< Genesis 46 >

1 And Israel took his journey with all that he had, and came to Beer-sheba, and offered sacrifices unto the God of his father Isaac.
Israeli akasafiri na yote aliyokuwa nayo na akaja Beersheba. Pale akatoa sadaka kwa Mungu wa Isaka baba yake.
2 And God spake unto Israel in the visions of the night, and said, Jacob, Jacob. And he said, Here am I.
Mungu akamwambia Israeli katika ndoto usiku, akisema, “Yakobo, Yakobo.”
3 And he said, I am God, the God of thy father: fear not to go down into Egypt; for I will there make of thee a great nation:
Akasema, “Mimi hapa.” Akasema, “Mimi ni Mungu, Mungu wa baba yako. Usiogope kushuka Misri, kwa maana nitakufanya taifa kubwa huko.
4 I will go down with thee into Egypt; and I will also surely bring thee up again: and Joseph shall put his hand upon thine eyes.
Nitakwenda pamoja nawe huko Misri, Nami nitakupandisha huku tena bila shaka. Na Yusufu akayafunika macho yako kwa mikono wake.”
5 And Jacob rose up from Beer-sheba: and the sons of Israel carried Jacob their father, and their little ones, and their wives, in the wagons which Pharaoh had sent to carry him.
Yakobo akainuka kutoka Beersheba. Wana wa Israeli wakamsafirisha Yakobo baba yao, watoto wao, na wake wao, katika mikokotene ambayo Farao alikuwa ameipeleka kuwachukua.
6 And they took their cattle, and their goods, which they had gotten in the land of Canaan, and came into Egypt, Jacob, and all his seed with him:
Wakachukua mifugo yao na mali zao walizokuwa wamezipata katika nchi ya Kanaani. Wakaja Misri, Yakobo na uzao wake wote pamoja naye.
7 his sons, and his sons’ sons with him, his daughters, and his sons’ daughters, and all his seed brought he with him into Egypt.
Akaja Misri pamoja na wanawe na wana wa wanawe, binti zake na wana wa binti zake, na uzao wake wote.
8 And these are the names of the children of Israel, which came into Egypt, Jacob and his sons: Reuben, Jacob’s firstborn.
Haya ni majina ya watoto wa Israeli waliokuja Misri, Yakobo na wanawe: Rubeni, mzaliwa wa kwanza wa Yakobo;
9 And the sons of Reuben; Hanoch, and Pallu, and Hezron, and Carmi.
wana wa Rubeni Hanoki na Palu na Hezroni na Karmi;
10 And the sons of Simeon; Jemuel, and Jamin, and Ohad, and Jachin, and Zohar, and Shaul the son of a Canaanitish woman.
wana wa Simoni, Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Zohari, na Shauli, wana wa mwanamke Mkanaani;
11 And the sons of Levi; Gershon, Kohath, and Merari.
wana wa Lawi Gershoni, Kohathi, na Merari.
12 And the sons of Judah; Er, and Onan, and Shelah, and Perez, and Zerah: but Er and Onan died in the land of Canaan. And the sons of Perez were Hezron and Hamul.
Wana wa Yuda: Eri, Shela, Peresi, na Zera, (Lakini Eri na Onani walikufa katika nchi ya Kanaani). Na wana wa Peresi walikuwa Hezroni na Hamuli.
13 And the sons of Issachar; Tola, and Puvah, and Iob, and Shimron.
Wana wa Isakari walikuwa Tola, Puva, Lobu, na Shimroni;
14 And the sons of Zebulun; Sered, and Elon, and Jahleel.
Wana wa Zabuloni walikuwa Seredi, Eloni, na Yahleeli
15 These are the sons of Leah, which she bare unto Jacob in Paddan-aram, with his daughter Dinah: all the souls of his sons and his daughters were thirty and three.
Hawa walikuwa wana wa Lea aliomzalia Yakobo huko Padani Aramu, pamoja na na Dina binti yake. Wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
16 And the sons of Gad; Ziphion, and Haggi, Shuni, and Ezbon, Eri, and Arodi, and Areli.
Wana wa Gadi walikuwa Zifioni, Hagi, Shuni, Ezboni, Eri, Arodi, na Areli.
17 And the sons of Asher; Imnah, and Ishvah, and Ishvi, and Beriah, and Serah their sister: and the sons of Beriah; Heber, and Malchiel.
Wana wa Asheri walikuwa Imna, Ishva, Ishvi, na Beria; na Sera alikuwa dada yao. Wana wa Beria walikuwa Heberi na Malkieli.
18 These are the sons of Zilpah, which Laban gave to Leah his daughter, and these she bare unto Jacob, even sixteen souls.
