< Job 36 >
1 Elihu also proceeded, and said,
Elihu aliendelea na kusema,
2 Suffer me a little, and I will shew thee: for I have yet somewhat to say on God’s behalf.
“Niruhusu niseme kidogo zaidi, nami nitakuonesha baadhi ya mambo kwasababu nina maneno machache ya kusema kwa ajili ya Mungu.
3 I will fetch my knowledge from afar, and will ascribe righteousness to my Maker.
Nitapata maarifa yangu kutoka mbali; nitatambua kwamba haki ni ya Muumba wangu.
4 For truly my words are not false: one that is perfect in knowledge is with thee.
Kwa kweli, maneno yangu hayatakuwa ya uongo; mtu fulani aliyekomaa katika maarifa yu pamoja nawe.
5 Behold, God is mighty, and despiseth not any: he is mighty in strength of understanding.
Angalia, Mungu ni mwenye nguvu, na hamdharau mtu yeyote; yeye ni mwenye nguvu katika uweza wa ufahamu.
6 He preserveth not the life of the wicked: but giveth to the afflicted [their] right.
Yeye huwa hayahifadhi maisha ya watu waovu bali badala yake hufanya yaliyo ya haki kwa wale wanaoteseka.
7 He withdraweth not his eyes from the righteous: but with kings upon the throne he setteth them for ever, and they are exalted.
Haondoi macho yake kwa wenye haki bali badala yake huwaweka juu ya viti vya enzi kama wafalme milele, nao wameinuliwa juu.
8 And if they be bound in fetters, and be taken in the cords of affliction;
Ikiwa wamefungwa minyororo na kunaswa katika kamba za mateso,
9 Then he sheweth them their work, and their transgressions, that they have behaved themselves proudly.
kisha huwafunulia kile walichokifanya, na maovu yao na kiburi chao.
10 He openeth also their ear to instruction, and commandeth that they return from iniquity.
Hufungua pia masikio yao kwa ajili ya agizo lake, na huwaamuru wageuke kutoka katika uovu.
11 If they hearken and serve [him], they shall spend their days in prosperity, and their years in pleasures.
Ikiwa watamsikiliza na kumwabudu yeye, wataishi katika mafanikio katika siku zao, na miaka yao katika hali ya kuridhika.
12 But if they hearken not, they shall perish by the sword, and they shall die without knowledge.
Hata hivyo, kama hawatasikiliza, wataangamia kwa upanga; watakufa kwasababu hawana maarifa.
13 But they that are godless in heart lay up anger: they cry not for help when he bindeth them.
Na wale wasiomjua Mungu hutunza hasiria zao katika mioyo; hawaombi msaada hata wakati ambapo Mungu huwafunga.
14 They die in youth, and their life [perisheth] among the unclean.
Hawa hufa katika ujana wao; na maisha yao hukoma kati ya makahaba.
15 He delivereth the afflicted by his affliction, and openeth their ear in oppression.
Mungu huwainua watu walioonewa kwa njia ya mateso yao; hufungua masikio yao kwa njia ya uonevu wao.
16 Yea, he would have led thee away out of distress into a broad place, where there is no straitness; and that which is set on thy table should be full of fatness.
Kwa hakika, yeye angependa kuwatoa ninyi katika mateso na kuwaweka katika sehemu pana ambapo hakuna masumbufu na mahali ambapo meza yenu ingewekwa ikiwa na chakula kilichojaa mafuta.
17 But thou art full of the judgment of the wicked: judgment and justice take hold [on thee].
Lakini wewe umejaa hukumu juu ya watu waovu; hukumu na haki umeziachilia.
18 Because there is wrath, beware lest thou be led away by [thy] sufficiency; neither let the greatness of the ransom turn thee aside.
Usiuache utajiri ukuvute katika udanganyifu; na sehemu kubwa ya rushwa isikugeuze upande kutoka katika haki.
19 Will thy riches suffice, [that thou be] not in distress, or all the forces of [thy] strength?
Je utajiri wako waweza kukunufaisha, ili kwamba usiwe katika taabu, au nguvu zako zote za uwezo zaweza kukusaidia?
20 Desire not the night, when peoples are cut off in their place.
Usiutamani usiku ili utende dhambi dhidi ya wengine wakati ambapo mataifa hukatiliwa mbali katika nafasi zao.
21 Take heed, regard not iniquity: for this hast thou chosen rather than affliction.
Uwe mwangalifu ili kwamba usigeukie dhambi kwasababu unajaribiwa kwa mateso ili kwamba ukae mbali na dhambi.
22 Behold, God doeth loftily in his power: who is a teacher like unto him?
Angalia, Mungu ameinuliwa katika nguvu zake; ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 Who hath enjoined him his way? or who can say, Thou hast wrought unrighteousness?
Ni nani alishamwalekeza njia yake? Nani anayeweza kumwambia, 'Wewe umetenda mambo yasiyo ya haki?'
24 Remember that thou magnify his work, whereof men have sung.
Kumbuka kuyasifu matendo yake, ambayo watu wameyaimba.
25 All men have looked thereon; man beholdeth it afar off.
Watu wote wameshayatazama hayo matendo, lakini wanayaona tu matendo hayo kwa mbali sana.
26 Behold, God is great, and we know him not; the number of his years is unsearchable.
Tazama, Mungu ni mkuu, lakini sisi hatumfahamu yeye vizuri; hesabu ya miaka yake haihesabiki.
27 For he draweth up the drops of water, which distil in rain from his vapour:
Kwa kuwa yeye huvuta matone ya maji ili kuyachuja kama mvua katka mvuke wake,
28 Which the skies pour down and drop upon man abundantly.
ambayo mawingu yake huyamwaga chini na kuyandondosha kwa wingi kwa mwanadamu.
29 Yea, can any understand the spreadings of the clouds, the thunderings of his pavilion?
Hakika, kuna hata mmoja awezaye kuelewa kwa undani kusambaa kwa mawingu na radi kutoka katika nyumba yake?
30 Behold, he spreadeth his light around him; and he covereth the bottom of the sea.
Angalia, hueneza mwanga wake kumzunguka na kufunika mizizi ya bahari.
31 For by these he judgeth the peoples; he giveth meat in abundance.
Kwa namna hii huyahukumu mataifa na kuwapa chakula kwa wingi.
32 He covereth his hands with the lightning; and giveth it a charge that it strike the mark.
Yeye huuijaza mikono yake kwa mwanga mpaka pale anapouamuru kupiga shabaha yake.
33 The noise thereof telleth concerning him, the cattle also concerning [the storm] that cometh up.
Na muungurumo wake huonya kwa dhoruba, wanyama wanaweza kusikia kuja kwake.