< Psalms 112 >
1 Hallelujah. Happy are those who fear the Lord, and greatly delight in his commandments.
Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
2 Mighty on earth shall be their seed; a blessing shall rest on the race of the upright.
Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
3 Wealth and riches are in their houses, their prosperity stands forever.
Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
4 To the upright arises light in the darkness; full of favor and pity and kindness are they.
Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
5 It is well with those who show pity and lend, who support all their affairs upon justice.
Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
6 For they will never be shaken; the just will be forever remembered.
Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
7 They will not be afraid of evil tidings, with steady heart they trust the Lord.
Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
8 Their heart is firm and unafraid: they know they will feast their eyes on their enemies.
Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
9 With lavish hands they give to the poor, and their prosperity stands forever. They are lifted to heights of triumph and honor.
Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
10 The sight of them fills the wicked with anger: grinding their teeth with despair. The hopes of the wicked will come to nothing.
Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.