< Mark 4 >

1 Jesus again began to teach by the sea; and, as an immense crowd was gathering around him, he got into a boat, and sat in it on the sea, while all the people were on the shore at the water’s edge.
Yesu akaanza kufundisha tena kando ya bahari. Umati wa watu uliokuwa umekusanyika kumzunguka ulikuwa mkubwa, kiasi kwamba ilimbidi Yesu aingie kwenye mashua iliyokuwa baharini na kuketi humo, nao watu wote walikuwa ufuoni mwa bahari.
2 Then he taught them many truths in parables; and in the course of his teaching he said to them:
Akawafundisha mambo mengi kwa mifano, naye katika mafundisho yake akasema:
3 “Listen! The sower went out to sow;
“Sikilizeni! Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake.
4 and presently, as he was sowing, some of the seed fell along the path; and the birds came, and ate it up.
Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia, nao ndege wakaja na kuzila.
5 Some fell on rocky ground, where it had not much soil, and, because the soil wasn’t deep, sprang up at once;
Nyingine zilianguka kwenye ardhi yenye mwamba isiyo na udongo wa kutosha. Zikaota haraka, kwa kuwa udongo ulikuwa haba.
6 but, when the sun rose, it was scorched, and, because their roots were not deep enough, withered away.
Lakini jua lilipozidi, mimea ikanyauka na kukauka kwa kuwa mizizi yake haikuwa na kina.
7 Some of the seed fell among brambles; but the brambles shot up and completely choked it, and it yielded no return.
Mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo miiba hiyo ikakua, ikaisonga hiyo mimea, hivyo haikutoa mazao.
8 Some fell into good soil, and, shooting up and growing, yielded a return, amounting to thirty, sixty, and even a hundred fold.”
Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri, zikaota vizuri na kukua, zikatoa mazao, moja mara thelathini, nyingine mara sitini, na nyingine mara mia moja.”
9 And Jesus said, “Let anyone who has ears to hear with hear.”
Kisha Yesu akasema, “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
10 Afterward, when he was alone, his followers and the Twelve asked him about his parables;
Alipokuwa peke yake, watu waliokuwepo naye pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili wakamuuliza kuhusu mifano yake.
11 and he said, “To you the hidden truth of the kingdom of God has been imparted; but to those who are outside it all teaching takes the form of parables so that –
Naye akawaambia, “Ninyi mmepewa kujua siri ya Ufalme wa Mungu. Lakini kwa wale walioko nje, kila kitu husemwa kwao kwa mifano,
12 ‘Though they have eyes, they may see without perceiving; and though they have ears, they may hear without understanding; otherwise some day they might turn and be forgiven.’”
ili, “‘daima waone lakini wasitambue, daima wasikie lakini wasielewe; wasije wakageuka, wakatubu na kusamehewa!’”
13 “You do not know the meaning of this parable?” he went on, “Then how will you understand all the other parables?
Kisha Yesu akawauliza, “Hamwelewi maana ya mfano huu? Basi mtaelewaje mifano mingine?
14 The sower sows the message.
Yule mpanzi hupanda neno.
15 The people meant by the seed that falls along the path are these – where the message is sown, but, as soon as they have heard it, Satan immediately comes and carries away the message that has been sown in them.
Hawa ndio wale walio kando ya njia ambako neno lilipandwa. Walisikiapo neno, Shetani huja mara na kulinyakua lile neno lililopandwa ndani yao.
16 So, too, those meant by the seed sown on the rocky places are the people who, when they have heard the message, at once accept it joyfully;
Nazo zile mbegu zilizoanguka kwenye udongo wenye miamba, ni wale wanaolisikia neno, na mara hulipokea kwa furaha.
17 but, as they have no root, they stand only for a short time; and so, when trouble or persecution arises because of the message, they fall away at once.
Lakini kwa kuwa hawana mizizi, wao hudumu kwa muda mfupi tu. Kisha dhiki au mateso yanapoinuka kwa ajili ya lile neno, mara wao huiacha imani.
18 Those meant by the seed sown among the brambles are different; they are the people who hear the message,
Lakini wengine, kama mbegu iliyopandwa kwenye miiba, hulisikia lile neno;
19 but the cares of life, and the glamour of wealth, and cravings for many other things come in and completely choke the message, so that it gives no return. (aiōn g165)
lakini masumbufu ya maisha haya, na udanganyifu wa mali na tamaa ya mambo mengine huja na kulisonga lile neno na kulifanya lisizae. (aiōn g165)
20 But the people meant by the seed sown on the good ground are those who hear the message, and welcome it, and yield a return, thirty, sixty, and even a hundred fold.”
Wengine, kama mbegu iliyopandwa kwenye udongo mzuri, hulisikia lile neno, wakalipokea na kuzaa mazao. Wao huzaa mara thelathini, au mara sitini, au mara mia ya mbegu iliyopandwa.”
