< Revelation 10 >

1 Then I saw another mighty angel, descending from heaven. His robe was a cloud; over his head was the rainbow; his face was like the sun, and his feet like pillars of fire;
Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa amevikwa wingu na upinde wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake ulingʼaa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto.
2 in his hand he held a little book open. He set his right foot on the sea, and his left on the land;
Mkononi mwake alikuwa ameshika kijitabu kilichokuwa kimefunguliwa. Akauweka mguu wake wa kuume juu ya bahari na mguu wake wa kushoto akauweka juu ya nchi kavu.
3 and he cried in a loud voice like the roaring of a lion. At his cry the seven peals of thunder spoke, each with its own voice.
Naye akapiga kelele kwa sauti kuu kama simba anayenguruma. Alipopiga kelele, zile radi saba zikatoa ngurumo zake.
4 And, when they spoke, I was about to write; but I heard a voice from heaven say – ‘Keep secret what the seven peals of thunder said, and do not write it down.’
Nazo zile radi saba zilipotoa ngurumo, nilitaka kuanza kuandika, lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Yatie muhuri hayo yaliyosemwa na hizo radi saba na usiyaandike.”
5 Then the angel, whom I had seen standing on the sea and on the land, raised his right hand to the heavens,
Kisha yule malaika niliyekuwa nimemwona akiwa amesimama juu ya bahari na juu ya nchi akainua mkono wake wa kuume kuelekea mbinguni.
6 and swore by him who lives for ever and ever, who created the heavens and all that is in them, and the earth and all that is in it, and the sea and all that is in it, that time should cease to be. (aiōn g165)
Naye akaapa kwa Yule aishiye milele na milele, aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote viijazavyo, pamoja na bahari na vyote vilivyomo ndani yake, akasema, “Hakuna kungoja tena! (aiōn g165)
7 Moreover at the time when the seventh angel will speak, when he is ready to blow his blast, then the hidden purposes of God, of which he told the good news to his servants, the prophets, are at once fulfilled.
Lakini katika siku zile ambazo huyo malaika wa saba atakapokaribia kuipiga hiyo tarumbeta yake, siri ya Mungu itatimizwa, kama vile alivyowatangazia watumishi wake manabii.”
8 Then came the voice which I had heard from heaven. It spoke to me again, and said – ‘Go and take the book that is open in the hand of the angel who stands on the sea and on the land.’
Ndipo ile sauti niliyokuwa nimeisikia kutoka mbinguni ikasema nami tena ikaniambia, “Nenda, chukua kile kitabu kilichofunguliwa kilichoko mkononi mwa yule malaika aliyesimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu.”
9 So I went to the angel and asked him to give me the little book. And he said ‘Take it, and eat it. It will be bitter to your stomach, but in your mouth it will be as sweet as honey.’
Basi nikamwendea nikamwomba yule malaika anipe kile kitabu kidogo. Akaniambia, “Chukua na ukile. Kitakuwa kichungu tumboni mwako, lakini kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali.”
10 I took the little book out of the angel’s hand and ate it, and, while in my mouth, it was like the sweetest honey; but, when I had eaten it, it was bitter to my stomach.
Hivyo nikakichukua kile kitabu kidogo kutoka mkononi mwa yule malaika nikakila. Kilikuwa kitamu kama asali kinywani mwangu, lakini baada ya kukila, tumbo langu likatiwa uchungu.
11 And I was told – ‘You must prophesy again about men of many peoples, and nations, and languages, and about many kings.’
Kisha nikaambiwa, “Imekupasa kutoa unabii tena kuhusu makabila mengi, mataifa, lugha na wafalme.”

< Revelation 10 >