< John 11 >

1 Now a certain man was sick, Lazarus of Bethany, of the village of Mary and her sister Martha.
Basi mtu mmoja jina lake Lazaro alikuwa mgonjwa. Yeye alikuwa akiishi Bethania kijiji cha Maria na Martha dada zake.
2 And it was that Mary which anointed the Lord with ointment, and wiped his feet with her hair, whose brother Lazarus was sick.
Huyu Maria, ambaye Lazaro kaka yake alikuwa mgonjwa, ndiye yule ambaye alimpaka Bwana mafuta na kuifuta miguu yake kwa nywele zake.
3 The sisters therefore sent unto him, saying, Lord, behold, he whom thou lovest is sick.
Hivyo hawa dada wawili walituma ujumbe kwa Yesu kumwambia, “Bwana, yule umpendaye ni mgonjwa.”
4 But when Jesus heard it, he said, This sickness is not unto death, but for the glory of God, that the Son of God may be glorified thereby.
Lakini Yesu aliposikia hayo, akasema, “Ugonjwa huu hautaleta mauti bali umetokea ili kudhihirisha utukufu wa Mungu, ili Mwana wa Mungu apate kutukuzwa kutokana na ugonjwa huu.”
5 Now Jesus loved Martha, and her sister, and Lazarus.
Pamoja na hivyo, ingawa Yesu aliwapenda Martha, Maria na Lazaro ndugu yao,
6 When therefore he heard that he was sick, he abode at that time two days in the place where he was.
baada ya kusikia kwamba Lazaro ni mgonjwa, aliendelea kukawia huko alikokuwa kwa siku mbili zaidi.
7 Then after this he saith to the disciples, Let us go into Judaea again.
Ndipo akawaambia wanafunzi wake, “Haya, turudi Uyahudi.”
8 The disciples say unto him, Rabbi, the Jews were but now seeking to stone thee; and goest thou thither again?
Wanafunzi wake wakamwambia, “Rabi, Wayahudi walikuwa wanataka kukupiga mawe, nawe unataka kurudi huko?”
9 Jesus answered, Are there not twelve hours in the day? If a man walk in the day, he stumbleth not, because he seeth the light of this world.
Yesu akawajibu, “Si kuna saa kumi na mbili za mchana katika siku moja? Wala watembeao mchana hawawezi kujikwaa kwa maana wanaona nuru ya ulimwengu huu.
10 But if a man walk in the night, he stumbleth, because the light is not in him.
Lakini wale watembeao usiku hujikwaa kwa sababu hakuna nuru ndani yao.”
11 These things spake he: and after this he saith unto them, Our friend Lazarus is fallen asleep; but I go, that I may awake him out of sleep.
Baada ya kusema haya, Yesu akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini naenda kumwamsha.”
12 The disciples therefore said unto him, Lord, if he is fallen asleep, he will recover.
Wanafunzi wakamwambia, “Bwana, kama amelala usingizi ataamka.”
13 Now Jesus had spoken of his death: but they thought that he spake of taking rest in sleep.
Hata hivyo, Yesu alikuwa anazungumzia kuwa Lazaro amekufa, lakini wanafunzi wake hawakuelewa, walidhani kwamba anasema Lazaro amelala usingizi tu.
14 Then Jesus therefore said unto them plainly, Lazarus is dead.
Kwa hiyo Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa.
15 And I am glad for your sakes that I was not there, to the intent ye may believe; nevertheless let us go unto him.
Hata hivyo nafurahi kwa kuwa sikuwepo huko kabla ya Lazaro kufa, ili mpate kuamini. Lakini sasa twendeni kwake.”
16 Thomas therefore, who is called Didymus, said unto his fellow-disciples, Let us also go, that we may die with him.
Tomaso aliyeitwa Pacha akawaambia wanafunzi wenzake, “Sisi nasi twendeni tukafe pamoja naye.”
17 So when Jesus came, he found that he had been in the tomb four days already.
Yesu alipowasili huko alikuta Lazaro amekuwa kaburini siku nne.
18 Now Bethany was nigh unto Jerusalem, about fifteen furlongs off;
Basi Bethania ulikuwa karibu na Yerusalemu umbali wa karibu maili mbili,
19 and many of the Jews had come to Martha and Mary, to console them concerning their brother.
na Wayahudi wengi walikuwa wamekuja kuwafariji Martha na Maria kwa ajili ya kufiwa na ndugu yao.
