, if ye have love one to another.
Kwa ajili ya hili watu watatambua kuwa ninyi ni wanafunzi wangu, ikiwa mna upendo kwa kila mmoja na mwingine.”
36 Simon Peter saith unto him, Lord, whither goest thou? Jesus answered, Whither I go, thou canst not follow me now; but thou shalt follow afterwards.
Simoni Petro alimwambia, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akajibu, “Mahali ninapokwenda kwa sasa hutaweza kunifuata, lakini utanifuata baadaye.”
37 Peter saith unto him, Lord, why cannot I follow thee even now? I will lay down my life for thee.
Petro akamwambia, “Bwana, kwa nini nisikufuate hata sasa? Mimi nitayatoa maisha yangu kwa ajili yako.”
38 Jesus answereth, Wilt thou lay down thy life for me? Verily, verily, I say unto thee, The cock shall not crow, till thou hast denied me thrice.
Yesu akajibu, “Je utayatoa maisha yako kwa ajili yangu? Amini amini nakwambia, jogoo hatawika kabla hujanikana mara tatu.”