< 1 Corinthians 15 >

1 Now I make known unto you brethren, the gospel which I preached unto you, which also ye received, wherein also ye stand,
Basi ndugu zangu nataka niwakumbushe kuhusu Injili niliyowahubiria, mkaipokea na ambayo katika hiyo mmesimama.
2 by which also ye are saved; [I make known, I say], in what words I preached it unto you, if ye hold it fast, except ye believed in vain.
Kwa Injili hii mnaokolewa mkishikilia kwa uthabiti neno nililowahubiria ninyi. La sivyo, mmeamini katika ubatili.
3 For I delivered unto you first of all that which also I received, how that Christ died for our sins according to the scriptures;
Kwa maana yale niliyopokea ndiyo niliyowapa ninyi, kama yenye umuhimu wa kwanza: Kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yasemavyo Maandiko,
4 and that he was buried; and that he hath been raised on the third day according to the scriptures;
ya kuwa alizikwa na alifufuliwa siku ya tatu, kama yasemavyo Maandiko,
5 and that he appeared to Cephas; then to the twelve;
na kwamba alimtokea Kefa, kisha akawatokea wale kumi na wawili.
6 then he appeared to above five hundred brethren at once, of whom the greater part remain until now, but some are fallen asleep;
Baadaye akawatokea wale ndugu waumini zaidi ya 500 kwa pamoja, ambao wengi wao bado wako hai, ingawa wengine wamelala.
7 then he appeared to James; then to all the apostles;
Ndipo akamtokea Yakobo na kisha mitume wote.
8 and last of all, as unto one born out of due time, he appeared to me also.
Mwisho wa wote, akanitokea mimi pia, ambaye ni kama aliyezaliwa si kwa wakati wake.
9 For I am the least of the apostles, that am not meet to be called an apostle, because I persecuted the church of God.
Kwa maana mimi ndiye mdogo kuliko mitume wote, nisiyestahili kuitwa mtume, kwa sababu nililitesa kanisa la Mungu.
10 But by the grace of God I am what I am: and his grace which was bestowed upon me was not found vain; but I laboured more abundantly than they all: yet not I, but the grace of God which was with me.
Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo na neema yake kwangu haikuwa kitu bure. Bali nilizidi sana kufanya kazi kuliko mitume wote, lakini haikuwa mimi, bali ni ile neema ya Mungu iliyokuwa pamoja nami.
11 Whether then [it be] I or they, so we preach, and so ye believed.
Hivyo basi, kama ilikuwa mimi au wao, hili ndilo tunalohubiri, na hili ndilo mliloamini.
12 Now if Christ is preached that he hath been raised from the dead, how say some among you that there is no resurrection of the dead?
Basi kama tumehubiri ya kwamba Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu, mbona baadhi yenu mnasema hakuna ufufuo wa wafu?
13 But if there is no resurrection of the dead, neither hath Christ been raised:
Lakini kama hakuna ufufuo wa wafu, basi hata Kristo hakufufuliwa.
14 and if Christ hath not been raised, then is our preaching vain, your faith also is vain.
Tena ikiwa Kristo hakufufuliwa kutoka kwa wafu, kuhubiri kwetu kumekuwa ni bure na imani yenu ni batili.
15 Yea, and we are found false witnesses of God; because we witnessed of God that he raised up Christ: whom he raised not up, if so be that the dead are not raised.
Zaidi ya hayo, twaonekana kuwa mashahidi wa uongo kuhusu Mungu, kwa sababu tumeshuhudia kumhusu Mungu kwamba alimfufua Kristo kutoka kwa wafu, lakini hilo haliwezi kuwa kweli kama wafu hawafufuliwi.
16 For if the dead are not raised, neither hath Christ been raised:
Kwa kuwa kama wafu hawafufuliwi, basi hata Kristo hajafufuka.
17 and if Christ hath not been raised, your faith is vain; ye are yet in your sins.
Tena kama Kristo hajafufuliwa, imani yenu ni batili; nanyi bado mko katika dhambi zenu.
18 Then they also which are fallen asleep in Christ have perished.
Hivyo basi, wote waliolala katika Kristo wamepotea.
19 If in this life only we have hoped in Christ, we are of all men most pitiable.
Ikiwa tumaini letu ndani ya Kristo ni kwa ajili ya maisha haya tu, sisi tunastahili kuhurumiwa kuliko watu wote.
20 But now hath Christ been raised from the dead, the firstfruits of them that are asleep.
Lakini kweli Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, tunda la kwanza la wale wote waliolala.