20 Martha therefore, when she heard that Jesus was coming, went and met him: but Mary still sat in the house.
Martha aliposikia kwamba Yesu anakuja, alitoka kwenda kumlaki, ila Maria alibaki nyumbani.
21 Martha therefore said unto Jesus, Lord, if thou hadst been here, my brother had not died.
Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.
22 And even now I know that, whatsoever thou shalt ask of God, God will give thee.
Lakini sasa ninajua kuwa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
23 Jesus saith unto her, Thy brother shall rise again.
Yesu akamwambia, “Ndugu yako atafufuka.”
24 Martha saith unto him, I know that he shall rise again in the resurrection at the last day.
Martha akamjibu, “Ninajua ya kuwa atafufuka wakati wa ufufuo wa wafu siku ya mwisho.”
25 Jesus said unto her, I am the resurrection, and the life: he that believeth on me, though he die, yet shall he live:
Yesu akamwambia, “Mimi ndiye huo ufufuo na uzima. Yeye aniaminiye mimi, hata akifa atakuwa anaishi
26 and whosoever liveth and believeth on me shall never die. Believest thou this? (aiōn g165)
na yeyote aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je, unasadiki haya?” (aiōn g165)
27 She saith unto him, Yea, Lord: I have believed that thou art the Christ, the Son of God, [even] he that cometh into the world.
Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana, ninaamini ya kuwa wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yeye ajaye ulimwenguni.”
28 And when she had said this, she went away, and called Mary her sister secretly, saying, The Master is here, and calleth thee.
Baada ya kusema haya Martha alikwenda, akamwita Maria dada yake faraghani na kumwambia, “Mwalimu yuko hapa anakuita.”
29 And she, when she heard it, arose quickly, and went unto him.
Maria aliposikia hivyo, akaondoka upesi akaenda mpaka alipokuwa Yesu.
30 (Now Jesus was not yet come into the village, but was still in the place where Martha met him.)
Yesu alikuwa hajaingia kijijini, bali alikuwa bado yuko mahali pale alipokutana na Martha.
31 The Jews then which were with her in the house, and were comforting her, when they saw Mary, that she rose up quickly and went out, followed her, supposing that she was going unto the tomb to weep there.
Wale Wayahudi waliokuwa pamoja na Maria nyumbani wakimfariji walipoona ameondoka haraka na kutoka nje, walimfuata wakidhani ya kwamba alikuwa anakwenda kule kaburini kulilia huko.
32 Mary therefore, when she came where Jesus was, and saw him, fell down at his feet, saying unto him, Lord, if thou hadst been here, my brother had not died.
Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa, alipiga magoti miguuni Pake na kusema, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.”
33 When Jesus therefore saw her weeping, and the Jews [also] weeping which came with her, he groaned in the spirit, and was troubled,
Yesu alipomwona Maria akilia na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye pia wakilia, Yesu alisikia uchungu moyoni, akafadhaika sana.
34 and said, Where have ye laid him? They say unto him, Lord, come and see.
Akauliza, “Mmemweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo upaone.”
35 Jesus wept.
Yesu akalia machozi.
36 The Jews therefore said, Behold how he loved him!
Ndipo Wayahudi wakasema, “Tazama jinsi alivyompenda Lazaro!”
37 But some of them said, Could not this man, which opened the eyes of him that was blind, have caused that this man also should not die?
Lakini wengine wakasema, “Je, yule aliyefungua macho ya kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife?”
38 Jesus therefore again groaning in himself cometh to the tomb. Now it was a cave, and a stone lay against it.
Yesu kwa mara nyingine akiwa amefadhaika sana, akafika penye kaburi. Hilo kaburi lilikuwa pango ambalo jiwe lilikuwa limewekwa kwenye ingilio lake.
39 Jesus saith, Take ye away the stone. Martha, the sister of him that was dead, saith unto him, Lord, by this time he stinketh: for he hath been [dead] four days.
Yesu akasema, “Liondoeni hilo jiwe.” Martha ndugu yake yule aliyekuwa amekufa akasema, “Lakini Bwana, wakati huu atakuwa ananuka kwani amekwisha kuwa kaburini siku nne.”
40 Jesus saith unto her, Said I not unto thee, that, if thou believedst, thou shouldest see the glory of God?
Yesu akamwambia, “Sikukuambia kwamba kama ukiamini utauona utukufu wa Mungu?”
