< Psalms 48 >
1 A song. A psalm of the Korahites. Great is the Lord and worthy all praise in the city of our God. His holy mountain,
Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
2 that rises so fair, is the joy of all the world. Like the mount of the gods is Mount Zion, the city of the great king.
Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
3 Once God made himself known as the defence of her palaces.
Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
4 For see! A concert of kings passed over the frontier together.
Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
5 But one glance, and they were astounded; they hastened away in dismay.
Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
6 Trembling took hold of them there, like the pains of a woman in labor.
Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
7 They were shattered, as east wind shatters the giant ships in pieces.
Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
8 What we heard, we now have seen in the city of the Lord of hosts, the city of our God. God will uphold her forever. (Selah)
Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
9 We think, O God, of your love, in the midst of your temple.
Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
10 Your fame, O God, like your name, shall extend to the ends of the earth. Victory fills your hand.
Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
11 Let mount Zion be glad; let the daughters of Judah rejoice because of your judgments.
Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
12 Walk about Zion, go round her; count her towers.
Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
13 Set your mind on her ramparts, consider her palaces; that you tell to the next generation
mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
14 That such is God, our God he it is who shall guide us for ever and ever.
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.