< Hosea 4 >

1 Hear the word of the LORD, ye children of Israel: for the LORD hath a controversy with the inhabitants of the land, because there is no truth, nor mercy, nor knowledge of God in the land.
Sikieni neno la Bwana, enyi Waisraeli, kwa sababu Bwana analo shtaka dhidi yenu ninyi mnaoishi katika nchi: “Hakuna uaminifu, hakuna upendo, hakuna kumjua Mungu katika nchi.
2 There is nought but swearing and breaking faith, and killing, and stealing, and committing adultery; they break out, and blood toucheth blood.
Kuna kulaani tu, uongo na uuaji, wizi na uzinzi, bila kuwa na mipaka, nao umwagaji damu mmoja baada ya mwingine.
3 Therefore shall the land mourn, and every one that dwelleth therein shall languish, with the beasts of the field and the fowls of heaven; yea, the fishes of the sea also shall be taken away.
Kwa sababu hii nchi huomboleza, wote waishio ndani mwake wanadhoofika, wanyama wa kondeni, ndege wa angani na samaki wa baharini wanakufa.
4 Yet let no man strive, neither let any man reprove; for thy people are as they that strive with the priest.
“Lakini mtu awaye yote na asilete shtaka, mtu yeyote na asimlaumu mwenzake, kwa maana watu wako ni kama wale waletao mashtaka dhidi ya kuhani.
5 And thou shalt stumble in the day, and the prophet also shall stumble with thee in the night; and I will destroy thy mother.
Unajikwaa usiku na mchana, nao manabii hujikwaa pamoja nawe. Kwa hiyo nitamwangamiza mama yako:
6 My people are destroyed for lack of knowledge: because thou hast rejected knowledge, I will also reject thee, that thou shalt be no priest to me: seeing thou hast forgotten the law of thy God, I also will forget thy children.
watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa, “Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeacha kuijali sheria ya Mungu wako mimi nami sitawajali watoto wako.
7 As they were multiplied, so they sinned against me: I will change their glory into shame.
Kadiri makuhani walivyoongezeka, ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu, walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.
8 They feed on the sin of my people, and set their heart on their iniquity.
Hujilisha dhambi za watu wangu na kupendezwa na uovu wao.
9 And it shall be, like people, like priest: and I will punish them for their ways, and will reward them their doings.
Hata itakuwa: Kama walivyo watu, ndivyo walivyo makuhani. Nitawaadhibu wote wawili kwa ajili ya njia zao na kuwalipa kwa matendo yao.
10 And they shall eat, and not have enough; they shall commit whoredom, and shall not increase: because they have left off to take heed to the LORD.
“Watakula lakini hawatashiba; watajiingiza katika ukahaba lakini hawataongezeka, kwa sababu wamemwacha Bwana na kujiingiza wenyewe
11 Whoredom and wine and new wine take away the understanding.
katika ukahaba, divai ya zamani na divai mpya, ambavyo huondoa ufahamu
12 My people ask counsel at their stock, and their staff declareth unto them: for the spirit of whoredom hath caused them to err, and they have gone a whoring from under their God.
wa watu wangu. Hutaka shauri kutoka kwa sanamu ya mti nao hujibiwa na fimbo ya mti. Roho ya ukahaba imewapotosha, hawana uaminifu kwa Mungu wao.
13 They sacrifice upon the tops of the mountains, and burn incense upon the hills, under oaks and poplars and terebinths, because the shadow thereof is good: therefore your daughters commit whoredom, and your brides commit adultery.
Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima na sadaka za kuteketezwa juu ya vilima, chini ya mialoni, milibua na miela, ambako kuna vivuli vizuri. Kwa hiyo binti zenu wamegeukia ukahaba na wake za wana wenu uzinzi.
14 I will not punish your daughters when they commit whoredom, nor your brides when they commit adultery; for they themselves go apart with whores, and they sacrifice with the harlots: and the people that doth not understand shall be overthrown.
“Sitawaadhibu binti zenu wakati wanapogeukia ukahaba, wala wake za wana wenu wanapofanya uzinzi, kwa sababu wanaume wenyewe huandamana na malaya na kutambikia pamoja na makahaba wa mahali pa kuabudia miungu: watu wasiokuwa na ufahamu wataangamia!
15 Though thou, Israel, play the harlot, yet let not Judah offend; and come not ye unto Gilgal, neither go ye up to Beth-aven, nor swear, As the LORD liveth.
“Ingawa umefanya uzinzi, ee Israeli, Yuda naye asije akawa na hatia. “Usiende Gilgali, usipande kwenda Beth-Aveni Wala usiape, ‘Hakika kama Bwana aishivyo!’
16 For Israel hath behaved himself stubbornly, like a stubborn heifer: now will the LORD feed them as a lamb in a large place.
Waisraeli ni wakaidi, kama mtamba wa ngʼombe ambaye ni mkaidi. Ni jinsi gani basi Bwana anaweza kuwachunga kama wana-kondoo katika shamba la majani?
17 Ephraim is joined to idols; let him alone.
Efraimu amejiunga na sanamu, ondokana naye!
18 Their drink is become sour: they commit whoredom continually; her rulers dearly love shame.
Hata wakati wamemaliza vileo vyao wanaendelea na ukahaba wao, watawala wao hupenda sana njia za aibu.
19 The wind hath wrapped her up in its wings; and they shall be ashamed because of their sacrifices.
Kisulisuli kitawafagilia mbali na dhabihu zao zitawaletea aibu.

< Hosea 4 >