< Job 40 >
1 Moreover the LORD answered Job, and said,
Bwana akamwambia Ayubu:
2 Shall he that cavilleth contend with the Almighty? he that argueth with God, let him answer it.
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 Then Job answered the LORD, and said,
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 Behold, I am of small account; what shall I answer thee? I lay mine hand upon my mouth.
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 Once have I spoken, and I will not answer; yea twice, but I will proceed no further.
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 Then the LORD answered Job out of the whirlwind, and said,
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 Gird up thy loins now like a man: I will demand of thee, and declare thou unto me.
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 Wilt thou even disannul my judgment? wilt thou condemn me, that thou mayest be justified?
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 Or hast thou an arm like God? and canst thou thunder with a voice like him?
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 Deck thyself now with excellency and dignity; and array thyself with honour and majesty.
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 Pour forth the overflowings of thine anger: and look upon every one that is proud, and abase him.
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 Look on every one that is proud, [and] bring him low; and tread down the wicked where they stand.
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 Hide them in the dust together; bind their faces in the hidden [place].
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 Then wilt I also confess of thee that thine own right hand can save thee.
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 Behold now behemoth, which I made with thee; he eateth grass as all ox.
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 Lo now, his strength is in his loins, and his force is in the muscles of his belly.
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 He moveth his tail like a cedar: the sinews of his thighs are knit together.
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 His bones are as tubes of brass; his limbs are like bars of iron.
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 He is the chief of the ways of God: he [only] that made him can make his sword to approach [unto him].
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 Surely the mountains bring him forth food; where all the beasts of the field do play.
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 He lieth under the lotus trees, in the covert of the reed, and the fen.
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 The lotus trees cover him with their shadow; the willows of the brook compass him about.
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 Behold, if a river overflow, he trembleth not: he is confident, though Jordan swell even to his mouth.
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 Shall any take him when he is on the watch, or pierce through his nose with a snare?
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?