< Job 40 >

1 Moreover the LORD answered Job, and said,
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 Shall he that cavilleth contend with the Almighty? he that argueth with God, let him answer it.
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 Then Job answered the LORD, and said,
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 Behold, I am of small account; what shall I answer thee? I lay mine hand upon my mouth.
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 Once have I spoken, and I will not answer; yea twice, but I will proceed no further.
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 Then the LORD answered Job out of the whirlwind, and said,
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 Gird up thy loins now like a man: I will demand of thee, and declare thou unto me.
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 Wilt thou even disannul my judgment? wilt thou condemn me, that thou mayest be justified?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 Or hast thou an arm like God? and canst thou thunder with a voice like him?
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 Deck thyself now with excellency and dignity; and array thyself with honour and majesty.
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 Pour forth the overflowings of thine anger: and look upon every one that is proud, and abase him.
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 Look on every one that is proud, [and] bring him low; and tread down the wicked where they stand.
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 Hide them in the dust together; bind their faces in the hidden [place].
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 Then wilt I also confess of thee that thine own right hand can save thee.
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 Behold now behemoth, which I made with thee; he eateth grass as all ox.
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 Lo now, his strength is in his loins, and his force is in the muscles of his belly.
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 He moveth his tail like a cedar: the sinews of his thighs are knit together.
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 His bones are as tubes of brass; his limbs are like bars of iron.
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 He is the chief of the ways of God: he [only] that made him can make his sword to approach [unto him].
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 Surely the mountains bring him forth food; where all the beasts of the field do play.
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 He lieth under the lotus trees, in the covert of the reed, and the fen.
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 The lotus trees cover him with their shadow; the willows of the brook compass him about.
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 Behold, if a river overflow, he trembleth not: he is confident, though Jordan swell even to his mouth.
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 Shall any take him when he is on the watch, or pierce through his nose with a snare?
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?

< Job 40 >