< 2 Corinthians 8 >
1 Moreover, brethren, we make known to you the grace of God which hath been given in the churches of Macedonia;
Basi sasa ndugu, nataka ninyi mjue kuhusu ile neema ambayo Mungu amewapa makanisa ya Makedonia.
2 how that in much proof of affliction the abundance of their joy and their deep poverty abounded unto the riches of their liberality.
Pamoja na majaribu makali na taabu walizopata, furaha waliyokuwa nayo ilikuwa kubwa, ingawa walikuwa maskini kupindukia, kwa upande wao walifurika kwa wingi wa ukarimu.
3 For according to their power, I bear witness, yea and beyond their power, [they gave] of their own accord,
Kwa maana nashuhudia kwamba wao walitoa kwa kadiri wawezavyo, hata na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe,
4 beseeching us with much entreaty in regard of this grace and the fellowship in the ministering to the saints:
wakitusihi kwa bidii wapewe fursa ya kushiriki katika huduma hii ya kuwasaidia watakatifu.
5 and [this], not as we had hoped, but first they gave their own selves to the Lord, and to us by the will of God.
Wala hawakufanya tulivyotazamia, bali walijitoa wao wenyewe kwa Bwana kwanza na ndipo wakajitoa kwa ajili yetu, kufuatana na mapenzi ya Mungu.
6 Insomuch that we exhorted Titus, that as he had made a beginning before, so he would also complete in you this grace also.
Kwa hiyo tulimsihi Tito, kwa kuwa ndiye alianzisha jambo hili, akamilishe tendo hili la neema kwa upande wenu.
7 But as ye abound in everything, [in] faith, and utterance, and knowledge, and [in] all earnestness, and [in] your love to us, [see] that ye abound in this grace also.
Lakini kama vile mlivyo mbele sana katika yote: Katika imani, katika usemi, katika maarifa, katika uaminifu wote na katika upendo wenu kwetu sisi, vivyo hivyo tunataka pia mzidi katika neema hii ya kutoa.
8 I speak not by way of commandment, but as proving through the earnestness of others the sincerity also of your love.
Siwaamrishi, lakini nataka kujaribu unyofu wa upendo wenu kwa kuulinganisha na bidii ya wengine.
9 For ye know the grace of our Lord Jesus Christ, that, though he was rich, yet for your sakes he became poor, that ye through his poverty might become rich.
Kwa maana mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba ingawa alikuwa tajiri, kwa ajili yenu alikubali kuwa maskini, ili kwa umaskini wake ninyi mpate kuwa matajiri.
10 And herein I give [my] judgment: for this is expedient for you, who were the first to make a beginning a year ago, not only to do, but also to will.
Ushauri wangu kuhusu lile lililo bora kwenu juu ya jambo hili ni huu: Mwaka uliopita ninyi mlikuwa wa kwanza si tu kutoa lakini pia mlikuwa na shauku ya kufanya hivyo.
11 But now complete the doing also; that as [there was] the readiness to will, so [there may be] the completion also out of your ability.
Sasa ikamilisheni kazi hii kwa shauku kama mlivyoanza, jitoleeni kulingana na uwezo wenu.
12 For if the readiness is there, [it is] acceptable according as [a man] hath, not according as [he] hath not.
Kwa kuwa kama nia ya kutoa ipo, kitolewacho kinakubalika kulingana na kile mtu alicho nacho, wala si kwa kile ambacho hana.
13 For [I say] not [this], that others may be eased, [and] ye distressed:
Nia yetu si kwamba wengine wasaidike wakati ninyi mnateseka, bali pawe na uwiano.
14 but by equality; your abundance [being a supply] at this present time for their want, that their abundance also may become [a supply] for your want; that there may be equality:
Kwa wakati huu, wingi wa vitu mlivyo navyo usaidie kutosheleza mahitaji yao, ili wakati wao watakapokuwa na wingi wa vitu, nao wapate kutosheleza mahitaji yenu.
15 as it is written, He that [gathered] much had nothing over; and he that [gathered] little had no lack.
Ndipo patakuwa na usawa, kama ilivyoandikwa: “Aliyekusanya zaidi hakuwa na ziada, wala aliyekusanya kidogo hakupungukiwa.”
16 But thanks be to God, which putteth the same earnest care for you into the heart of Titus.
Ninamshukuru Mungu ambaye amemtia Tito moyo wa kuwajali ninyi kama mimi ninavyowajali.
17 For indeed he accepted our exhortation; but being himself very earnest, he went forth unto you of his own accord.
Si kwamba Tito amekubali tu ombi letu, bali anakuja kwenu akiwa na shauku kuliko wakati mwingine, tena kwa hiari yake mwenyewe.
18 And we have sent together with him the brother whose praise in the gospel [is spread] through all the churches;
Nasi tunamtuma pamoja naye ndugu ambaye anasifiwa na makanisa yote kwa huduma yake ya kuhubiri Injili.
19 and not only so, but who was also appointed by the churches to travel with us in [the matter of] this grace, which is ministered by us to the glory of the Lord, and [to shew] our readiness:
Zaidi ya hayo, alichaguliwa na makanisa ili asafiri pamoja nasi tulipokuwa tunapeleka matoleo ya ukarimu, kwa ajili ya utukufu wa Bwana mwenyewe, na ili kuonyesha hisani yetu kuwasaidia.
20 Avoiding this, that any man should blame us in [the matter of] this bounty which is ministered by us:
Tunataka kuepuka lawama yoyote kuhusu jinsi tunavyosimamia matoleo haya ya ukarimu.
21 for we take thought for things honourable, not only in the sight of the Lord, but also in the sight of men.
Kwa kuwa tunakusudia kufanya kile kilicho haki si machoni mwa Bwana peke yake, bali pia machoni mwa watu wengine.
22 And we have sent with them our brother, whom we have many times proved earnest in many things, but now much more earnest, by reason of the great confidence which [he hath] in you.
Pamoja nao, tunamtuma ndugu yetu ambaye mara kwa mara ametuthibitishia kwa njia nyingi kwamba ana shauku, naam, zaidi sana sasa kwa sababu analo tumaini kuu kwenu.
23 Whether [any inquire] about Titus, [he is] my partner and [my] fellow-worker to you-ward; or our brethren, [they are] the messengers of the churches, [they are] the glory of Christ.
Kwa habari ya Tito, yeye ni mwenzangu na mtendakazi pamoja nami miongoni mwenu. Kwa habari za ndugu zetu, wao ni wawakilishi wa makanisa, na utukufu kwa Kristo.
24 Shew ye therefore unto them in the face of the churches the proof of your love, and of our glorying on your behalf.
Kwa hiyo waonyesheni wazi hawa ndugu uthibitisho wa upendo wenu na sababu inayotufanya tujivune kwa ajili yenu, mbele ya makanisa, ili yapate kuona.