< Psalms 30 >

1 A psalm of David. A song for the dedication of the Temple. I will extol you, O Lord, because you have lifted me up, and not suffered my foes to rejoice over me.
Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
2 I cried to you for help, O Lord my God, and you healed me.
Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
3 You have brought me up, Lord, from Sheol, from my way to the pit back to life you have called me. (Sheol h7585)
Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol h7585)
4 Sing praise to the Lord, faithful people; give thanks to his holy name.
Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
5 For his anger lasts only a moment, his favour endures for a lifetime. Weeping may lodge for the night, but the morning brings shouts of joy.
Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
6 When all went well, I imagined that never should I be shaken.
Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
7 For by your favour, O Lord, you had set me on mountains strong: but you hide your face, and I was confounded.
Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
8 Then to you, Lord, I cried, to the Lord I begged for mercy,
Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
9 ‘What profit is there in my blood, if I go down to the pit? Can you be praised by dust? Can it tell of your faithfulness?
“Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
10 Hear, Lord, and show me your favour, Lord be a helper to me.’
Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
11 You have turned my mourning to dancing; my sackcloth you have unloosed, and clothed me with joy:
Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
12 that unceasingly I should sing your praise, and give thanks to you, Lord my God, forever.
ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.

< Psalms 30 >