< Revelation 4 >

1 After this I saw, and lo! an open door in heaven; and the former voice, which I heard as of a trumpet speaking with me, said, Come up hither, and I will show thee what things must take place after these.
Baada ya mambo hayo nilitazama, nami nikaona mbele yangu mlango uliokuwa wazi mbinguni. Nayo ile sauti niliyokuwa nimeisikia hapo mwanzo ikisema nami kama tarumbeta ikasema, “Njoo, huku, nami nitakuonyesha yale ambayo hayana budi kutokea baada ya haya.”
2 Immediately I was in the Spirit; and lo! a throne was set ha heaven, and one sat on the throne.
Ghafula nilikuwa katika Roho, na hapo mbele yangu kilikuwepo kiti cha enzi mbinguni, kikiwa kimekaliwa na mtu.
3 And he who sat was in appearance like a jasper stone and a sardius; and there was a rainbow around the throne like in appearance to an emerald.
Aliyekuwa amekikalia alikuwa anaonekana kama yaspi na akiki. Kukizunguka kile kiti cha enzi palikuwa na upinde wa mvua ulioonekana kama zumaridi.
4 And around the throne were twenty-four thrones; and upon the thrones I saw the twenty-four elders sitting, clothed in white garments, and on their heads crowns of gold.
Kukizunguka hicho kiti cha enzi palikuwa na viti vingine vya enzi ishirini na vinne, na juu ya hivyo viti walikuwa wameketi wazee ishirini na wanne. Walivaa mavazi meupe, na walikuwa na taji za dhahabu vichwani mwao.
5 And out of the throne proceed lightnings, and voices and thunders; and there were seven lamps of fire burning before the throne, which are the seven spirits of God;
Kwenye kile kiti cha enzi palikuwa panatoka miali ya umeme wa radi, ngurumo na sauti za radi. Mbele ya kiti cha enzi, taa saba zilikuwa zinawaka. Hizi ndizo roho saba za Mungu.
6 and before the throne there was as it were a sea of glass like to crystal; and in the middle before the throne, and around the throne, were four living creatures full of eyes before and behind.
Pia mbele ya kiti cha enzi palikuwa na kile kilichoonekana kama bahari ya kioo, iliyokuwa angavu kama bilauri. Katikati, kukizunguka kile kiti cha enzi, kulikuwa na viumbe wanne wenye uhai, wakiwa wamejawa na macho mbele na nyuma.
7 And the first living creature was like a lion, and the second living creature like a calf, and the third living creature had the face of a man, and the fourth living creature was like a flying eagle.
Kiumbe wa kwanza mwenye uhai alikuwa kama simba, wa pili alikuwa kama ngʼombe dume, wa tatu alikuwa na uso kama wa mwanadamu, na wa nne alikuwa kama tai anayeruka.
8 And the four living creatures, having each of them six wings, around and within are full of eyes; and they have no rest day and night, saying, Holy, holy, holy, Lord God Almighty, who was, and who is, and who is to come.
Kila mmoja wa hawa viumbe wanne wenye uhai alikuwa na mabawa sita, na kujawa na macho pande zote hadi chini ya mabawa. Usiku na mchana hawaachi kusema:
9 And when the living creatures give glory, and honor, and thanksgiving to him that sitteth on the throne, who liveth for ever and ever, (aiōn g165)
Kila mara viumbe hao wanne wenye uhai wanapomtukuza, kumheshimu na kumshukuru yeye aketiye kwenye kile kiti cha enzi, tena aishiye milele na milele, (aiōn g165)
10 the twenty-four elders fall down before him that sitteth on the throne, and worship him that liveth for ever and ever, and cast their crowns before the throne, saying, (aiōn g165)
wale wazee ishirini na wanne huanguka mbele zake aketiye kwenye kiti cha enzi na kumwabudu yeye aliye hai milele na milele. Huziweka taji zao mbele ya kiti cha enzi, wakisema: (aiōn g165)
11 Worthy art thou, O Lord, and our God, to receive the glory, and the honor, and the power; for thou didst create all things, and on account of thy will they were, and were created.
“Bwana wetu na Mungu wetu, wewe unastahili kupokea utukufu na heshima na uweza, kwa maana ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa mapenzi yako viliumbwa na vimekuwako.”

< Revelation 4 >