< 1 Chronicles 8 >
1 And Benjamin begat Bela his firstborn, Ashbel the second, and Aharah the third;
Benyamini akamzaa: Bela mzaliwa wake wa kwanza, Ashbeli mwanawe wa pili, Ahara mwanawe wa tatu,
2 Nohah the fourth, and Rapha the fifth.
Noha mwanawe wa nne na Rafa mwanawe wa tano.
3 And Bela had sons, Addar, and Gera, and Abihud;
Wana wa Bela walikuwa: Adari, Gera, Abihudi,
4 and Abishua, and Naaman, and Ahoah;
Abishua, Naamani, Ahoa,
5 and Gera, and Shephuphan, and Huram.
Gera, Shefufani na Huramu.
6 And these are the sons of Ehud: these are the heads of fathers’ [houses] of the inhabitants of Geba, and they carried them captive to Manahath:
Hawa ndio wazao wa Ehudi, waliokuwa viongozi wa jamaa za wale walioishi huko Geba na ambao walihamishiwa Manahathi:
7 and Naaman, and Ahijah, and Gera, he carried them captive; and he begat Uzza and Ahihud:
Naamani, Ahiya na Gera. Gera alikuwa baba yao Uza na Ahihudi na ndiye aliwaongoza kwenda uhamishoni.
8 And Shaharaim begat children in the field of Moab, after he had sent them away; Hushim and Baara were his wives.
Shaharaimu aliwazaa wana katika nchi ya Moabu baada ya kuwapa talaka wake zake wawili yaani, Hushimu na Baara.
9 And he begat of Hodesh his wife, Jobab, and Zibia, and Mesha, and Malcam;
Kwa mkewe Hodeshi, akawazaa wana saba: Yobabu, Sibia, Mesha, Malkamu,
10 and Jeuz, and Shachia, and Mirmah. These were his sons, heads of fathers’ [houses].
Yeuzi, Sakia na Mirma. Hawa ndio waliokuwa wanawe, viongozi wa jamaa zao.
11 And of Hushim he begat Abitub and Elpaal.
Hushimu alimzalia: Abitubu na Elpaali.
12 And the sons of Elpaal; Eber, and Misham, and Shemed, who built Ono and Lod, with the towns thereof:
Wana wa Elpaali walikuwa: Eberi, Mishamu, Shemedi (aliyeijenga miji ya Ono na Lodi, pamoja na vijiji vilivyoizunguka),
13 and Beriah, and Shema, who were heads of fathers’ [houses] of the inhabitants of Aijalon, who put to flight the inhabitants of Gath;
na Beria na Shema, waliokuwa viongozi wa zile jamaa zilizokuwa zinaishi katika mji wa Aiyaloni, na ambao waliwafukuza wenyeji wa Gathi.
14 and Ahio, Shashak, and Jeremoth;
Wana wa Beria walikuwa Ahio, Shashaki, Yeremothi,
15 and Zebadiah, and Arad, and Eder;
Zebadia, Aradi, Ederi,
16 and Michael, and Ishpah, and Joha, the sons of Beriah;
Mikaeli, Ishpa, na Yoha.
17 and Zebadiah, and Meshullam, and Hizki, and Heber;
Zebadia, Meshulamu, Hizki, Heberi,
18 and Ishmerai, and Izliah, and Jobab, the sons of Elpaal;
Ishmerai, Izlia na Yobabu ndio waliokuwa wana wa Elpaali.
19 and Jakim, and Zichri, and Zabdi;
Yakimu, Zikri, Zabdi,
20 and Elienai, and Zillethai, and Eliel;
Elienai, Silethai, Elieli,
21 and Adaiah, and Beraiah, and Shimrath, the sons of Shimei;
Adaya, Beraya na Shimrathi walikuwa wana wa Shimei.
22 and Ishpan, and Eber, and Eliel;
Wana wa Shashaki walikuwa Ishpani, Eberi, Elieli,
23 and Abdon, and Zichri, and Hanan;
Abdoni, Zikri, Hanani,
24 and Hananiah, and Elam, and Anthothijah;
Hanania, Elamu, Anthothiya,
25 and Iphdeiah, and Penuel, and sons of Shashak;
Ifdeya na Penueli.
26 and Shamsherai, and Shehariah, and Athaliah;
Shamsherai, Sheharia, Athalia,
27 and Jaareshiah, and Elijah, and Zichri, the sons of Jeroham.
Yaareshia, Eliya na Zikri walikuwa wana wa Yerohamu.
28 These were heads of fathers’ [houses] throughout their generations, chief men: these dwelt in Jerusalem.
Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao wakuu, kama ilivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.
29 And in Gibeon there dwelt the father of Gibeon, [Jeiel], whose wife’s name was Maacah:
Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka.
30 and his firstborn son Abdon, and Zur, and Kish, and Baal, and Nadab;
Mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,
31 and Gedor, and Ahio, and Zecher.
Gedori, Ahio, Zekeri,
32 And Mikloth begat Shimeah. And they also dwelt with their brethren in Jerusalem, over against their brethren.
na Miklothi ambaye alikuwa baba yake Shimea. Hawa pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu.
33 And Ner begat Kish; and Kish begat Saul; and Saul begat Jonathan, and Malchi-shua, and Abinadab, and Eshbaal.
Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli, Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.
34 And the son of Jonathan was Merib-baal; and Merib-baal begat Micah.
Yonathani akamzaa: Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika.
35 And the sons of Micah; Pithon, and Melech, and Tarea, and Ahaz.
Wana wa Mika walikuwa: Pithoni, Meleki, Tarea na Ahazi.
36 And Ahaz begat Jehoaddah; and Jehoaddah begat Alemeth, and Azmaveth, and Zimri; and Zimri begat Moza:
Ahazi akamzaa Yehoada. Naye Yehoada akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa.
37 And Moza begat Binea; Raphah was his son, Eleasah his son, Azel his son:
Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Rafa, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli.
38 And Azel had six sons, whose names are these; Azrikam, Bocheru, and Ishmael, and Sheariah, and Obadiah, and Hanan. All these were the sons of Azel.
Aseli alikuwa na wana sita; haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa wote ndio waliokuwa wana wa Aseli.
39 And the sons of Eshek his brother; Ulam his firstborn, Jeush the second, and Eliphelet the third.
Wana wa Esheki, nduguye Aseli, walikuwa: Mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Ulamu, wa pili Yeushi na wa tatu Elifeleti.
40 And the sons of Ulam were mighty men of valour, archers, and had many sons, and sons’ sons, an hundred and fifty. All these were of the sons of Benjamin.
Wana wa Ulamu walikuwa mashujaa hodari walioweza kutumia upinde. Alikuwa na wana wengi na wajukuu, jumla yao 150. Hawa wote ndio walikuwa wazao wa Benyamini.