21 Jesus said to them, “Is a lamp brought to be put under a basket or under the couch, instead of being put on the lamp-stand?
Akawaambia, “Je, taa huwashwa na kufunikwa chini ya kikapu au mvunguni mwa kitanda? Je, haiwashwi na kuwekwa juu ya kinara chake?
22 There is nothing hidden that will not come to light and nothing is concealed that will not be brought into the open.
Kwa kuwa hakuna kilichofichika ambacho hakitafunuliwa, wala hakuna jambo lolote la siri ambalo halitaletwa nuruni.
23 Let all who have ears to hear with hear.
Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
24 “Take care what you listen to,” said Jesus. “The standard you use will be used for you, and more will be added for you.
Naye akawaambia, “Kuweni waangalifu na yale mnayosikia. Kipimo kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa ninyi, hata na zaidi.
25 For, to those who have, more will be given; while, from those who have nothing, even what they have will be taken away.”
Kwa maana kila mtu aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.”
26 Jesus also said, “This is what the kingdom of God is like – like a man who has scattered seed on the ground,
Pia akawaambia, “Ufalme wa Mungu unafanana na mtu apandaye mbegu shambani.
27 and then sleeps by night and rises by day, while the seed is shooting up and growing – he knows not how.
Akiisha kuzipanda, usiku na mchana, akiwa amelala au ameamka, mbegu huota na kukua pasipo yeye kujua ikuavyo.
28 The ground bears the crop of itself – first the blade, then the ear, and then the full grain in the ear;
Udongo huifanya iote kuwa mche, halafu suke, kisha nafaka kamili kwenye suke.
29 but, as soon as the crop is ready, immediately he puts in the sickle because harvest has come.”
Lakini nafaka inapokuwa imekomaa, mara mkulima huingia shambani na mundu wa kuvunia, maana mavuno yamekuwa tayari.”
30 Jesus also said, “To what can we liken the kingdom of God?
Akawaambia tena, “Tuufananishe Ufalme wa Mungu na nini? Au tutumie mfano gani ili kuueleza?
31 By what can we illustrate it? Perhaps by the growth of a mustard seed. This seed, when sown in the ground, though it is smaller than all other seeds,
Ni kama punje ya haradali, ambayo ni mbegu ndogo sana kuliko mbegu zote zinazopandwa ardhini.
32 yet, when sown, shoots up, and becomes larger than any other herb, and puts out great branches, so that even the wild birds can roost in its shelter.”
Lakini ikishaota, hukua ikawa mmea mkubwa kuliko yote ya bustanini, ikawa na matawi makubwa hata ndege wa angani wanaweza kujenga viota kwenye matawi yake.”
33 With many such parables Jesus used to speak to the people of his message, as far as they were able to receive it;
Kwa mifano mingine mingi kama hii Yesu alinena nao neno lake, kwa kadiri walivyoweza kulielewa.
34 and to them he never used to speak except in parables; but in private to his own disciples he explained everything.
Hakusema nao neno lolote pasipo mfano. Lakini alipokuwa na wanafunzi wake, aliwafafanulia kila kitu.
35 In the evening of the same day, Jesus said to them, “Let us go across.”
Siku hiyo ilipokaribia jioni, aliwaambia wanafunzi wake, “Tuvukeni twende mpaka ngʼambo.”
36 So, leaving the crowd behind, they took him with them, just as he was, in the boat; and there were other boats with him.
Wakauacha ule umati wa watu, na wakamchukua vile alivyokuwa kwenye mashua. Palikuwa pia na mashua nyingine nyingi pamoja naye.
37 A violent squall came on, and the waves kept dashing into the boat, so that the boat was actually filling.
Kukawa na dhoruba kali, nayo mawimbi yakaipiga ile mashua hata ikawa karibu kujaa maji.
38 Jesus was in the stern asleep on the cushion; and the disciples roused him and cried, “Teacher! Is it nothing to you that we are lost?”
Yesu alikuwa katika shetri, akiwa analala juu ya mto. Wanafunzi wake wakamwamsha, wakamwambia, “Mwalimu, hujali kama tunazama?”
39 Jesus rose and rebuked the wind, and said to the sea, “Hush! Be still!” Then the wind dropped, and a great calm followed.
Akaamka, akaukemea ule upepo, akayaambia yale mawimbi, “Uwe kimya! Tulia!” Ule upepo ukatulia, kukawa shwari kabisa.
40 “Why are you so timid?” he exclaimed. “Have you no faith yet?”
Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa nini mnaogopa hivyo? Je, bado hamna imani?”
41 But they were struck with great awe, and said to one another, “Who can this be that even the wind and the sea obey him?”
Nao wakawa wameogopa sana, wakaulizana, “Ni nani huyu ambaye hata upepo na mawimbi vinamtii?”

< Mark 4 >