Hawa walikuwa wana wa Zilpa, ambaye Labani alikuwa amempa Lea binti yake. Wana aliomzalia Yakobo wote walikuwa kumi na sita.
19 The sons of Rachel Jacob’s wife; Joseph and Benjamin.
Wana wa Raheli mkewe Yakobo walikuwa Yusufu na Benjamini.
20 And unto Joseph in the land of Egypt were born Manasseh and Ephraim, which Asenath the daughter of Poti-phera priest of On bare unto him.
Huko Misri Manase na Efraimu walizaliwa kwa Yusufu na Asenathi, binti Potifera kuhani wa Oni.
21 And the sons of Benjamin; Bela, and Becher, and Ashbel, Gera, and Naaman, Ehi, and Rosh, Muppim, and Huppim, and Ard.
Wana wa Benjamini walikuwa Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu, na Ardi.
22 These are the sons of Rachel, which were born to Jacob: all the souls were fourteen.
Hawa walikuwa wana wa Raheli waliozaliwa kwa Yakobo - jumla yao kumi na wanne.
23 And the sons of Dan; Hushim.
Mwana wa Dani alikuwa Hushimu.
24 And the sons of Naphtali; Jahzeel, and Guni, and Jezer, and Shillem.
Wana wa Naftali walikuwa Yahzeeli, Guni, Yezeri, na Shilemi.
25 These are the sons of Bilhah, which Laban gave unto Rachel his daughter, and these she bare unto Jacob: all the souls were seven.
Hawa walikuwa wana Bilha aliomzalia Yakobo, ambaye Labani alimpa Raheli binti yake - wote walikuwa saba.
26 All the souls that came with Jacob into Egypt, which came out of his loins, besides Jacob’s sons’ wives, all the souls were threescore and six;
Wate waliokwenda na Yakobo, waliokuwa uzao wake, bila kuhesabu wake wa wana wa Yakobo walikuwa sitini na sita.
27 and the sons of Joseph, which were born to him in Egypt, were two souls: all the souls of the house of Jacob, which came into Egypt, were threescore and ten.
Pamoja na wana wawili wa Yusufu waliozaliwa kwake huko Misri, watu wa familia yake waliokwenda Misri walikuwa sabini jumla yao.
28 And he sent Judah before him unto Joseph, to shew the way before him unto Goshen; and they came into the land of Goshen.
Yakobo akamtuma Yuda kuwatangulia mbele kwa Yusufu kuonesha njia mbele yake kwenda Gosheni, nao wakaja katika eneo la Gosheni.
29 And Joseph made ready his chariot, and went up to meet Israel his father, to Goshen; and he presented himself unto him, and fell on his neck, and wept on his neck a good while.
Yusufu akaandaa kibandawazi chake na akaenda kumlaki baba yake huko Gosheni. Akamwona, akaikumbatia shingo yake, na akalia shingoni mwake kwa kitambo.
30 And Israel said unto Joseph, Now let me die, since I have seen thy face, that thou art yet alive.
Israeli akamwambia Yusufu, “Basi na nife sasa, kwa kuwa nimeuona uso wako, kwamba bado uko hai.”
31 And Joseph said unto his brethren, and unto his father’s house, I will go up, and tell Pharaoh, and will say unto him, My brethren, and my father’s house, which were in the land of Canaan, are come unto me;
Yusufu akawambia ndungu zake na nyumba ya baba yake, “Nitakwenda na kumwambia Farao, kusema, 'Ndugu zangu na nyumba ya baba yangu, waliokuwa katika nchi ya Kanaani, wamenijia.
32 and the men are shepherds, for they have been keepers of cattle; and they have brought their flocks, and their herds, and all that they have.
Watu hawa ni wafugaji, kwani wamekuwa watunza wanyama. Wamekuja na makundi yao ya kondoo, na mbuzi, na vyote walivyonavyo.'
33 And it shall come to pass, when Pharaoh shall call you, and shall say, What is your occupation?
Itakuwa, Farao atakapowaita na kuwauliza, 'Kazi yenu ni ipi?'
34 that ye shall say, Thy servants have been keepers of cattle from our youth even until now, both we, and our fathers: that ye may dwell in the land of Goshen; for every shepherd is an abomination unto the Egyptians.
mwambieni, 'Watumishi wako wamekuwa watunza wanyama tangu ujana wetu mpaka sasa, sisi, na baba zetu.' Fanyeni hivyo ili mweze kuishi katika nchi ya Gosheni, kwani kila mfugaji ni chukizo kwa Wamisri.”

< Genesis 46 >