< Psalms 106 >
1 Hallelujah! Give thanks to the Lord for his goodness, for his kindness endures forever.
Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2 Who can describe his heroic deeds, or publish all his praise?
Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
3 Happy they who act justly, and do righteousness evermore.
Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
4 Remember me, Lord, as you remember your people, and visit me with your gracious help.
Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
5 May I see the good fortune of your elect, may I share in the joy of your nation, and in the pride of your heritage.
ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
6 We, like our fathers, have sinned, we have done perversely and wickedly
Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
7 In the land of Egypt our fathers, all heedless of your wonders, and unmindful of your great kindness, at the Red Sea defied the Most High.
Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
8 But true to his name he saved them, in order to show his might.
Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
9 He rebuked the Red Sea, and it dried; they marched through the depths as through desert,
Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
10 saved from the hand of the hostile, redeemed from the hand of the foe.
Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
11 The waters covered their enemies: not one of them was left.
Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
12 So then they believed in his words, and began to sing his praise.
Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
13 But soon they forgot his deeds: they did not wait for his counsel.
Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
14 Their greed was ravenous in the desert; they put God to the test in the wilderness.
Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
15 He gave them the thing they had asked for, but sent wasting disease among them.
Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
16 The camp grew jealous of Moses and of Aaron, holy one of the Lord.
Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
17 The earth opened and swallowed up Dathan, and covered Abiram’s company.
Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
18 Fire broke out on their company, flame kindled upon the wicked.
Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
19 They made a calf in Horeb, and bowed to the molten image.
Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
20 They exchanged their glorious God for the image of ox that eats grass.
Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
21 They forgot the God who had saved them by mighty deeds in Egypt
Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
22 Wonders in the land of Ham, terrors by the Red Sea.
miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
23 So he vowed, and would have destroyed them, but for Moses his elect, who stepped into the breach before him, to divert his deadly wrath.
Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
24 They spurned the delightsome land, they refused to believe in his word.
Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
25 They grumbled in their tents, would not listen to the voice of the Lord.
Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
26 So he swore with uplifted hand to lay them low in the wilderness;
Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
27 to disperse their seed among heathen, to scatter them over the world.
kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
28 Then they joined them to Baal of Peor, and ate what was offered the dead.
Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
29 They provoked him to wrath by their deeds, and plague broke out among them.
Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
30 Then Phinehas stood between, and so the plague was stayed;
Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
31 and it was counted to him for righteousness unto all generations forever.
Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
32 They angered him at the waters of Meribah, through them it went ill with Moses.
Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
33 They rebelled against his spirit, and he uttered speech that was rash.
kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
34 They did not destroy the nations, as the Lord had commanded them;
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
35 but they mingled with the heathen, and learned to do as they did.
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
36 Their idol gods they worshipped, and they were ensnared by them.
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
37 They sacrificed their sons and their daughters to the demons.
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
38 They poured out innocent blood the blood of their sons and daughters whom they offered to Canaan’s idols, and the land was polluted with blood.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
39 They became unclean by their works, and adulterous in their deeds.
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
40 Then the Lord’s fury was on his people, filled with horror at his inheritance.
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
41 He delivered them to the heathen, to the sway of those who hated them.
Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
42 Their enemies oppressed them, and subdued them under their hand.
Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
43 Many a time he saved them, but they rebelled at his counsel, and were brought low by their wrongdoing.
Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
44 Yet he looked upon their distress, when he heard their cry.
Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
45 He remembered his covenant, and, in his great kindness, relented.
kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
46 He caused them to be pitied by all who carried them captive.
Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
47 Save us, O Lord our God, and gather us out of the nations, to give thanks to your holy name, and to make our boast of your praise.
Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
48 Blessed be the Lord, the God of Israel, from everlasting to everlasting. And let all the people say “Amen.” Praise the Lord.
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.