21 For since by man [came] death, by man [came] also the resurrection of the dead.
Kwa maana kama vile mauti ilivyokuja kwa njia ya mtu mmoja, vivyo hivyo, ufufuo wa wafu umekuja kwa njia ya mtu mmoja.
22 For as in Adam all die, so also in Christ shall all be made alive.
Kwa maana kama vile katika Adamu watu wote wanakufa, vivyo hivyo katika Kristo wote watafanywa hai.
23 But each in his own order: Christ the firstfruits; then they that are Christ’s, at his coming.
Lakini kila mmoja kwa wakati wake: Kristo, tunda la kwanza kisha, wale walio wake, wakati atakapokuja.
24 Then [cometh] the end, when he shall deliver up the kingdom to God, even the Father; when he shall have abolished all rule and all authority and power.
Ndipo mwisho utafika, wakati atakapomkabidhi Mungu Baba ufalme, akiisha angamiza kila utawala na kila mamlaka na nguvu.
25 For he must reign, till he hath put all his enemies under his feet.
Kwa maana lazima Kristo atawale mpaka awe amewaweka adui zake wote chini ya miguu yake.
26 The last enemy that shall be abolished is death.
Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni mauti.
27 For, He put all things in subjection under his feet. But when he saith, All things are put in subjection, it is evident that he is excepted who did subject all things unto him.
Kwa maana Mungu “ameweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Lakini isemapo kwamba “vitu vyote” vimewekwa chini yake, ni wazi kwamba Mungu aliyetiisha vitu vyote chini ya Kristo hayumo miongoni mwa hivyo vilivyotiishwa.
28 And when all things have been subjected unto him, then shall the Son also himself be subjected to him that did subject all things unto him, that God may be all in all.
Atakapokuwa amekwisha kuyafanya haya, ndipo Mwana mwenyewe atatiishwa chini yake yeye aliyetiisha vitu vyote, ili Mungu awe yote katika yote.
29 Else what shall they do which are baptized for the dead? If the dead are not raised at all, why then are they baptized for them?
Basi kama hakuna ufufuo, watafanyaje wale wabatizwao kwa ajili ya wafu? Kama wafu hawafufuliwi kamwe, mbona watu wanabatizwa kwa ajili yao?
30 Why do we also stand in jeopardy every hour?
Nasi kwa upande wetu kwa nini tunajihatarisha kila saa?
31 I protest by that glorying in you, brethren, which I have in Christ Jesus our Lord, I die daily.
Kama majivuno yangu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu Bwana wetu ni kweli, ndugu zangu, ninakufa kila siku.
32 If after the manner of men I fought with beasts at Ephesus, what doth it profit me? If the dead are not raised, let us eat and drink, for tomorrow we die.
Kama kwa sababu za kibinadamu tu nilipigana na wanyama wakali huko Efeso, ningekuwa nimepata faida gani? Kama wafu hawafufuliwi, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa.”
33 Be not deceived: Evil company doth corrupt good manners.
Msidanganyike: “Ushirika na watu wabaya huharibu tabia njema.”
34 Awake up righteously, and sin not; for some have no knowledge of God: I speak [this] to move you to shame.
Zindukeni mwe na akili kama iwapasavyo, wala msitende dhambi tena; kwa maana watu wengine hawamjui Mungu. Nasema mambo haya ili mwone aibu.
35 But some one will say, How are the dead raised? and with what manner of body do they come?
Lakini mtu anaweza kuuliza, “Wafu wafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani?”
36 Thou foolish one, that which thou thyself sowest is not quickened, except it die:
Ninyi wapumbavu kiasi gani? Mpandacho hakiwi hai kama hakikufa.
37 and that which thou sowest, thou sowest not the body that shall be, but a bare grain, it may chance of wheat, or of some other kind;
Mpandapo, hampandi mwili ule utakao kuwa, bali mwapanda mbegu tu, pengine ya ngano au ya kitu kingine.
38 but God giveth it a body even as it pleased him, and to each seed a body of its own.
Lakini Mungu huipa mbegu umbo kama alivyokusudia mwenyewe na kila aina ya mbegu huipa umbo lake.
39 All flesh is not the same flesh: but there is one [flesh] of men, and another flesh of beasts, and another flesh of birds, and another of fishes.
Kwa maana nyama zote si za aina moja. Binadamu wana nyama ya aina moja, wanyama wana aina nyingine, kadhalika ndege na samaki wana nyama tofauti.
40 There are also celestial bodies, and bodies terrestrial: but the glory of the celestial is one, and the [glory] of the terrestrial is another.
Pia kuna miili ya mbinguni na miili ya duniani, lakini fahari wa ile miili ya mbinguni ni wa aina moja na fahari wa ile miili ya duniani ni wa aina nyingine.