41 So they took away the stone. And Jesus lifted up his eyes, and said, Father, I thank thee that thou heardest me.
Kwa hiyo wakaliondoa lile jiwe kutoka kaburini. Yesu akainua macho yake juu akasema, “Baba, ninakushukuru kwa kuwa wanisikia.
42 And I knew that thou hearest me always: but because of the multitude which standeth around I said it, that they may believe that thou didst send me.
Ninajua ya kuwa wewe hunisikia siku zote, lakini nimesema haya kwa ajili ya umati huu uliosimama hapa, ili wapate kuamini ya kuwa wewe umenituma.”
43 And when he had thus spoken, he cried with a loud voice, Lazarus, come forth.
Baada ya kusema haya, Yesu akapaza sauti yake akaita, “Lazaro, njoo huku!”
44 He that was dead came forth, bound hand and foot with grave-clothes; and his face was bound about with a napkin. Jesus saith unto them, Loose him, and let him go.
Yule aliyekuwa amekufa akatoka nje, mikono yake na miguu yake ikiwa imeviringishiwa vitambaa vya kitani na leso usoni pake. Yesu akawaambia, “Mfungueni, mwacheni aende zake.”
45 Many therefore of the Jews, which came to Mary and beheld that which he did, believed on him.
Hivyo Wayahudi wengi waliokuwa wamekuja kumfariji Maria, walipoona yale Yesu aliyoyatenda wakamwamini.
46 But some of them went away to the Pharisees, and told them the things which Jesus had done.
Lakini baadhi yao wakaenda kwa Mafarisayo na kuwaambia mambo Yesu aliyoyafanya.
47 The chief priests therefore and the Pharisees gathered a council, and said, What do we? for this man doeth many signs.
Kwa hiyo viongozi wa makuhani na Mafarisayo wakaita mkutano wa baraza. Wakaulizana, “Tufanyeje? Huyu mtu anafanya ishara nyingi.
48 If we let him thus alone, all men will believe on him: and the Romans will come and take away both our place and our nation.
Kama tukimwacha aendelee hivi, kila mtu atamwamini, nao Warumi watakuja na kupaharibu mahali petu patakatifu na taifa letu.”
49 But a certain one of them, Caiaphas, being high priest that year, said unto them, Ye know nothing at all,
Mmoja wao aliyeitwa Kayafa, ambaye alikuwa kuhani mkuu mwaka huo, akasema, “Ninyi hamjui kitu chochote!
50 nor do ye take account that it is expedient for you that one man should die for the people, and that the whole nation perish not.
Hamjui kwamba ni afadhali mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa lote liangamie?”
51 Now this he said not of himself: but being high priest that year, he prophesied that Jesus should die for the nation;
Hakusema haya kutokana na mawazo yake mwenyewe bali kama kuhani mkuu mwaka huo, alitabiri kuwa Yesu angelikufa kwa ajili ya taifa la Wayahudi,
52 and not for the nation only, but that he might also gather together into one the children of God that are scattered abroad.
wala si kwa ajili ya taifa hilo pekee, bali pia kwa ajili ya watoto wa Mungu waliotawanyika, ili kuwaleta pamoja na kuwafanya wawe wamoja.
53 So from that day forth they took counsel that they might put him to death.
Hivyo tangu siku hiyo wakawa wanafanya mipango ili wamuue Yesu.
54 Jesus therefore walked no more openly among the Jews, but departed thence into the country near to the wilderness, into a city called Ephraim; and there he tarried with the disciples.
Kwa hiyo Yesu akawa hatembei hadharani miongoni mwa Wayahudi, bali alijitenga akaenda sehemu iliyo karibu na jangwa kwenye kijiji kiitwacho Efraimu. Akakaa huko na wanafunzi wake.
55 Now the passover of the Jews was at hand: and many went up to Jerusalem out of the country before the passover, to purify themselves.
Basi Pasaka ya Wayahudi ilipokuwa imekaribia, watu wengi walitoka vijijini wakaenda Yerusalemu kabla ya Pasaka ili wakajitakase.
56 They sought therefore for Jesus, and spake one with another, as they stood in the temple, What think ye? That he will not come to the feast?
Watu wakawa wanamtafuta Yesu, nao waliposimama kwenye eneo la Hekalu waliulizana, Je, mtu huyu hatakuja kamwe kwenye Sikukuu?
57 Now the chief priests and the Pharisees had given commandment, that, if any man knew where he was, he should shew it, that they might take him.
Viongozi wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kuwa yeyote atakayejua mahali Yesu aliko, lazima atoe taarifa ili wapate kumkamata.

< John 11 >