< Ephesians 5 >
1 Be ye therefore imitators of God, as beloved children;
Kwa hiyo, mwigeni Mungu, maana ninyi ni watoto wake wapenzi.
2 and walk in love, even as Christ also loved you, and gave himself up for us, an offering and a sacrifice to God for an odour of a sweet smell.
Upendo uongoze maisha yenu, kama vile Kristo alivyotupenda, na kwa ajili yetu akajitoa mwenyewe kama dhabihu yenye harufu nzuri na tambiko impendezayo Mungu.
3 But fornication, and all uncleanness, or covetousness, let it not even be named among you, as becometh saints;
Kwa vile ninyi ni watu wa Mungu, basi uasherati, uchafu wowote ule au choyo visitajwe kamwe miongoni mwenu.
4 nor filthiness, nor foolish talking, or jesting, which are not befitting: but rather giving of thanks.
Tena maneno ya aibu, ya upuuzi au ubishi, yote hayo hayafai kwenu; maneno ya kumshukuru Mungu ndiyo yanayofaa.
5 For this ye know of a surety, that no fornicator, nor unclean person, nor covetous man, which is an idolater, hath any inheritance in the kingdom of Christ and God.
Jueni wazi kwamba mwasherati yeyote au mchafu au mfisadi, (ufisadi ni sawa na kuabudu sanamu), au mtu yeyote wa aina hiyo hataambulia chochote katika Utawala wa Kristo na wa Mungu.
6 Let no man deceive you with empty words: for because of these things cometh the wrath of God upon the sons of disobedience.
Msikubali kudanganywa na mtu kwa maneno matupu; maana, kwa sababu ya mambo kama hayo ghadhabu ya Mungu huwajia wote wasiomtii.
7 Be not ye therefore partakers with them;
Basi, msishirikiane nao.
8 For ye were once darkness, but are now light in the Lord: walk as children of light
Zamani ninyi mlikuwa gizani, lakini sasa ninyi mko katika mwanga kwa kuungana na Bwana. Ishini kama watoto wa mwanga:
9 (for the fruit of the light is in all goodness and righteousness and truth),
maana matokeo ya mwanga ni wema kamili, uadilifu na ukweli.
10 proving what is well-pleasing unto the Lord;
Jaribuni kujua yale yanayompendeza Bwana.
11 and have no fellowship with the unfruitful works of darkness, but rather even reprove them;
Msishiriki katika matendo yasiyofaa, ya giza bali yafichueni.
12 for the things which are done by them in secret it is a shame even to speak of.
Mambo yanayotendwa kwa siri ni aibu hata kuyataja.
13 But all things when they are reproved are made manifest by the light: for everything that is made manifest is light.
Lakini mambo yale yanayotendwa katika mwanga, ukweli wake hudhihirishwa;
14 Wherefore [he] saith, Awake, thou that sleepest, and arise from the dead, and Christ shall shine upon thee.
na kila kilichodhihirishwa huwa mwanga. Ndiyo maana Maandiko yasema: “Amka wewe uliyelala, fufuka kutoka wafu, naye Kristo atakuangaza.”
15 Look therefore carefully how ye walk, not as unwise, but as wise;
Basi, muwe waangalifu jinsi mnavyoishi: Msiishi kama wapumbavu, bali kama wenye hekima.
16 redeeming the time, because the days are evil.
Tumieni vizuri muda mlio nao maana siku hizi ni mbaya.
17 Wherefore be ye not foolish, but understand what the will of the Lord is.
Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.
18 And be not drunken with wine, wherein is riot, but be filled with the Spirit;
Acheni kulewa divai maana hiyo itawaangamiza, bali mjazwe Roho Mtakatifu.
19 speaking one to another in psalms and hymns and spiritual songs, singing and making melody with your heart to the Lord;
Zungumzeni kwa maneno ya Zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Bwana nyimbo na zaburi kwa shukrani mioyoni mwenu.
20 giving thanks always for all things in the name of our Lord Jesus Christ to God, even the Father;
Mshukuruni Mungu Baba daima kwa ajili ya yote, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
21 subjecting yourselves one to another in the fear of Christ.
Kila mmoja amstahi mwenzake kwa sababu ya kumcha Kristo.
22 Wives, [be in subjection] unto your own husbands, as unto the Lord.
Wake wawatii waume zao kama kumtii Bwana.
23 For the husband is the head of the wife, as Christ also is the head of the church, [being] himself the saviour of the body.
Maana mume anayo mamlaka juu ya mkewe, kama vile Kristo alivyo na mamlaka juu ya kanisa; naye Kristo mwenyewe hulikomboa kanisa, mwili wake.
24 But as the church is subject to Christ, so [let] the wives also [be] to their husbands in everything.
Kama vile kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo, wake wawatii waume zao katika mambo yote.
25 Husbands, love your wives, even as Christ also loved the church, and gave himself up for it;
Nanyi waume, wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa, akajitoa mwenyewe sadaka kwa ajili yake.
26 that he might sanctify it, having cleansed it by the washing of water with the word,
Alifanya hivyo, ili kwa neno lake, aliweke wakfu kwa Mungu, baada ya kulifanya safi kwa kuliosha katika maji,
27 that he might present the church to himself a glorious [church], not having spot or wrinkle or any such thing; but that it should be holy and without blemish.
kusudi ajipatie kanisa lililo takatifu na safu kabisa, kanisa lisilo na doa, kasoro au chochote cha namna hiyo.
28 Even so ought husbands also to love their own wives as their own bodies. He that loveth his own wife loveth himself:
Basi, waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.
29 for no man ever hated his own flesh; but nourisheth and cherisheth it, even as Christ also the church;
(Hakuna mtu yeyote auchukiaye mwili wake; badala ya kuuchukia, huulisha na kuuvika. Ndivyo naye Kristo anavyolitunza kanisa,
30 because we are members of his body.
maana sisi ni viungo vya mwili wake.)
31 For this cause shall a man leave his father and mother, and shall cleave to his wife; and the twain shall become one flesh.
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Kwa hiyo, mwanamume atawaacha baba na mama yake, ataungana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja.”
32 This mystery is great: but I speak in regard of Christ and of the church.
Kuna ukweli uliofichika katika maneno haya, nami naona kwamba yamhusu Kristo na kanisa lake.
33 Nevertheless do ye also severally love each one his own wife even as himself; and [let] the wife [see] that she fear her husband.
Lakini yanawahusu ninyi pia: kila mume lazima ampende mkewe kama nafsi yake mwenyewe, naye mke anapaswa kumstahi mumewe.