41 There is one glory of the sun, and another glory of the moon, and another glory of the stars; for one star differeth from another star in glory.
Jua lina fahari ya aina moja, mwezi nao una fahari yake na nyota pia, nazo nyota hutofautiana katika fahari.
42 So also is the resurrection of the dead. It is sown in corruption; it is raised in incorruption:
Hivyo ndivyo itakavyokuwa wakati wa ufufuo wa wafu. Ule mwili wa kuharibika uliopandwa, utafufuliwa usioharibika,
43 it is sown in dishonour; it is raised in glory: it is sown in weakness; it is raised in power:
unapandwa katika aibu, unafufuliwa katika utukufu, unapandwa katika udhaifu, unafufuliwa katika nguvu,
44 it is sown a natural body; it is raised a spiritual body. If there is a natural body, there is also a spiritual [body].
unapandwa mwili wa asili, unafufuliwa mwili wa kiroho. Kama kuna mwili wa asili, basi kuna mwili wa kiroho pia.
45 So also it is written, The first man Adam became a living soul. The last Adam [became] a life-giving spirit.
Kwa hiyo imeandikwa, “Mtu wa kwanza Adamu alifanyika kiumbe hai”; Adamu wa mwisho, yeye ni roho iletayo uzima.
46 Howbeit that is not first which is spiritual, but that which is natural; then that which is spiritual.
Lakini si ule wa kiroho uliotangulia, bali ni ule wa asili, kisha ule wa kiroho.
47 The first man is of the earth, earthy: the second man is of heaven.
Mtu wa kwanza aliumbwa kwa mavumbi ya ardhini, mtu wa pili alitoka mbinguni.
48 As is the earthy, such are they also that are earthy: and as is the heavenly, such are they also that are heavenly.
Kama vile alivyokuwa yule wa ardhini, ndivyo walivyo wale walio wa ardhini; na kwa vile alivyo mtu yule aliyetoka mbinguni, ndivyo walivyo wale walio wa mbinguni.
49 And as we have borne the image of the earthy, we shall also bear the image of the heavenly.
Kama vile tulivyochukua mfano wa mtu wa ardhini, ndivyo tutakavyochukua mfano wa yule mtu aliyetoka mbinguni.
50 Now this I say, brethren, that flesh and blood cannot inherit the kingdom of God; neither doth corruption inherit incorruption.
Ndugu zangu nisemalo ni hili: nyama na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu, wala kuharibika kurithi kutokuharibika.
51 Behold, I tell you a mystery: We shall not all sleep, but we shall all be changed,
Sikilizeni, nawaambia siri: Sote hatutalala, lakini sote tutabadilishwa
52 in a moment, in the twinkling of an eye, at the last trump: for the trumpet shall sound, and the dead shall be raised incorruptible, and we shall be changed.
ghafula, kufumba na kufumbua, parapanda ya mwisho itakapolia. Kwa kuwa parapanda italia, nao wafu watafufuliwa na miili isiyoharibika, nasi tutabadilishwa.
53 For this corruptible must put on incorruption, and this mortal must put on immortality.
Kwa maana mwili huu wa kuharibika lazima uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa lazima uvae kutokufa.
54 But when this corruptible shall have put on incorruption, and this mortal shall have put on immortality, then shall come to pass the saying that is written, Death is swallowed up in victory.
Kwa hiyo, mwili huu wa kuharibika utakapovaa kutokuharibika, nao huu mwili wa kufa utakapovaa kutokufa, ndipo lile neno lililoandikwa litakapotimia: “Mauti imemezwa kwa kushinda.”
55 O death, where is thy victory? O death, where is thy sting? (Hadēs g86)
“Kuko wapi, ee mauti, kushinda kwako? Uko wapi, ee mauti, uchungu wako?” (Hadēs g86)
56 The sting of death is sin; and the power of sin is the law:
Uchungu wa mauti ni dhambi na nguvu ya dhambi ni sheria.
57 but thanks be to God, which giveth us the victory through our Lord Jesus Christ.
Lakini ashukuriwe Mungu, yeye atupaye ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
58 Wherefore, my beloved brethren, be ye stedfast, unmoveable, always abounding in the work of the Lord, forasmuch as ye know that your labour is not vain in the Lord.
Kwa hiyo, ndugu zangu wapenzi, simameni imara, msitikisike, mzidi sana katika kuitenda kazi ya Bwana, kwa maana mnajua ya kuwa, kazi yenu katika Bwana si bure.

< 1 Corinthians 15 >